Showing posts with label Matukio. Show all posts
Showing posts with label Matukio. Show all posts

Joseph Panga Apokelewa na Viongozi wa Mkoa wa Arusha

September 23, 2025

 

Mwanariadha Joseph T. Panga apokelewa na Viongozi waandamizi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mkoa wa Arusha Babu Gerald (Mwenye Koti la Suti) katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro baada ya kushika nafasi ya tisa kwa muda wa saa mbili , dakika tisa na sekunde thelathini na tano (2:09:35) katika mashindano ya Berlin Marathon 2025




RT Kuwabana Waandaaji wa Mbio

August 20, 2025


WhatsApp%20Image%202025-08-20%20at%2015.09.17


SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT) limepanga kuweka sheria mpya itakayowalazimisha wandaaji wa mashindano kuhakikisha wanajumuisha pia mbio za watoto katika kila tukio litakaloandaliwa.


Hatua hiyo inalenga kujenga msingi imara wa vipaji na kuwekeza mapema kwenye maendeleo ya riadha nchini.


Rais mpya wa RT, Rogath John Stephen Akhwari, alisema mpango huo utahusisha kuandaa mashindano maalumu ya watoto na vijana kwa kila kanda, yakiratibiwa kwa kushirikiana na vyama vya mikoa ili kuhakikisha kunakuwepo mtiririko wa mashindano kuanzia ngazi ya chini.


Akhwari alibainisha kuwa wapo mbioni kuandaa kanuni mpya za kusimamia mbio za barabarani, ambapo kutakuwa na utaratibu wa kutofautisha mashindano ya kimaifa yatakayosimamiwa na RT moja kwa moja na yale ya ndani yenye malengo ya kitaifa, kwa lengo la kuongeza ubora na hadhi ya riadha nchini.


“Hizi mbio itakuwa ni lazima, siyo chaguo tunataka kuboresha kanuni zetu na yeyote atakayehitaji kibali cha kuandaa mashindano atalazimika kuhakikisha mbio za watoto pia zitakuwepo,” alisema Akhwari.


Alieleza watapeleka wataalamu waliobobea ili kusaidia wandaaji kuelewa namna sahii ya kuandaa mashindano ya watoto, akisisitiza kuwa changamoto kubwa iliyokuwepo awali ni watoto kukimbia mbio ndefu zisizolingana na umri wao.


"Watoto wetu wamekuwa wakikosa fursa hizi, kwa sababu mara nyingi wakipewa mbio wanakimbizwa umbali wa kilometa tano, hapo awali tulivumilia kwa sababu tulikuwa hatuna mfumo madhubuti lakini sasa tunataka kubadilisha hilo,” aliongeza.


Aidha kabla ya sheria mpya kupitishwa, RT imesema itatoa elimu kwa wandaaji wote wa mbio, kisha kuwapa muda wa maandalizi kabla ya utekelezaji rasmi.


Akhwari anasema hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa kuhakikisha riadha Tanzania inakua kwa kuanzia watoto, vijana hadi kuzalisha wanariadha wa kiwango cha kimataifa.


Imeandaliwa na Mwananchi Communications Limited

MAPOKEZI YA RAIS WA RT ROGATH JOHN STEPHEN AKHWARI JIJINI ARUSHA

August 18, 2025

 

Kocha Mwingereza akimpongeza rais wa shirkisho la Riadha Tanzania -RT Kocha Rogath John Stephen Akhwari wakati wa mapokezi katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha Leo.

Mke wa Rogath John (katikati mwenye jaketi jekundu) akimpongeza mume wake kwa kuchaguliwa kuwa rais wa shirikisho la Riadha Tanzania -RT wakati wa mapokezi katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha Leo.
Rais wa shirikisho la Riadha Tanzania -RT Kocha Rogath John Stephen Akhwari Akiwashukuru Watanzania wote kwa Kumuombea na hatimaye kuchaguliwa kuwa rais , pia amechukua nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mchango wake kwenye michezo.


Na John Mhala, Arusha.

ARUSHA: Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Rogath John Stephen Akhwari amesema safari ya kuendeleza mchezo wa riadha ndio imeanza kwani shirikisho hilo litaanzisha rasmi mbio za watoto na vijana lengo ni kuwatayarisha wenye umri huo kuwa kurithi mikoba ya wanariadha wanaojiandaa kustaafu.

Stephen amesema hayo leo alfajiri alipowasili jijini Arusha akitokea Mwanza baada ya kuchaguliwa na wajumbe wa RT kuwa Rais wa Shirikisho hilo na kusema kuwa wakati umefika sasa wa kuwaandaa watoto na vijana kushiriki mchezo wa riadha ili waweze kushika nafasi za akina Alphonce Simbu ,Magdalena Shauri,Jackline Sakilu na Gabriel Geay watakapostaafu.

Amesema RT lazima ijiandae kwa kuwaanda watoto na vijana ili waupende mchezo huo na hatimaye waweze kufanya vizuri kitaifa na kimataifa ikiwa ni pamoja na kushika zile nafasi walizofanya vizuri wanariadha wenzao hivyo wale wote wanaoanzisha na walioanzisha mbio kote nchini kipaumbele ni kuanzisha mbio za watoto na vijana mara moja kwani ndio lengo la msingi la kukuza mchezo huo unapendwa kwa sasa hapa nchini.

Rais huyo amesema ajira kwa sasa ni ngumu iwe ndani ya serikali na nje ya serikali na ajira nzuri ni mchezo wa riadha hivyo aliwaasa wazazi kuwapa ushirikiano watoto na vijana kujikita katika mchezo huo kwani una pesa nyingi kwa muda mfupi na kutoa mfano Simbu aliposhinda mbio za Boston amepata fedha nyingi ambazo hata waziri akistaafu serikali hawezi kuzipata.

Rogath ambaye mwajiriwa wa jeshi la Polisi nchini na kituo chake cha kazi Polisi Kati Arusha kwa cheo cha Mrakibu Msaidizi Mwandamizi (ASP) alimshukuru sana Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Inspekta General wa Polisi, Camilius Wambura kwa kumpa baraka za kuchukua fomu za kuwania kinyang’anyanyiro hicho na hatimaye kushinda urais.

CRDB BANK MARATHON YAFANYIKA DAR

August 17, 2025


Dar es Salaam, 17 Agosti 2025 - Maelfu ya wakimbiaji na wapenda michezo kutoka ndani na nje ya Tanzania wamejitokeza leo katika viwanja vya The Green, Oysterbay, kushiriki CRDB Bank Marathon 2025, mbio za hisani ambazo mwaka huu zimekusanya Shilingi Bilioni 2 ili kusaidia matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo, wakinamama wenye ujauzito hatarishi, na vijana kupitia programu ya iMBEJU.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mwansasu, aliongoza maelfu ya washiriki kwenye msimu huu wa sita wa CRDB Bank Marathon. 
Akitoa salamu zake, Dkt. Tulia alipongeza ubunifu wa CRDB Bank Foundation katika kuunganisha jamii kupitia michezo na kusaidia wenye uhitaji, akieleza kuwa mbio hizo ni mfano wa vitendo vya huruma vinavyogusa maisha ya wengi. 
 
“Ushiriki wetu katika CRDB Bank Marathon ni tendo la huruma linaloleta faraja kwa watoto na wakinamama na familia zao. Ni ushahidi kwamba tukishirikiana, tunaweza kubadilisha maisha,” alisema.
Akitoa salamu zake, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, aliipongeza Benki ya CRDB na CRDB Bank Foundation kuendelea kuandaa mbio hizo. 
 
Alisema, “CRDB Bank Marathon si tu imekuwa ikikuza afya na mshikamano wa kijamii, bali pia imekuwa ikifungua milango ya ajira na fursa za kiuchumi kwa vijana wetu. Michezo ni sekta inayoweza kubadili maisha, na ninapongeza sana kitendo cha kuweka zawadi nono kwa washindi. Hizi ni fursa ambazo zinaweza kuwa mtaji wa kuanzisha biashara na kuimarisha maisha ya vijana wetu. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau kama CRDB Bank Foundation kuhakikisha michezo inakuwa chachu ya maendeleo ya taifa.”
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alibainisha kuwa msimu wa sita wa CRDB Bank Marathon umefanyika sambamba na maadhimisho ya miaka 30 ya Benki ya CRDB, na kuendelea kupanua wigo wa matokeo yake ndani na nje ya Tanzania. Kwa mara ya pili, mbio hizi zimefanyika pia nchini Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), zikikusanya fedha kwa ajili ya miradi ya afya na ustawi wa jamii katika nchi hizo. 

Nsekela alisema kuwa mbio za mwaka huu zimeweza kuvutia zaidi ya washiriki 16,000, na kufanikisha lengo la kukusanya shilingi bilioni 2 ambapo pamoja na kusaidia maandalizi ya mbio hizo, shilingi milioni 450, zimeelekezwa kusaidia wenye uhitaji katika jamii. 
 
Kati ya hizo shilingi milioni 100 zimekwenda hospitali ya CCBRT kusaidia wakinama wenye ujauzito hatarishi kujifungua salama, shilingi milioni 100 zimekwenda Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kusaidia upasuaji wa Watoto wenye matatizo ya moyo, na shilingi 250 zitaelekezwa katika uwezeshaji wa vijana.
Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya mbio hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa, alieleza kuwa safari ya msimu wa sita imeanzia Lubumbashi, DRC, ambako zilikusanywa Dola za Marekani 70,000 kwa ajili ya kuboresha huduma za afya katika hospitali ya Jeshi la Ruashi, na kuendelea Bujumbura, Burundi, ambapo zilipatikana Faranga za Burundi milioni 175 kusaidia bima ya afya kwa zaidi ya watu 58,000 wasiojiweza. 
 
Mwambapa alisisitiza kuwa mafanikio haya ni matokeo ya mshikamano wa kipekee wa serikali za nchi shiriki, wadhamini na washiriki, akiwashukuru wadau wote waliotoa jitokeza kuchangia ikiwamo kampuni za bima za Sanlam Life na Alliance Life ambao wamekuwa sehemu ya mbio hizi tangu kuanzishwa kwake.
Washindi wa mbio za mwaka huu upande wa Tanzania kwa Kilometa 42 upande wa wanawake ni Joyloyce Kemuma kutoka Kenya, upande wa wanaume mshindi ni Abraham Kiptum kutoka Kenya. Kilometa 21 upande wa wanawake ni Catherine Syokau kutoka Kenya, na upande wa wanaume ni Joseph Panga kutoka Tanzania. Kilometa 10 upande wa wanawake ni Silia Ginoka kutoka Tanzania, na upande wa wanaume ni Boayi Maganga kutoka Tanzania.
 
Joseph Panga mshindi wa mbio za Kilometa 21 upande wa wanawake ameeleza furaha yake kushiriki katika mbio hizo na kusema kuwa ushindi wake ni sehemu ya kusaida matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo na matibabu ya wakinamama wenye ujauzito hatarishi hospitali ya CCBRT. 
 
“Mimi kama Mtanzania najisikia fahari kubwa kushiriki kusambaza tabasamu kwa watoto na wakinamama. Ni muhimu watu kufahamu kuwa afya bora ni haki ya kila mtoto, na hakuna mama anayestahili kupoteza maisha wakati wa kujifungua. Tunawashukuru CRDB Bank Foundation kwa kutuleta pamoja katika harakati hizi za kuokoa maisha,” amesema.
CRDB Bank Marathon imekuwa jukwaa muhimu la kuchochea ustawi wa kijamii katika ukanda huu wa Afrika ya Mashariki na kati hivi karibuni ikipata heshima ya kutambuliwa kimataifa kwa kushinda tuzo ya jukwaa bora la taasisi za fedha katika kusaidia kusaidia jamii.

ROGATH JOHN STEPHEN AKHWARI ACHAGULIWA KUWA RAIS WA SHIRIKISHO LA RIADHA TANZANIA

August 17, 2025

 

Kocha wa Polisi Tanzania na Katibu Mkuu wa Riadha Chama cha Mkoa wa Arusha Rogath John Stephen Akhwari amechaguliwa na wajumbe kuwa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania huko Mwanza tarehe 16/08/2025 kwa kupata Kura 27 kati ya 47 na mpinzani wake Bw. Nsolo Malongo Mlozi kupata kura 20. 
Wakili Jackson Beda Ndaweka Achaguliwa kuwa Makamu wa Shirikisho la Riadha Tanzania -RT , baada ya kuitumikia shirikisho la riadha Tanzania kama Kaimu Katibu Mkuu kwa Muda mrefu.

TIMU YA TAIFA YA RIADHA YAAGWA, KUSHIRIKI MASHINDANO YA “13TH ALL AFRICAN GAMES” ACCRA , GHANA.

March 17, 2024


 Timu ya Taifa ya Riadha Imeagwa na Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania Silas Isangi na Kaimu katibu mkuu Wakili Jackson Ndaweka katika uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro Leo tarehe 14/03/2024. 

Wanariadha 8 wakiwemo wa Mbio za Uwanjani, Mbio ndefu na Mrusha mkuki, wameondoka kwenda Accra , Ghana kushiriki mashindano ya Afrika “All African Games” ambayo yalianza toka tarehe 8 Machi hadi 23 Machi 2024.

Hapa Wakiwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid , na makocha na viongozi wao kufanya Majaribio "Trials" kabla ya kwenda Ghana.

hapa wanariadha na makocha wakiwa Kambini, Ngaramtoni, Arusha.

Mwanariadha Andrew Rhobi amepata muda wake Bora

March 10, 2024

 

Copyright @gettyimages

Hongera kwa Andrew Boniface Rhobi kutoka jeshi la polisi Tanzania kwa kupata muda wako bora wa dakika tatu na sekunde hamsini na moja ( 3:51.44) yaani ( Personal Best) mita 1500 (1500M) na kuwa nafasi ya Saba kwenye heat ya kwanza, kwenye Mashindano ya Dunia ya Ndani ( World Athletics indoors Championships Glasgow 2024) tarehe 1-3 Machi 2024, huko Glasgow, Scotland.

GEAY 'AKICHAFUA' MBEYA TULIA MARATHON 2023

May 06, 2023


 

BINGWA wa Taifa anayeshikilia rekodi ya Marathon Tanzania, Gabriel Gerald Geay amekuwa kivutio kikubwa Mbeya Tulia Marathon, aliposhiriki na kuibuka mshindi katika mbio za mita 1500.

Mbeya Tulia Marathon, imekata utepe Leo Mei 5 kwa mbio za uwanjani, kabla ya kesho Jumamosi Mei 6 kurindima Marathon.

Katika mbio hizo za mita 1500, Geay alianza taratibu raundi ya kwanza akiwa nyuma, kabla ya mzunguko wa pili kupata dhoruba la kuangushwa, lakini alinyanyuka na kukiwasha na hatimaye kuibuka mshindi akitumia dakika 3:58.46.

Geay alifuatiwa na Faraja Damas wa JWTZ aliyetumia dakika 4:00.08 huku nafasi ya tatu ikienda kwa John Joseph pia JWTZ 4:06.25. 

Mashabiki na viongozi mbalimbali waliojitokeza, wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Beno Malisa, walishindwa kujizua kumshangilia Geay wakati akikiwasha katika mbio hizo.

Kwa upande wa wanawake Mita 1500, Magdalena Shauri wa JWTZ, alishinda akitumia dakika 4:31.13 na kufuatiwa na Salma Charles ambaye katoka Zambia na Timu ya Taifa U 18 na 20 iliyoshiriki mashindano ya Afrika, dakika 4:46.55 na wa tatu akiwa ni Mayselina Mbua JWTZ 4:53.16.

Mbali na Geay ambaye katoka kufanya kweli katika mbio kongwe za Boston Marathon nchini Marekani alikoshika nafasi ya pili hivi karibuni, pia mkali mwingine, ambaye pia ni Mshindi wa medali ya Fedha Jumuiya na Mwanamichezo Bora Tuzo za BMT 2022, Alphonce Simbu, naye alikuwepo kushuhudia mbio hizo.

Pia, Timu ya Taifa ya Vijana iliyopumzika hapa ikitokea Ndola Zambia ilikojinyakulia medali mbili katika mashindano ya Afrika, baadhi walipata nafasi ya kushiriki mbio za uwanjani Mbeya Tulia Marathon.

Timu hiyo inatarajiwa kuondoka Mbeya kesho Jumapili kurejea Dar es Salaam.

Pia, mbio hizo zilipambwa program ya watoto 'Kids Athletics', ambayo ilikuwa kivutio kwa watoto wa shule za msingi walioshiriki.

RT YAUONGEZEA THAMANI UWANJA WA BENJAMIN MKAPA, DAR

March 12, 2023

 







 NA TULLO CHAMBO, RT


SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT), kwa ushirikiano na shirikisho la mchezo huo nchini Kenya (AK), wamezindua kifaa maalum cha kupima hali ya hewa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Kifaa hicho ni maalumu kwa ajili ya kupima ubora wa hali ya hewa sehemu husika, kama iko sawa kwa matumizi ya wanamichezo shiriki wakati wa tukio ama haiko sawa.

Ufungaji wa kifaa hicho ni maagizo ya Shirikisho la Riadha la Kimataifa (WA), ambapo Tanzania imekuwa nchi ya nne barani Afrika kupata teknolojia hiyo. 

Akizungumza  wakati wa uzinduzi huo mbele ya Mgeni rasmi Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha, Rais wa AK ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Riadha Ukanda wa Afrika Mashariki (EAAR), Luteni Jenerali mstaafu Jackson Tuwei, alisema kifaa hicho ni muhimu kwani binadamu hata wanyama wanahitaji kuishi katika mazingira ya hali ya hewa safi.

Luteni Jenelari Tuwei, alisema teknolojia hiyo imeanza kutumika nchini Kenya, kisha ilifuatiwa na Dakar Senegal, Addis Ababa Ethiopia na Tanzania imekuwa ni nchi ya nne kufungwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa na badae wanatarajia kufunga kifaa hicho nchini Zambia ambako yanatarajiwa kufanyika mashindano ya vijana Afrika Aprili 27 hadi Mei 3.

Kwa upande wake, Katibu wa BMT, Neema Msitha, alishukuru kwa jambo hilo ambalo linauongezea thamani wa Uwanja wa Benjamin Mkapa kimataifa, na kwamba Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, mbali ya kuipongeza RT kwa kufanikisha jambo hilo lenye manufaa kwa wanamichezo wote watakaokuwa wanautumia uwanja huo, iko tayari kutoa Ushirikiano katika kila  jambo lenye maendeleo kwenye sekta ya michezo na kwamba wadau wote wa michezo wanakaribishwa.

Kifaa hicho kimetengenezwa na taasisi ya mazingira nchini Sweden ijulikanayo kama Stocklohom Environment Instute (SEI).

19 WAPENYA TIMU YA TAIFA VIJANA EAAR

March 05, 2023


Wanariadha wakichuana kwenye mashindano ya Majaribio Jijini Dar es Salaam.

Makamu wa rais wa shirikisho la Riadha la Tanzania, Ndugu William Kallaghe akizungumza na wanariadha waliopenya kwenye timu ya Taifa ya Vijana ya EAAR Dar es Salaam.


NA TULLO CHAMBO, RT

WANARIADHA 19 wamefanikiwa kuchaguliwa timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 18 na 20 itakayoiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Afrika Mashariki (EAAR U 18 & U 20 yanayotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam, kuanzia Machi 9 mwaka huu.
Wanariadha hao wamepatikana kupitia mashindano ya wazi ya Taifa, yaliyofanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es  Salaam Machi 4 mwaka huu, ambayo yaliandaliwa na Shirikisho la Riadha Tanzania (RT).

Jopo la Wataalamu wakiongozwa na Makocha wa Taifa wa timu hiyo, Robert Kalyahe na Mwinga Mwanjala, lilichagua wanariadha hao kutokana na viwango ambavyo wanariadha hao walivionyesha na si kutokana na nafasi walizoshika katika mchezo husika.

Aidha makocha hao, walibainisha kuwa wameshuhudia vipaji vipya vingi wameviona na kama vikiendelezwa vitakuja kuwa lulu kwa Taifa siku zijazo.
Kutokana na vijana hao 19 waliofuzu, wengine nane watajumuishwa nao ambao walifanya vema katika mashindano mengineyo ikiwemo Ladies First yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada kutangazwa timu hiyo mbele ya viongozi wa mikoa iliyoshiriki Tabora, Mbeya, Pwani, Dar es Salaam, Arusha, Morogoro, makocha mbalimbali na Waandaaji wa Matukio ya Riadha 'Race Organizers' (RO's), Makamu wa Rais wa RT, William Kallaghe, aliwapongeza wote waliofanikisha tukio hilo na kubainisha kwamba, kati ya malengo makuu ya shirikisho hivi sasa ni kuwekeza kwa vijana ambao ndio hazina ya kesho ya Taifa.

"Kati ya mikakati mikubwa hivi sasa ya RT ni kwenye mbio za uwanjani....Na hakuna ujanja bali kuwekeza kwa vijana na ndio maana tunawaomba na kuwahimiza wadau kusapoti katika hili.
"Vijana hawa tuliowapata ndo tunaanza nao, hivyo tunawaomba wadau mbalimbali mtuunge mkono katika hili kwa manufaa ya Taifa siku zijazo, na ambao hamkufanikiwa kuingia katika timu hii, msikate tamaa kwani bado nafasi mnayo mzidishe juhudi," alisema Kallaghe na kuongeza.

Timu hiyo itaingia kambini mapema Jumatatu kwenye hosteli za Baraza la Maaskofu (TEC), Kurasini jijini Dar es Salaam.
Wanariadha 19 waliopenya ni pamoja na Siwema Julias, Shija Donald, Salma Samwel, Christina George, Elizabeth Kirario,     Bravo George, Kimena Kibase, Damian Christian, Fedelis Amadi, Baraka Tiluli na Emmanuel Amos.

Wengine ni Elizabeth Ilanda, Gaudensia Maneno, Elia Clement, Nicodemus Joseph, Nelson Mangura, Jackson Sylvester, Dickson Mangura na Malcolm Kazmir.

RT YATEKELEZA MAAGIZO YA BMT

March 05, 2023

 

Kulia ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania RT , Ndugu William Kallaghe akikabidhi ripoti kwa Katibu Mkuu Mtendaji wa BMT, Bi. Neema Msitha Jijini Dar es Salaam.


SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT), Machi 3, 2022, limetekeleza agizo la Baraza la Michezo la Taifa (BMT), baada ya kukabidhi ripoti ya mapato na matumizi.

Ripoti hiyo imekabidhiwa na Makamu wa Rais wa RT, William Kallaghe, kwa Katibu Mtendaji wa BMT, Neema Msitha.
BMT ilifanya kikao na Kamati ya Utendaji ya RT,    Januari 21 kwenye moja ya kumbi za Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, na moja ya maelekezo ya Baraza, ilikuwa ni kuitaka RT kuwasilisha ripoti ya mapato na matumizi 2020/21 hadi 2021/22.

Baada ya kuipokea ripoti hiyo, Katibu Mtendaji BMT, Msitha, alisema watakaa na kuifanyia kazi.

RT YAWATAKA WATAALAM WA RIADHA NCHINI KUWASILISHA TAARIFA ZAO

February 05, 2023

 





NA TULLO CHAMBO, RT

SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT), limewataka wataalamu wote wa mchezo huo kuwasilisha taarifa zinazoonyesha fani zao.
Agizo hilo, limetolewa na Kaimu Katibu Mkuu RT, Wakili Jackson Ndaweka, ambako amewataka makatibu wa vyama vya riadha mikoa yote ya Tanzania Bara, kuwajulisha wataalam wa riadha waliopo mikoani mwao, kuwasilisha taarifa zinazoonyesha fani zao katika mchezo huo. 

Wakili Ndaweka,amesema RT inakusudia kuendesha kozi mbalimbali za kuboresha uwezo wa wataalamu wa mchezo wa riadha waliopo na kuzalisha wengine katika fani ambazo zina upungufu. 

"Ili mpango huu uweze kutekelezeka kwa ufanisi, ni lazima kuwa na taarifa za wataalamu wa Riadha nchini, zitakazowezesha kuainisha maeneo yenye upungufu na kuyawekea mpango maalum," alisema na kufafanua. 

Taarifa zinazotakiwa zinapaswa kuwasilishwa kupitia wasifu 'CV', ambayo inapaswa kuambatanishwa na vivuli vya vyeti vya elimu ya Riadha na elimu ya kawaida. 

Wakili Ndaweka, alisema takwimu hizo ni muhimu sana kwa maendeleo ya mchezo wa riadha nchini. 

"Makatibu wanapaswa kuwajulisha wataalam waliopo kwenye mikoa yao, wawasilishe taarifa hizo kupitia anuani ya barua pepe ya shirikisho ambayo ni tan@mf.worldathletics.org si zaidi ya tarehe 20/02/2023," alisisitiza Ndaweka.

HURDLE RACE : What is Hurdle Race ?

August 28, 2021



Hurdling, sport in athletics (track and field) in which a runner races over a series of obstacles called hurdles, which are set a fixed distance apart.

Traditionally, there are two types of hurdle races—the 120-yard (110 meter) high hurdle and the 440-yard (403 meter) intermediate hurdle. The hurdles are 42 inches (1.06 meters) high in the 120-yard event and 36 inches (. 91 meters) high in the 440-yard event.



Image result for hurdle race
The most prominent hurdles events are 110 meters hurdles for men, 100 meters hurdles for women, and 400 meters hurdles (both sexes) – these three distances are all contested at the Summer Olympics and the World Athletics Championships.

Hurdling is a man killer event because it may cause injuries like lower back pain, groin, hip flexors and calves. This event need raw speed, strength, endurance and technical ability over the hurdles.
The hurdles are a slightly different height for each race, according to the International Association of Athletics Federation: 110m men's race: 1.067m or 3.5 feet. 100m women's race: 0.838m or 2.75 feet. 400m men's race: 0.914m or 2.99 feet.
How high are hurdles for 13 year olds?
As it stands now, in youth track there are 80 meter hurdles for the 11-12 year old's, 100 meter hurdles at 30” for 13-14 year-old girls, 100 meter hurdles at 33” for 15-16 and 17-18 year-old girls and 13-14 year-old boys, and 39” hurdles for 15-16 and 17-18 boys.
Which male hurdler won 122 consecutive hurdle races?
Moses
In Montreal in 1976, Moses won the 400m hurdles in. world record time. Eight years later in Los Angeles, he won a second gold medal. Between September 1977 and June 1987, Moses won 122 consecutive races.
What is meant by hurdle?
Image result
1 : a barrier to be jumped in a race. 2 hurdles plural : a race in which runners must jump over barriers. 3 : obstacle He overcame many hurdles to become successful.



What is world record of 400m race?
400 metres
Athletics 400 metres
The closing stages of a men's 400 m race
World records
MenWayde van Niekerk 43.03 (2016)
WomenMarita Koch 47.60 (1985)


The World Athletics Championships Oregon22 Marathon and Race Walks to be held in Eugene and Springfield, Oregon

August 28, 2021
TOC

 






The Local Organizing Committee (LOC) for the World Athletics Championships (WCH) Oregon22 has announced the global event’s marathons and race walks will be held in Eugene and Springfield, Oregon. These locations are within miles of the event’s main venue, Hayward Field at the University of Oregon.

The perimeter of Autzen Stadium, also located on the University of Oregon campus, will serve as a hub for the start and finish of all WCH Oregon22 Road Events, including the men’s and women’s marathon and men’s and women’s race walk events.

The LOC has been working with the Eugene Marathon team to develop courses for the road events that allow athletes, spectators, and digital fans to share in the glory of Oregon and the history of track & field in this community.

“We’re thrilled to have the chance to manage the WCH Oregon22 road events next summer,” Eugene Marathon Race Director and Oregon22 Road Events Course Manager Ian Dobson said. "We run on these roads every day and the thought of showing off our extraordinary community to the world, while also inspiring our own running community by bringing the world’s best athletes to them, is an opportunity unlike any other."

On the first day of competition, July 15, 2022, the women’s and men’s 20-kilometers race walk will take place. The only morning session of Day 8 is the women’s 35-kilometers race walk, the first of its kind in the World Championship series. Day 10, the final day of WCH Oregon22 is opened with the men’s 35-kilometers race walk. All race walk events will be conducted on a 1-kilometer looped course near Autzen Stadium.

The men’s marathon is set to open Day 3 of competition. The women’s marathon will be held the following morning on Day 4 of competition. Both the men’s and women’s marathon course will be a 14-kilometer looped course circling through Eugene and Springfield, Oregon. It will highlight the natural beauty and history of the heart and home of track and field in the U.S.

 

Copyright © 2015 - 2025 Athletics Tanzania All Right Reserved

Developed by Gadiola Emanuel
Theme By AP | Developed By Gadiola Emanuel