HURDLE RACE : What is Hurdle Race ?

August 28, 2021



Hurdling, sport in athletics (track and field) in which a runner races over a series of obstacles called hurdles, which are set a fixed distance apart.

Traditionally, there are two types of hurdle races—the 120-yard (110 meter) high hurdle and the 440-yard (403 meter) intermediate hurdle. The hurdles are 42 inches (1.06 meters) high in the 120-yard event and 36 inches (. 91 meters) high in the 440-yard event.



Image result for hurdle race
The most prominent hurdles events are 110 meters hurdles for men, 100 meters hurdles for women, and 400 meters hurdles (both sexes) – these three distances are all contested at the Summer Olympics and the World Athletics Championships.

Hurdling is a man killer event because it may cause injuries like lower back pain, groin, hip flexors and calves. This event need raw speed, strength, endurance and technical ability over the hurdles.
The hurdles are a slightly different height for each race, according to the International Association of Athletics Federation: 110m men's race: 1.067m or 3.5 feet. 100m women's race: 0.838m or 2.75 feet. 400m men's race: 0.914m or 2.99 feet.
How high are hurdles for 13 year olds?
As it stands now, in youth track there are 80 meter hurdles for the 11-12 year old's, 100 meter hurdles at 30” for 13-14 year-old girls, 100 meter hurdles at 33” for 15-16 and 17-18 year-old girls and 13-14 year-old boys, and 39” hurdles for 15-16 and 17-18 boys.
Which male hurdler won 122 consecutive hurdle races?
Moses
In Montreal in 1976, Moses won the 400m hurdles in. world record time. Eight years later in Los Angeles, he won a second gold medal. Between September 1977 and June 1987, Moses won 122 consecutive races.
What is meant by hurdle?
Image result
1 : a barrier to be jumped in a race. 2 hurdles plural : a race in which runners must jump over barriers. 3 : obstacle He overcame many hurdles to become successful.



What is world record of 400m race?
400 metres
Athletics 400 metres
The closing stages of a men's 400 m race
World records
MenWayde van Niekerk 43.03 (2016)
WomenMarita Koch 47.60 (1985)


The World Athletics Championships Oregon22 Marathon and Race Walks to be held in Eugene and Springfield, Oregon

August 28, 2021
TOC

 






The Local Organizing Committee (LOC) for the World Athletics Championships (WCH) Oregon22 has announced the global event’s marathons and race walks will be held in Eugene and Springfield, Oregon. These locations are within miles of the event’s main venue, Hayward Field at the University of Oregon.

The perimeter of Autzen Stadium, also located on the University of Oregon campus, will serve as a hub for the start and finish of all WCH Oregon22 Road Events, including the men’s and women’s marathon and men’s and women’s race walk events.

The LOC has been working with the Eugene Marathon team to develop courses for the road events that allow athletes, spectators, and digital fans to share in the glory of Oregon and the history of track & field in this community.

“We’re thrilled to have the chance to manage the WCH Oregon22 road events next summer,” Eugene Marathon Race Director and Oregon22 Road Events Course Manager Ian Dobson said. "We run on these roads every day and the thought of showing off our extraordinary community to the world, while also inspiring our own running community by bringing the world’s best athletes to them, is an opportunity unlike any other."

On the first day of competition, July 15, 2022, the women’s and men’s 20-kilometers race walk will take place. The only morning session of Day 8 is the women’s 35-kilometers race walk, the first of its kind in the World Championship series. Day 10, the final day of WCH Oregon22 is opened with the men’s 35-kilometers race walk. All race walk events will be conducted on a 1-kilometer looped course near Autzen Stadium.

The men’s marathon is set to open Day 3 of competition. The women’s marathon will be held the following morning on Day 4 of competition. Both the men’s and women’s marathon course will be a 14-kilometer looped course circling through Eugene and Springfield, Oregon. It will highlight the natural beauty and history of the heart and home of track and field in the U.S.

World Athletics makes commitment to a cleaner, greener, more equitable world

April 18, 2020
World Athletics President Sebastian Coe, Sustainable Development Advisory Group Chair Sylvia Barlag and HSH Prince Albert II are shown the air quality monitor by Kunak Technologies CEO Javier Fernandez Huerta (Philippe Fitte) © Copyright

World Athletics has today launched its Sustainability Strategy, which has a central goal of making the organisation carbon neutral by 2030. The strategy addresses global issues that pose a threat to the quality of our lives, using the power of sport and athletics to create a better world for communities.
The organisation will embrace sustainability principles and practices within its operations, its Member Federations and the organisation of future World Athletics Series events.
The ten-year strategy is designed to deliver tangible benefits across environmental, social and economic sustainability.
Among its commitments, World Athletics will reduce its carbon output by ten percent each year, switch to 100 percent renewable energy at its headquarters this year, introduce a sustainable procurement code and travel policy and develop best practice guides for its 214 Member Federations and its event organisers.
The strategy is divided into six pillars, each of which contain actions and targets for the organisation to pursue.
Some of the key components are:

Leadership in sustainability

  • Produce best practice guides for Member Federations and World Athletics Series event organisers
  • Embed sustainability principles in permit and licensing programmes
  • Align and embed sustainability goals into partnership agreements
  • Identify and engage our partners around the sustainability programme

Sustainable production and consumption

  • At headquarters, switch to 100 percent renewable energy
  • Implement comprehensive waste management system targeting reduction and reuse
  • Embed responsible procurement for all World Athletics activities and sanctioned events

Climate change and carbon

  • Reduce carbon footprint by ten percent each year to reach goal of carbon neutrality by 2030
  • Implement a sustainable travel policy reducing travel and building local capacity
  • All sanctioned events to commit to carbon neutrality targets

Local environment and air quality

  • Working with partners, establish low emission zones around athletics arenas
  • Maximise local economic impact around events by supporting local businesses
  • Develop a toolkit for improving air quality.
  • Air quality targets to be understood, set and monitored to protect runners and athletes
  • Air quality emissions to be included in equipment and venue standards.

Global equality

  • All geographic areas to have recognised opportunity pathways for both genders in all professions in athletics across athletes, coaches, technical officials, administrators
  • Build gender capacity with annual female leadership seminars conducted in all Areas

Diversity, accessibility and wellbeing

  • Protect athlete welfare with standardised basic health checks for all athletes before they compete in international events.
  • Ensure headquarters and other facilities are fully accessible
  • Ensure diverse workforce and fair treatment of staff and those working at and on our events, and for our suppliers and partners

World Athletics president Sebastian Coe said it was important for the organisation to make a commitment to a better future for coming generations.
“In the modern world, it has become apparent that our athletes and fans expect more from us than good governance of our sport. They also expect us to be a good global citizen, to take a leadership role in issues that affect the wider world and their communities. Sustainability is one of the great global challenges. We want to do our part to make this a better world and contribute to a cleaner, greener, more equitable future for everyone.
“We started on this path a couple of years ago when we made a commitment to assist the global campaign for improved air quality, and began installing air quality monitors in stadiums around the world, but it’s time for us to do more and I’m delighted to launch this roadmap for our organisation and our sport over the next decade. We have already ticked one item off the list, by switching to 100 percent renewable energy at our headquarters this year, and our ambition is to be a leader in organising sustainable events as we go forward.”
World Athletics

NGORONGORO NATIONAL OPEN ATHLETICS CHAMPIONSHIP 2019

May 01, 2019
 Katibu Mkuu Wilhelm Gidabuday , Mgeni rasmi na Viongozi wa RT
 High Jump
 Mgeni rasmi , Wanariadha na Viongozi wa RT

Serikali yakerwa na RT kutaka kuondoa jina la Alphonce Simbu katika Michezo ya Madola 2018

January 23, 2018


Mwanariadha nyota wa Tanzania, Alphonce Simbu.

Na Mwandishi Wetu
SUALA la Riadha Tanzania (RT) kutaka kuengua jina na mwanariadha nyota wa Tanzania, Alphonce Simbu limeingia sura mpya baada ya Serikali kuingilia kati.
Katika siku za hivi karibuni Katibu Mkuu wa RT, Wilhelm Gidabuday amekuwa akisisitiza kuwa mwanariadha huyo hatakwenda katika Michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Gold Coast, Australia Aprili.


Mkurugenzi wa Maendeleo nchini, Dk Yusuph Singo alisema jana kwa njia ya simu kutoka Dodoma kuwa, ameamua kuwaita Simbu, Gidabuday na Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi ili kupata ukweli wa jambo hilo.


Singo akizungumza na gazeti hili kutoka Dodoma alisema kuwa amekuwa akisikia uvumi wa taarifa hizo, lakini anapojaribu kuwaliza RT anaambiwa wamenukuliwa vibaya.


Mkurugenzi wa Michezo nchini, Dk Yusuph Singo.

Hatahivyo, mkurugenzi alisema kuwa anajua kuna kitu kinafichwa, hivyo ameamua kuitisha kikao mara moja kati ya watu hao ili kupata ukweli halisi.


Alisema kikao hicho kinaweza kufanyikia jijini Dar es Salaam au Dodoma kutegemea na nafasi yake (Dk Singo).


Alisema kuwa akimpigia simu Gidabuday anapata jibu tofauti kwani anasema waandishi wamemnukuu vibaya na akipiga kwa wengine anapata jibu tofauti, “hivyo nimeamua kuwaita kupata ukweli kamili.”


Juzi Gidabuday alisema kuwa Kamati ya Ufundi ya RT ilikutana kwadharura jijini Dar es Salaam na kuamu kutoa jina la Simbu katika orodha ya majina ya wanariadha watakaoshiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola.


Alisema wameamua hivyo ili kumuwezesha mchezaji huyo kupumzika na kujiandaa kwa ajili ya London Marathon zitakazofanyika London, Uingereza Aprili ili kujipatia fedha.

Katibu Mkuu TOC, Filbert Bayi.

Alisema mwanariadha huyo atawakilisha taifa katika mashindano ya dunia ya riadha yatakayofanyika Doha mwakani na yale ya Olimpiki Tokyo, Japan 2020, ili kulipatia taifa medali za dhahabu.


Gidabuday alisema Simbu amekimbia mashindano mengi ya kuliwakilisha taifa, ambayo yana presha kubwa, sasa anahitaji kupumzika na kukimbia mashindano ya mwaliko kama London Marathon.



Hivi karibuni Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi alisema kuwa wao kama waratibu wa michezo hiyo, hawana taarifa na kutolewa kwa jina la Simbu na kuitaka RT kupeleka barua TOC kama kweli wanataka kuliondoa jina hilo.

Katibu RT, Wilhelm Gidabuday.

Tigo yatangaza Zawadi Nono za Kili Marathon 2018

January 23, 2018


Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya simu za Mkononi ya Tigo Kanda ya Kaskazini, Henry Kinabo akizungumza wakati wa uzinduzi wa Msimu wa 16 wa Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro Marathon 2018,Uzinduzi uliofanyika katika Hoteli ya Kibo Palace Homes mjini Moshi juzi, Mashindano ambayo Kampuni ya Tigo inadhamini Mbio za Nusu Marathon,Km 21. Pichani (mwenye kofia) Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira na wadau mbalimbali. (Na Mpigapicha Wetu).

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Simu za mkononi ya Tigo imesema kuwa itadhamini tena mbio za nusu marathon za Kilimanjaro zitakazofanyika Machi 4 mjini Moshi.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mbio hizo juzi, Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya simu za Mkononi ya Tigo Kanda ya Kaskazini, Henry Kinabo alisema wanadhamini tena mbio hizo kwa mwaka wanne mfululizo.


Kinabo alisema wanaunga mkono mbio hizo, ambazo zinasaidia kuibua na kuviendeleza vipaji vya vijana na kuhakikisha Watanzania wanaishi katika maisha ya kiafya kwa kushiriki katika mchezo huo wa riadha.


Alitaja zawadi, ambazo zitatolewa kwa washindi wa kwanza kwa upande wa wanawake na wanaume, kila mmoja ataondoka na kitita cha sh milioni 2.


Huku washindi wa pili kila mmoja tazawadiwa sh milioni 1 huku mshindi watatu ataondoka n ash 650,000, wanne sh 500,000, mshindi wa sita sh 325,000 wakati wasabi atapewa sh 250,000.


Alisema kuwa mshindi wanane ataondoka na kiasi cha sh 150,000, huku mshindi wa tisa atapewa sh 125,000 na wa 10 atabeba sh 100,000.

Waziri Maghembe 'kuibeba' Rock City Marathon

August 22, 2017





Dar es Salaam;WAZIRI wa Maliasili na Utalii Prof Jumanne Maghembe mwishoni mwa wiki hii alizindua rasmi usajili wa msimu wa nane wa mbio za Rock City Marathon huku akiahidi kushirikiana na waandaaji wa mbio hizo katika kuhakikisha kuwa zinatumika vema kuutangaza utalii wa ndani.


Akizungumza kwenye hafla fupi ya uzinduzi huo iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa mchezo huo wakiwemo viongozi wa serikali pamoja na wadhamini mbalimbali wa mbio hizo, Waziri Maghembe alisema azma yake hiyo inasukumwa na malengo ya mbio hizo ambayo ni kutumia mchezo wa riadha katika kutangaza utalii hususani katika Ukanda wa Ziwa.


"Kwa kuzingatia uzito wa malengo ya mbio hizo nitamke bayana kuwa nipo tayari kushirikiana na waandaaji wa mbio hizi kuhakikisha kwamba kuanzia mwaka huu mbio hizi zinafana na zinavutia washiriki wengi zaidi hususani wa kimataifa,'' alisema Waziri Maghembe ambae pia alithibitisha ushiriki wake kwenye mbio hizo zinazoratarajiwa kufanyika Octoba 29, mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na kupita katika barabara mbalimbali za jiji hilo kabla hazijamalizikia katika uwanja huo.


Mbali na ushiriki wake,Waziri Maghembe alitoa wito kwa mashirika mbalimbali yaliyo chini ya wizara yake ikiwemo la Hifadhi za Taifa(Tanapa), Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori (TAWA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) na Makumbusho ya Taifa kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika kufanikisha mbio hizo.


"Ukanda wa Ziwa una vivutio vingi ambavyo pia kama Wizara yenye dhamana ya utalii lazima tuvigeukie na kuvitangaza kwa nguvu na kwa njia tofauti ikiwemo michezo,'' alisema Waziri Maghembe huku akivitaja baadhi ya vivutio hivyo kuwa ni pamoja na Kisiwa cha Saanane, Makumbusho ya kabila la Wasukuma pamoja na tamaduni za makabila ya wakazi wa Kanda ya Ziwa.


Mbio za Rock City Marathon zilizoanzishwa miaka minane iliyopita zinazozidi kujiongezea umaarufu kila mwaka na tayari zimefanikiwa kuwavutia baadhi ya wadhamini ikiwa ni pamoja na kampuni za TIPER, PUMA, Bodi ya Utalii Tanzania (TTB),Mwanza Hotel , Real PR Solutions Limited, Afrimax Strategic Partnerships Limited, EF Outdoor, CF Hospital na ATCL.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio hizo, Bw Zenno Ngowi alitoa wito kwa washiriki wa ndani hususani wa mikoa ya Kanda ya Ziwa pamoja na wadhamini kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mbio hizo ambazo kwa mwaka jana zilifanikiwa kuhusisha washiriki zaidi ya 2000 na watazamaji zaidi ya 30,000.


Naye Mratibu wa mbio hizo zinazoandaliwa na kampuni ya Capital Plus International, Bi Adeline Ndesanjo alisema mbio za mwaka huu zinatarajiwa kuhusisha washiriki wengi zaidi kutoka kila kona ya dunia ikiwemo Afrika, Ulaya,China,Mashariki ya Kati hususani Israel na Marekani huku akitoa wito kwa washiriki wa ndani kujisajili kwa wingi ili kuthibitisha ushiriki wao kwenye mbio hizo.


Akizungumza kwa niaba ya wadhamini wengine wa mbio hizo Meneja Masoko wa Kampuni ya mafuta ya Puma, Bw Machumani Shebe alisema ushiriki wao umechagizwa zaidi na azma ya kampuni hiyo kuisaidia serikali katika kuutangaza utalii wa ndani.


"Tukiwa kama wadau muhimu katika biashara ya mafuta hususani mafuta ya ndege tunategemea sana ustawi wa sekta ya utalii katika kuongeza soko la biashara yetu na kwa kuwa mchezo wa riadha umekuwa ukitumika zaidi katika kuwavutia watalii tukaona kuna haja ya kuunga mkono ufanikishaji wa mbio hizi,'' alisema.




WAZIRI wa Maliasili na Utalii Prof Jumanne Maghembe akizungumza na wadau mbalimbali wa mchezo wa riadha hapa nchini pamoja na waandaaji wa mbio za Rock City Marathon kwenye hafla maalumu ya uzinduzi rasmi usajili wa msimu msimu wa nane wa mbio hizo iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio hizo, Bw Zenno Ngowi akizungumza kwenye hafla hiyo. Alitoa wito kwa washiriki wa ndani hususani wa mikoa ya Kanda ya Ziwa pamoja na wadhamini kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mbio hizo ambazo kwa mwaka jana zilifanikiwa kuhusisha washiriki zaidi ya 2000 na watazamaji zaidi ya 30,000.

Mratibu wa mbio hizo zinazoandaliwa na kampuni ya Capital Plus International, Bi Adeline Ndesanjo akitoa maelezo kuhusu maandalizi ya mbio hizo kwenye hafla hiyo. Alisema mbio za mwaka huu zinatarajiwa kuhusisha washiriki wengi zaidi kutoka kila kona ya dunia ikiwemo Afrika, Ulaya,China,Mashariki ya Kati hususani Israel na Marekani .

Wadhamini nao hawakuwa nyuma!Meneja Masoko wa Kampuni ya mafuta ya Puma Energy, Bw Machumani Shebe alisema ushiriki wao kwenye mbio hizo umechagizwa zaidi na azma ya kampuni yake hiyo kuisaidia serikali katika kuutangaza utalii wa ndani.


Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.


WAZIRI wa Maliasili na Utalii Prof Jumanne Maghembe akiwa kwenye picha ya pamoja na waandaaji wa mbio hizo pamoja na wadau mbalimbali wa mchezo huo wakiwemo viongozi wa serikali pamoja na wadhamini wa mbio hizo.

WATANZANIA KUTIMUA VUMBI LONDON LEO! KUONEKANA MBASHARA DStv

August 05, 2017






Timu ya Taifa ya Riadha inayoshiriki mashindano ya Dunia ya riadha yanayoendelea jijini London inaanza kibarua cha kuipeperusha bendera yetu leo (Jumamosi 05/08/2017) ambapo mfukuza upepo Failuna Abdi Matanga atakimbia mbio za mita 10,000 leo .


Failuna atashuhudiwa na maelfu ya watanzania kupitia DStv Muda wa saa mbili usiku.

Akithibitisha kuonekana kwa matangazo hayo kupitia DStv, Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania Maharage Chande amesema DStv imefanya jitihada kubwa na kuhakikisha kuwa watanzania wanaishuhudia timu yetu ikituwakilisha katika mashindano hayo muhimu ulimwenguni.

“Tunawahakikishia watanzania burudani hii moja kwa moja kupitia DStv chaneli za Supersport. Tunaamini sote tutakuwa nyuma yao wachezaji wetu kuwashuhudia jinsi wanavyotuwakilisha” alisema Maharage

“Suala la watanzania kuwashuhudia vijana wetu wakishiriki katika mashindano makubwa kama haya lina maana kubwa sana. Vijana wadogo wakiwaona dada zao na kaka zao wakishiriki mashindano makubwa kama haya inawatia moyo na kuwapa ari na tamaa ya wao kujitahidi na kufika hatua kama hizo. Hili ni jambo la muhimu sana na sisi DStv tunalitilia mkazo sana. Ni njia moja wapo ya kuwashawishi na kuwatia moyo vijana wetu wanaochipukia na kuwajengea kujiamini”

Baada ya Failuna anayekimbia mita 10,000, watanzania watashuhudia tena shughuli pevu siku ya jumapili kupitia DStv kuanzia majira ya saa nne asubuhi ambapo vidume watatu - Alphonce Felix Simbu, Ezekiel Jafari Ng’imba na Stefano Huche Gwandu watakuwa wakikata upepo katika viunga vya jiji la Malkia London ikiwa ni mbio ndefu za kilomita 42.

Baada ya vidume hao kukamilisha kazi tuliyowatuma, wanawake wetu wa shoka nao wataingia barabarani ambapo Tanzania inawakilishwa na Sara Ramadhani Makera na Magdalena Crispin Shauri ambao nao watafukuza upepo umbali wa kilomita 42 majira ya saa nane mchana. Patashika yote hii itaonekana DStv.

Wanariadha wengine wawili wa mbio fupi za mita 5,000 ambao ni Emmanuel Giniki Gisamoda na Gabriel Gerald Geay watatimka siku ya Jumatano tarehe 9 Agosti majira ya mbili usiku hii ikiwa ni raundi ya mchujo na wakifuzu watashiriki fainali ya mita 5,000 siku ya Jumamosi Agost 12, majira ya mbili usiku. Nao pia watashuhudiwa mbashara kupitia DStv

Mashindano ya Dunia ya Riadha yalianza rasmi 1983 ambapo Tanzania imewahi kupata medali 1 tu ya Fedha kupitia mwanariadha Christopher Isegwe kwenye mbio za Marathon 2005 Helsinki Finland.

Ni mashindano ya pili kwa ukubwa baada ya Olimpiki ambapo nchi 204 zinashiriki mashindano hayo mwaka huu. Tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo mwaka huu ndiyo mwaka ambao Tanzania imeleta timu kubwa ya wanariadha 8, ambao ina mchanganyiko wa wanaume na wanawake na pia kuna wakimbiaji wa mbio za uwanjani.
Wanariadha wote wanaoshiriki wamefikia viwango vinavyotakiwa na Shirikisho la Riadha Duniani (IAAF)

Health Nusu Marathon Kufanyika Dar Aprili 26

April 21, 2017


Katibu Mkuu wa Taasisi ya Tanzania Health Summit Bi. Rebecca John (katikati) akisisitiza jambo kwa wandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akielezea maandalizi ya mbio za heart marathon na upimaji wa afya yenye lengo la kuisaidia serikali kupunguza magonjwa yasiyoambukizika mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Riadha Tanzania Bi. Ombeni Zavara na kulia ni Katibu Mkuu Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Lucas Nkungu.
Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Riadha Tanzania Bi. Ombeni Zavara akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya ya mbio za heart marathon na upimaji wa afya yenye lengo la kuisaidia serikali kupunguza magonjwa yasiyoambukizika mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Katibu Mkuu wa Taasisi ya Tanzania Health Summit Bi. Rebecca John.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Tanzania Health Summit Dkt. Omary Chillo (kulia) akifafanua jambo kwa wandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akielezea maandalizi ya mbio za heart marathon na upimaji wa afya yenye lengo la kuisaidia serikali kupunguza magonjwa yasiyoambukizika mapema hii leo jijini Dar es Salaam, katikati ni Katibu Mkuu Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Lucas Nkungu na kushoto ni Katibu Mkuu wa Taasisi ya Tanzania Health Summit Bi. Rebecca John.

……………..

Na Nuru Juma-Maelezo

Taasisi ya Tanzania Health Summit yaandaa mbio za nusu Marathon na Upimaji wa afya kwa lengo la kusaidia juhudi za serikali katika kupunguza magonjwa yasioambukiza, mbio hizo zinazotarajia kufanyika Aprili 26 katika barabara ya Kaole iliyopo Masaki jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Taasisi hiyo Rebecca John wakati alipokutana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuhamasisha jamii kushiriki.

“Kamati ya maandalizi ya ya mbio za Heart Marathon inapenda kuwa taarifu wadau wote wa sekta ya afya hapa nchini na jamii kwa ujumla juu ya mbio za Heart Marathon na upimaji wa afya ili kuungana na serikali katika juhudi za kupunguza magonjwa yasiyoambukiza” alisema Rebecca.

Aliongeza kuwa kwa mwaka huu mbio hizi zitashirikisha washiriki zaidi ya elfu mbili kutoka rika mbalimbali wakiwemo vijana, watoto, wazee, makundi ya watu wenye ulemavu na watu wenye magonjwa yasiyoambukiza.

Pia washiriki watapata nafasi ya kupima afya magonjwa mbalimbali kama vile shinikizo la damu ,wingi wa sukari katika damu, kiasi cha mafuta mwilini, uchunguzi wa uvimbe katika matiti na kupata ushauri wa wataalam kuhusiana na vyakula bora, magonjwa ya moyo na mishipa ya damu.

Aidha Bi. Rebecca aliongeza kuwa washiriki watakimbia umbali tofauti, kwani kuna mbio ndefu za kilometa 21.1 kwa ajili ya wakimbiaji wazoefu, kilometa 10 kwa wakimbiaji wa kati, kilometa 5 kwa wakimbiaji wa kawaida, kifamilia na kampuni na mbio za watoto chini ya miaka 12 ni meta 700 na zawadi itatolewa kwa mshindi wa kilometa 21.1 pekee kwa kiasi cha shilingi laki tano.

Kwa upande wake Rais wa Tanzania Health Summit Dr.Omary Chillo alisema kuwa washiriki watatakiwa kutoa kiasi kidogo cha fedha kwa ajili ya kununua flana pamoja na kifaaa maalum cha kuhesabia muda wakati wa kukimbia ila maji ya kutosha yatatolewa bure kwa ajili ya wakimbiaji.

Aliongeza kuwa wameimarisha ulinzi kwa kushirikiana na jeshi la polisi na ili kulinda usalama kwa washiriki na wananchi watakaokuwepo katika mashindano hayo.

“wananchi wasiwe na wasiwasi wa usalama kwani tutashirikiana na jeshi la polisi ili kuimarisha usalama na tumeweza kupata baraka nyingi kutoka kwao kwa kuweza kushirikiana nao” aliongeza Chillo.

Pia Katibu msaidizi wa Chama cha Riadha nchini Bi Ombeni Zavala alisema anashukuru wananchi wanavyoweza kujitokeza katika mashindano hayo na pia anawaomba wananchi hasa vijana waendelee kujitokeza kwa wingi kwani wanaweza kupata nafasi ya kuunda timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17.

Naye Sajenti Isaya Mlokozi kutoka kanda ya usalama barabarani alisema jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani litahusika vizuri katika sehem inayowahusu kuhakikisha watu wanafanya zoezi hilo kwa hali ya usalama na litajumuika na wananchi popote pale watakapokuwa wanakwenda.

Mashindano haya mwaka jana yalifanyika katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam lakini kutokana na kuongezeka kwa watu mwaka huu yatafanyikia barabara ya kaole yenye kauli mbiu ‘piga hatua moja mbele ya magonjwa sugu’

RT Yataja Majina 23 Waliochaguliwa kuunda timu ya Taifa ya Vijana

April 17, 2017
Na Mwandishi Wetu
RIADHA Tanzania (RT) imetangaza majina 23 kwa ajili ya kuunda timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 kwa ajili ya kushiriki katika mashindano ya Kanda ya Tano ya Afrika yatakayofanyika jijini Dar es Salaam mapema mwezi ujao.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa RT, Whilhem Gidabuday, timu hiyo itapiga kambi katika hosteli za Filbert Bayi zilizoko Mkuza Kibaha kuanzia Jumanne chini ya makocha Robert Kalyahe na Mwinga Mwanjala.
Timu hiyo inaundwa na wachezaji 12 wavulana wakatu wasichana katika timu hiyo wako 11 ma watashiriki katika michezo yam bio za meta 100, 200, 400, 800, 1500 na 3000 pamoja na miruko na mitupo.


Gidabuday alisema kuwa kambi hiyo itagharimu kiasi cha sh Milioni 20 kuanzia timu hiyo itakapokuwa kambini kwa karibu siku 20, wakati wa mashindano na huduma zingine.


Mbali na wenyeji Tanzania Bara, nchini zingine zitakazoshiriki ni pamoja na Zanzibar, Uganda, Kenya, Rwanda, Sudan, Sudan Kusini, Ethiopia, Eritrea na Djibout.


Timu hiyo ilichaguliwa jana mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya wazi ya taifa yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa na kuhudhuriwa na mikoa michache.
Baadhi ya wanariadha walioshiriki walitoka katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Arusha na Manyara, ambapo shule ya Filbert Bayi iliyopo mkoani Pwani, imeto wachezaji watano katika timu ya wasichana kutokana na umahiri wao.

Ukiondoa baadhi ya kasoro zilizokuwepo ikiwemo kutokuwa na huduma ya kwanza wala gari la wagonjwa, wachezaji wakishiriki bila ya kuwa na namba za kuwatambua na kuleta ugumu kwa waandishi wa habari kujua nani ni nani, mashindano yalienda vizuri.






















Mwanariadha wa Kimataifa, Alphonce Simbu Kuanza Safari ya Kushiriki London Marathon

April 17, 2017



Na Mwandishi Wetu

MWANARIADHA wa kimataifa wa Tanzania, Alphonce Simbu kesho Jumatatu atapanda pipa kwenda Afrika Kusini akiwa njiani kwenda Uingereza, ambako atashiriki London Marathon Jumapili ijayo Aprili 23.

Simbu anapitia Afrika Kusini kwa ajili ya kupatiwa viza ya dharura ya kuingia Uingereza baada ya kuikosa ile ya kawaida jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania (RT), Wilhelm Gidabuday alisema jana kuwa, Simbu ataondoka kesho Jumatatu kwenda Afrika kusini kushughulikia viza ya kuingia Uingereza kabla ya kwenda nchini humo ambako Jumapili atashiriki London Marathon.

Simbu alifuzu kwa mbio hizo baada ya kumaliza katika nafasi ya tano katika Michezo ya Olimpiki iliyofanyika Rio de Janeiro, Brazil 2016 kabla ya kushinda mbio za Mumbai Marathon.

Kwa mujibu wa Gida, tayari mwanariadha huyo ameingia katika orodha ya wanariadha bora kabisa duniani na ndio maana waandaaji wa London Marathon kuna fedha atapewa mara tu atakapoanza mbio hizo (Appearance Fees).

Gidabuday alisema kuwa Simbu hata kama hatashinda mbio hizo lakini akimaliza tu amejihakikishia fungu nono na kama akimaliza, basi ataondoka na maelfu ya dola za Marekani.

Simbu endapo atashinda mbio hizo za London Marathon ataondoka na kitita cha dola za Marekani 55,000 kama zaidi yash Milioni 150, na kama atafanikiwa kuvunja rekodi ataongezewa dola za Marekani 25,000 (ikiwa ni zaidi ya sh Mil 50),

Mshindi wa kwanza hadi wa 12 wa mbio hizo ataondoka na kitita cha fedha, huku wale watakaokimbia muda bora bbila kujali kama umevunja rekodi ya njia au ya dunia, nao wataongezewa fedha za bonasi.

Athletics Body to Move Its Haedquarters to Dodoma

December 22, 2016
Left, Secretary General (AT) Wilhelm Gidabuday and the Former New York City Marathon Champion, Juma Ikangaa. Picture by Gadiola Emanuel.



By Zephania Ubwani

Arusha — Athletics Tanzania (AT) may be the first national sports association to shift its head offices from Dar es Salaam to the designated capital Dodoma, according to its recently elected secretary general, Wilhelm Gidabuday.

The body is already in contact with the Capital Development Authority (CDA), a government institution in charge of infrastructure development in Dodoma, to secure a plot for construction of its headquarters. "We need a plot for our permanent home. After securing it, we will apply for a grant to meet the cost of construction," he told The Citizen here on Monday during an interview on a wide range of issues

He said AT president Anthony Mtaka, who doubles as the Simiyu regional commissioner, has been in touch with CDA officials over the issue.

"After getting the plot, we will seek a title deed we will use as collateral to secure a loan for the project," he said, noting that they will approach the social security institutions for financial support.

Gidabuday, a former national athlete and until recently, a coordinator of various athletics promotion programmes, was elected the new AT secretary general early this month.

He succeeded Suleiman Nyambui who is now an athletics coach in Brunei, a South East Asia sultanate.

He said he would address the major challenges facing the association, including lack of office accommodation that merits its status, working equipment and competent staff for its secretariat.

"We need a modern, spacious and well equipped office which will suffice all our administrative needs," he said, noting that AT, which is one of the oldest sports associations in the country, currently does not have an office that meets its requirements.

"Presently, I can dare say, we have no clear office. There is a room near the Uhuru Stadium, but it's in poor shape," he said, adding that he would fight for a comfortable office space in Dar es Salaam before the Dodoma project is realised.

The long-term plan is to construct the multi-purpose building in Dodoma which will be known as Riadha Tanzania House. Besides serving as the permanent home for AT, some rooms would be rented out to other institutions.

However, Gidabuday insisted that their dreams for a permanent home would depend on support from the government, especially the ministry responsible for sports, CDA, the National Sports Council (NSC) as well as the International Association of Athletics Federation (IAAF), a governing body for the athletics in the world headquartered in Monaco.

TANAPA yaiongezea nguvu timu ya RT, kwa ajili ya wanariadha wanaojiandaa na Olimpiki

July 26, 2016

Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akitoa neno la ukaribisho kwa wanahabari na wageni wengine katika hafla fupi ya kukabidhi hundi kwa wanariadha wanaounda timu ya taifa, inayojiandaa na mashindano ya Olimpiki yatakayoafanyika mwezi Agosti  nchini Brazil.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi,akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi hundi ya Shilingi Milioni tano kwa wanariadha wanaounda timu ya taifa inayojiandaa na mashindano ya Olimpiki.
Mkurugenzi Mkuu  wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akikabidhi mfano wa hundi ya Shilingi Milioni tano kwa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka kwa ajili ya kusaidia wanariadha wanaounda timu ya taifa wakijiandaa na mashindano ya Olimpiki. 
Mkurugenzi Mkuu  wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akikabidhi "Track Suit "maalumu zenye maandishi na nembo yanayotangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini kwa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka kwa ajili ya kusaidia wanariadha wanaounda timu ya taifa wanaojiandaa na mashindano ya Olimpiki
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka akizungumza mara baada ya kukabidhiwa hundi pamoja na mavazi maalumu kwa ajili ya wanariadha hao .
Baadhi ya viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) waliohudhuria hafla hiyo.kutoka kushoto Mkurugenzi wa Utalii na Masoko,Ibtahim Musa,Meneja Utalii Johnson Manase na Mhifadhi Vitalis Uruka.
Wanariadha watakaoiwakilisha nchi katika mashindano ya Olimpiki katika jiji la Reo De Jeneiro nchini Brazil wakiwa katika mavazi maalumu yanaotangaza vivutio vilivyoko nchini.
Mkufunzi wa Wanariadha wanaojiandaa na mashindano ya Olyimpiki ,Francis John akizungumzia matarajio yake juu ya vijana hao.
Mmoja wa Wanariadha hao,Alphonce Felix Simbu akizungumza mara baada ya kupoke msaada kutoka  TANAPA.
Baadhi ya Wanahabari na wageni wengine waliofika katika ofisi za Makao Makuu ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kushuhudia makabidhiano hayo.
Mwanariadha Said Makuka atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Mwanariadha Sara Ramadhan ,mwanadada pekee atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Mwanariadha Alphonce Felix atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Mwanariadha Fabian Joseph atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Wanariadha wanne watakao iwakilisha Tanzania katika Michuano ya Olyimpiki nchini Brazil wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi pamoja na Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Antony Mtaka ,wengine kutoka kulia ni Mkufunzi wa wanariadha hao,Francis John na anyefuatia ni Mkurugenzi wa Utalii na Masokowa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa.

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog,Kanda ya Kaskazini.

SHIRIKA la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limetangaza  kutumia fursa ya mashindano ya Olyimpiki yanayotarajia kuanza mwezi ujao katika jiji la Rio de Janeiro nchini Brazili kutangaza vivutio vya utalii kupitia wanariadha wa Tanzania.

Hadi sasa ni wanariadha wanne ,wakiume watatu na wa kike mmoja ndio waliofuzu kushiriki mashindano hayo na tayari wako kambini katika hosteli za Chuo cha Misitu cha FITI zilizoko West Kilimanjaro wilayani Siha.

Akiongea mjini Arusha wakati akikabidhi msaada wa fedha na vifaa kwa ajili ya wanariadha hao Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA,Allan Kijazi amesema wameamua kutumia fursa hiyo pia kusaidia wanariadha hao wanaoiwakilisha nchi katika mashindano hayo ili waweze kurejea na medali.

Akishukuru kwa msaada huo Rais wa Shirikisho la Riadha nchini ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu AnthonY Mtaka amesema fedha hizo zitatumika kwa ajili ya kuwakatia bima ya Afya mwaka mmoja wanariadha hao pamoja na familia zao ili wanapokua nchini Brazili wasiwe na mawazo mengi kuhusiana na familia zao walizoziacha hapa nchini.

Naye mmoja wa wanariadha waliofuzu kushiriki mashindano hayo Alphonce Felix pamoja na mkufunzi wa timu hiyo ya Riadha Francis John wameushukuru uongozi wa Riadha kwa kuiwezesha timu hiyo kukaa kambini kwa miezi saba na kuahidi safari hii timu hiyo haiendi kushiriki bali kupambania medali.

Wanariadha waliopo katika timu hiyo ya taifa wanaotarajiwa kwenda Brazili ni mwanamke pekee Sara Ramadhani, Fabiani Joseph, Saidi Makuka na Alfonce Felix .
 

Copyright © 2015 - 2025 Athletics Tanzania All Right Reserved

Developed by Gadiola Emanuel
Theme By AP | Developed By Gadiola Emanuel