RIADHA Tanzania (RT) imetangaza majina 23 kwa ajili ya kuunda timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 kwa ajili ya kushiriki katika mashindano ya Kanda ya Tano ya Afrika yatakayofanyika jijini Dar es Salaam mapema mwezi ujao.
Baadhi ya wanariadha walioshiriki walitoka katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Arusha na Manyara, ambapo shule ya Filbert Bayi iliyopo mkoani Pwani, imeto wachezaji watano katika timu ya wasichana kutokana na umahiri wao.
0 Comments