Simbu Ateka Mitaa ya Jiji la Dar es Salaam

September 24, 2025


WhatsApp%20Image%202025-09-23%20at%2019.48.18

WhatsApp%20Image%202025-09-23%20at%2019.48.19

WhatsApp%20Image%202025-09-23%20at%2019.48.22

WhatsApp%20Image%202025-09-23%20at%2019.48.25

WhatsApp%20Image%202025-09-23%20at%2019.48.25%20(1)

WhatsApp%20Image%202025-09-23%20at%2019.48.17


Na Tullo Chambo, Riadha Tanzania.

MWANARIADHA wa Kimataifa wa Tanzania, Bingwa wa Dunia Marathon,   Sajenti Alphonce Simbu, amekuwa kivutio kikubwa kwa wananchi mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam, mara aliporejea nchini akitokea Tokyo Japan.

Simbu, Septemba 16 mwaka huu, aliandika historia baada ya kuibuka Bingwa wa Dunia Marathon akitumia saa 2:09:48.03 katika Mashindano ya Dunia 'World Athletics Championship 2025 Tokyo Japan na kuwa Mtanzania wa kwanza kutwaa medali ya dhahabu katika mashindano hayo makubwa kabisa duniani.

Simbu akiambatana na Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Rogath John na Kocha Denis Malle,  alirejea nchini alfajiri ya Septemba 23  na kupata mapokezi makubwa yaliyoongozwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha sambamba na Naibu Mkurugenzi wa Michezo Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Luteni Kanali Penina Igwe.

Mara baada kuwasili, Simbu alipata mapumziko katika hoteli ya Blue Saphire Vingunguti na majira ya saa 4 asubuhi akiwa katika gari maalumu na msafara wa magari kadhaa ukiongozwa na Polisi wa Jeshi (MP), ulizunguka katika mitaa mbalimbali ya Dar es Salaam na kupita maeneo ya Karume, Kariakoo (Mzunguko wa Msimbazi), Mnazi Mmoja, Posta Mpya, Bandarini hadi hoteli ya Tiffany Diamond.

Simbu akiwa na medali yake ya dhahabu, akiwa juu ya gari akiwapungia wananchi waliokuwa pembezoni mwa barabara ambao walikuwa wamejaa shangwehuku wengine wakipigana vikumbo kumshika mkono na wengine kupiga naye picha huku wakimpongeza.

Kufika barabara ya Morogoro  msafara wa Simbu ulipita mbele ya Shule ya Msingi Mtendeni ambapo wanafunzi walishindwa kujizuia na kupanda ukuta ili kumshuhudia.

Kivutio kingine alikuwa mwananchi mmoja mlemavu wa miguu, ambaye alikuwa amepandwa na hisia kali akitamani naye kumshika mkono Simbu, lakini akawa anashindwa kumfikia juu ya gari, kabla msamaria mmoja kumnyanyua na hatimaye kufanikisha azma yake ya kusalimiana na Bingwa huyo wa Dunia kwa staili ya kugonga naye 'tano'.

Msafara huo wa Simbu, pia ulipambwa na burudani ya matarumbeta kutoka kikundi cha Jeshi, ambacho kilikuwa burudani ya aina yake.
Hafla maalumu ya Simbu, inatarajiwa kufanyika Septemba 27 mwaka huu.

Joseph Panga Apokelewa na Viongozi wa Mkoa wa Arusha

September 23, 2025

 

Mwanariadha Joseph T. Panga apokelewa na Viongozi waandamizi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mkoa wa Arusha Babu Gerald (Mwenye Koti la Suti) katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro baada ya kushika nafasi ya tisa kwa muda wa saa mbili , dakika tisa na sekunde thelathini na tano (2:09:35) katika mashindano ya Berlin Marathon 2025




Simbu takes Tanzania's first global title with marathon victory in Tokyo

September 15, 2025

 







Alphonce Felix Simbu made history on Monday (15), becoming the first athlete from Tanzania to win a global title by claiming gold in the men's marathon at the World Athletics Championships Tokyo 25.

He achieved the feat in style – with the smallest winning margin ever in a global championships marathon, having outsprinted Germany's Amanol Petros in the closing stages to finish just 0.03 ahead.

One of only two athletes representing Tanzania at the World Championships, Simbu was always in contention. He kicked in the closing 30 metres and with victory, he upgraded the world bronze medal he won in 2017 to gold.

“Today means celebrations in Tanzania,” he said. “We have written new history as a country. It was my dream. I am at peace. It is about discipline, training and never giving up.

“After 2017 I have been trying to win another medal but failed at it. Last year Paris was a challenge and this year I told myself: I will try my best. I did different types of training under different weather conditions.”

Simbu and Petros were both credited with the same time: 2:09:48.

“I have never seen something like this in the marathon – both races (men and women) came down to a sprint finish. It's like the 100m,” said Petros.

“This is four months of hard work in training – running, eating and sleeping. It was hard. But this silver gives me energy and bigger motivation that I can win bigger competitions. I was so sure I was winning, he (Simbu) surprised me. He kicked like crazy. I accept I lost today but tomorrow I can win. Today is a learning experience.”

Italy’s Iliass Aouani took bronze in 2:09:53.

“I am proud and happy about the way I conducted the race,” he said. “I was relaxed at the end and pushed through, but the other guys had more legs than me. It means a lot. This is a hard sport, people do not know that behind this medal are a lot of frustrations, a lot of bad races, missed opportunities.”

Kenya’s Vincent Ngetich took an early lead, with all the athletes grouped together. He led through 5km in 15:22, followed closely by athletes including Petros, Simbu and Aouani, plus Abel Chelangat, Isaac Mpofu, Sondre Moen, Suldan Hassan, Deresa Geleta and Stephen Kissa.

In the hot and humid conditions, athletes cooled themselves with ice and sponges, even passing them to each other.

Ngetich, running on the edge of the course, slightly increased the pace, with Chelangat and Kissa close behind. The leading pack briefly scattered before regrouping.

At Akihabara turn, Ngetich pushed the pace again, but Germany’s Richard Ringer took over and led the group through 10km in 30:48, alongside defending champion Victor Kiplangat, Chelangat, Petros, Simbu, Ngetich and Mohamed Reda El Aaraby. 

The leading roles kept changing, with Morocco’s El Aaraby taking over before Ethiopia’s Tadese Takele – this year’s Tokyo Marathon champion – surged ahead. Ngetich again took the lead through the Ginza turn.

Kiplangat then grabbed a cooler and moved to the front, pushing the pace downhill. Sweden’s Hassan led a group of more than 20 runners through 20km in 1:01:54 but Kiplangat remained in control at the halfway point (1:05:19), followed by the likes of Hassan, Geleta, Kissa, Elroy Gelant and Kipkoech.

Geleta took a turn at the front, leading the pack through 30km in 1:32:27, but it was Kiplangat who surged at 33km – leading for around 6km before falling back and out of contention.

Meanwhile, his compatriot Chelangat took the lead, followed by a series of challengers – all in single file. Soon, the lead group was down to five.

As the race wound up, Chelangat and Haimro Alame dropped back, leaving Aouani, Petros and Simbu to battle for the gold. With the stadium in sight, Simbu nearly went off course.

Once inside, Petros surged with 200 metres to go, with Simbu in pursuit. Petros glanced back twice and the world title came down to a photo finish. Both were timed at 2:09:48, separated by just three hundredths of a second.

“When we entered the stadium, I was not sure if I would win. I did not know if I won. But when I saw the video screens and me on the top of the results, I felt relieved,” said Simbu.

“Before this event, I was training in Tanzania, and the conditions there helped me to win this race. I remember, when I was in Paris last year (at the Olympics), it was very challenging for me – the hills, all ups and downs. So, before Tokyo, I decided to train on different surfaces. Sometimes I went to hills, and that is what made the difference here. I had many tough moments during the race, but I told myself that I would never give up.”

Credit : Michelle Katami for World Athletics

Alphonce Felix Simbu is Ready for World Championships Tokyo 2025

September 14, 2025

 


The Kit for Alphonce Felix Simbu, Ready for the Race, World Athletics Championships Tokyo 2025 Japan,  Sponsored by Xtep Gears

Simbu , Gisemo Kuipeperusha Bendera ya Tanzania Tokyo Japan.

September 14, 2025

 

Wanariadha wa Kimataifa , Alphonce Felix Simbu na Josephat Joshua Gisemo kuipeperusha Bendera ya Tanzania leo Usiku kwenye Mashindano ya Dunia (World Championships 2025) ya Riadha huko Tokyo Japan.

Bofya Hapa kwa Maelezo Zaidi

RT Kuwabana Waandaaji wa Mbio

August 20, 2025


WhatsApp%20Image%202025-08-20%20at%2015.09.17


SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT) limepanga kuweka sheria mpya itakayowalazimisha wandaaji wa mashindano kuhakikisha wanajumuisha pia mbio za watoto katika kila tukio litakaloandaliwa.


Hatua hiyo inalenga kujenga msingi imara wa vipaji na kuwekeza mapema kwenye maendeleo ya riadha nchini.


Rais mpya wa RT, Rogath John Stephen Akhwari, alisema mpango huo utahusisha kuandaa mashindano maalumu ya watoto na vijana kwa kila kanda, yakiratibiwa kwa kushirikiana na vyama vya mikoa ili kuhakikisha kunakuwepo mtiririko wa mashindano kuanzia ngazi ya chini.


Akhwari alibainisha kuwa wapo mbioni kuandaa kanuni mpya za kusimamia mbio za barabarani, ambapo kutakuwa na utaratibu wa kutofautisha mashindano ya kimaifa yatakayosimamiwa na RT moja kwa moja na yale ya ndani yenye malengo ya kitaifa, kwa lengo la kuongeza ubora na hadhi ya riadha nchini.


“Hizi mbio itakuwa ni lazima, siyo chaguo tunataka kuboresha kanuni zetu na yeyote atakayehitaji kibali cha kuandaa mashindano atalazimika kuhakikisha mbio za watoto pia zitakuwepo,” alisema Akhwari.


Alieleza watapeleka wataalamu waliobobea ili kusaidia wandaaji kuelewa namna sahii ya kuandaa mashindano ya watoto, akisisitiza kuwa changamoto kubwa iliyokuwepo awali ni watoto kukimbia mbio ndefu zisizolingana na umri wao.


"Watoto wetu wamekuwa wakikosa fursa hizi, kwa sababu mara nyingi wakipewa mbio wanakimbizwa umbali wa kilometa tano, hapo awali tulivumilia kwa sababu tulikuwa hatuna mfumo madhubuti lakini sasa tunataka kubadilisha hilo,” aliongeza.


Aidha kabla ya sheria mpya kupitishwa, RT imesema itatoa elimu kwa wandaaji wote wa mbio, kisha kuwapa muda wa maandalizi kabla ya utekelezaji rasmi.


Akhwari anasema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa kuhakikisha riadha Tanzania inakua kwa kuanzia watoto, vijana hadi kuzalisha wanariadha wa kiwango cha kimataifa.


Imeandaliwa na Mwananchi Communications Limited

MAPOKEZI YA RAIS WA RT ROGATH JOHN STEPHEN AKHWARI JIJINI ARUSHA

August 18, 2025

 

Kocha Mwingereza akimpongeza rais wa shirkisho la Riadha Tanzania -RT Kocha Rogath John Stephen Akhwari wakati wa mapokezi katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha Leo.

Mke wa Rogath John (katikati mwenye jaketi jekundu) akimpongeza mume wake kwa kuchaguliwa kuwa rais wa shirikisho la Riadha Tanzania -RT wakati wa mapokezi katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha Leo.
Rais wa shirikisho la Riadha Tanzania -RT Kocha Rogath John Stephen Akhwari Akiwashukuru Watanzania wote kwa Kumuombea na hatimaye kuchaguliwa kuwa rais , pia amechukua nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mchango wake kwenye michezo.


Na John Mhala, Arusha.

ARUSHA: Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Rogath John Stephen Akhwari amesema safari ya kuendeleza mchezo wa riadha ndio imeanza kwani shirikisho hilo litaanzisha rasmi mbio za watoto na vijana lengo ni kuwatayarisha wenye umri huo kuwa kurithi mikoba ya wanariadha wanaojiandaa kustaafu.

Stephen amesema hayo leo alfajiri alipowasili jijini Arusha akitokea Mwanza baada ya kuchaguliwa na wajumbe wa RT kuwa Rais wa Shirikisho hilo na kusema kuwa wakati umefika sasa wa kuwaandaa watoto na vijana kushiriki mchezo wa riadha ili waweze kushika nafasi za akina Alphonce Simbu ,Magdalena Shauri,Jackline Sakilu na Gabriel Geay watakapostaafu.

Amesema RT lazima ijiandae kwa kuwaanda watoto na vijana ili waupende mchezo huo na hatimaye waweze kufanya vizuri kitaifa na kimataifa ikiwa ni pamoja na kushika zile nafasi walizofanya vizuri wanariadha wenzao hivyo wale wote wanaoanzisha na walioanzisha mbio kote nchini kipaumbele ni kuanzisha mbio za watoto na vijana mara moja kwani ndio lengo la msingi la kukuza mchezo huo unapendwa kwa sasa hapa nchini.

Rais huyo amesema ajira kwa sasa ni ngumu iwe ndani ya serikali na nje ya serikali na ajira nzuri ni mchezo wa riadha hivyo aliwaasa wazazi kuwapa ushirikiano watoto na vijana kujikita katika mchezo huo kwani una pesa nyingi kwa muda mfupi na kutoa mfano Simbu aliposhinda mbio za Boston amepata fedha nyingi ambazo hata waziri akistaafu serikali hawezi kuzipata.

Rogath ambaye mwajiriwa wa jeshi la Polisi nchini na kituo chake cha kazi Polisi Kati Arusha kwa cheo cha Mrakibu Msaidizi Mwandamizi (ASP) alimshukuru sana Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Inspekta General wa Polisi, Camilius Wambura kwa kumpa baraka za kuchukua fomu za kuwania kinyang’anyanyiro hicho na hatimaye kushinda urais.

CRDB BANK MARATHON YAFANYIKA DAR

August 17, 2025


Dar es Salaam, 17 Agosti 2025 - Maelfu ya wakimbiaji na wapenda michezo kutoka ndani na nje ya Tanzania wamejitokeza leo katika viwanja vya The Green, Oysterbay, kushiriki CRDB Bank Marathon 2025, mbio za hisani ambazo mwaka huu zimekusanya Shilingi Bilioni 2 ili kusaidia matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo, wakinamama wenye ujauzito hatarishi, na vijana kupitia programu ya iMBEJU.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mwansasu, aliongoza maelfu ya washiriki kwenye msimu huu wa sita wa CRDB Bank Marathon. 
Akitoa salamu zake, Dkt. Tulia alipongeza ubunifu wa CRDB Bank Foundation katika kuunganisha jamii kupitia michezo na kusaidia wenye uhitaji, akieleza kuwa mbio hizo ni mfano wa vitendo vya huruma vinavyogusa maisha ya wengi. 
 
“Ushiriki wetu katika CRDB Bank Marathon ni tendo la huruma linaloleta faraja kwa watoto na wakinamama na familia zao. Ni ushahidi kwamba tukishirikiana, tunaweza kubadilisha maisha,” alisema.
Akitoa salamu zake, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, aliipongeza Benki ya CRDB na CRDB Bank Foundation kuendelea kuandaa mbio hizo. 
 
Alisema, “CRDB Bank Marathon si tu imekuwa ikikuza afya na mshikamano wa kijamii, bali pia imekuwa ikifungua milango ya ajira na fursa za kiuchumi kwa vijana wetu. Michezo ni sekta inayoweza kubadili maisha, na ninapongeza sana kitendo cha kuweka zawadi nono kwa washindi. Hizi ni fursa ambazo zinaweza kuwa mtaji wa kuanzisha biashara na kuimarisha maisha ya vijana wetu. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau kama CRDB Bank Foundation kuhakikisha michezo inakuwa chachu ya maendeleo ya taifa.”
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alibainisha kuwa msimu wa sita wa CRDB Bank Marathon umefanyika sambamba na maadhimisho ya miaka 30 ya Benki ya CRDB, na kuendelea kupanua wigo wa matokeo yake ndani na nje ya Tanzania. Kwa mara ya pili, mbio hizi zimefanyika pia nchini Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), zikikusanya fedha kwa ajili ya miradi ya afya na ustawi wa jamii katika nchi hizo. 

Nsekela alisema kuwa mbio za mwaka huu zimeweza kuvutia zaidi ya washiriki 16,000, na kufanikisha lengo la kukusanya shilingi bilioni 2 ambapo pamoja na kusaidia maandalizi ya mbio hizo, shilingi milioni 450, zimeelekezwa kusaidia wenye uhitaji katika jamii. 
 
Kati ya hizo shilingi milioni 100 zimekwenda hospitali ya CCBRT kusaidia wakinama wenye ujauzito hatarishi kujifungua salama, shilingi milioni 100 zimekwenda Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kusaidia upasuaji wa Watoto wenye matatizo ya moyo, na shilingi 250 zitaelekezwa katika uwezeshaji wa vijana.
Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya mbio hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa, alieleza kuwa safari ya msimu wa sita imeanzia Lubumbashi, DRC, ambako zilikusanywa Dola za Marekani 70,000 kwa ajili ya kuboresha huduma za afya katika hospitali ya Jeshi la Ruashi, na kuendelea Bujumbura, Burundi, ambapo zilipatikana Faranga za Burundi milioni 175 kusaidia bima ya afya kwa zaidi ya watu 58,000 wasiojiweza. 
 
Mwambapa alisisitiza kuwa mafanikio haya ni matokeo ya mshikamano wa kipekee wa serikali za nchi shiriki, wadhamini na washiriki, akiwashukuru wadau wote waliotoa jitokeza kuchangia ikiwamo kampuni za bima za Sanlam Life na Alliance Life ambao wamekuwa sehemu ya mbio hizi tangu kuanzishwa kwake.
Washindi wa mbio za mwaka huu upande wa Tanzania kwa Kilometa 42 upande wa wanawake ni Joyloyce Kemuma kutoka Kenya, upande wa wanaume mshindi ni Abraham Kiptum kutoka Kenya. Kilometa 21 upande wa wanawake ni Catherine Syokau kutoka Kenya, na upande wa wanaume ni Joseph Panga kutoka Tanzania. Kilometa 10 upande wa wanawake ni Silia Ginoka kutoka Tanzania, na upande wa wanaume ni Boayi Maganga kutoka Tanzania.
 
Joseph Panga mshindi wa mbio za Kilometa 21 upande wa wanawake ameeleza furaha yake kushiriki katika mbio hizo na kusema kuwa ushindi wake ni sehemu ya kusaida matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo na matibabu ya wakinamama wenye ujauzito hatarishi hospitali ya CCBRT. 
 
“Mimi kama Mtanzania najisikia fahari kubwa kushiriki kusambaza tabasamu kwa watoto na wakinamama. Ni muhimu watu kufahamu kuwa afya bora ni haki ya kila mtoto, na hakuna mama anayestahili kupoteza maisha wakati wa kujifungua. Tunawashukuru CRDB Bank Foundation kwa kutuleta pamoja katika harakati hizi za kuokoa maisha,” amesema.
CRDB Bank Marathon imekuwa jukwaa muhimu la kuchochea ustawi wa kijamii katika ukanda huu wa Afrika ya Mashariki na kati hivi karibuni ikipata heshima ya kutambuliwa kimataifa kwa kushinda tuzo ya jukwaa bora la taasisi za fedha katika kusaidia kusaidia jamii.

ROGATH JOHN STEPHEN AKHWARI ACHAGULIWA KUWA RAIS WA SHIRIKISHO LA RIADHA TANZANIA

August 17, 2025

 

Kocha wa Polisi Tanzania na Katibu Mkuu wa Riadha Chama cha Mkoa wa Arusha Rogath John Stephen Akhwari amechaguliwa na wajumbe kuwa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania huko Mwanza tarehe 16/08/2025 kwa kupata Kura 27 kati ya 47 na mpinzani wake Bw. Nsolo Malongo Mlozi kupata kura 20. 
Wakili Jackson Beda Ndaweka Achaguliwa kuwa Makamu wa Shirikisho la Riadha Tanzania -RT , baada ya kuitumikia shirikisho la riadha Tanzania kama Kaimu Katibu Mkuu kwa Muda mrefu.

 

Copyright © 2015 - 2025 Athletics Tanzania All Right Reserved

Developed by Gadiola Emanuel
Theme By AP | Developed By Gadiola Emanuel