Showing posts with label Marathon. Show all posts
Showing posts with label Marathon. Show all posts

CRDB BANK MARATHON YAFANYIKA DAR

August 17, 2025


Dar es Salaam, 17 Agosti 2025 - Maelfu ya wakimbiaji na wapenda michezo kutoka ndani na nje ya Tanzania wamejitokeza leo katika viwanja vya The Green, Oysterbay, kushiriki CRDB Bank Marathon 2025, mbio za hisani ambazo mwaka huu zimekusanya Shilingi Bilioni 2 ili kusaidia matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo, wakinamama wenye ujauzito hatarishi, na vijana kupitia programu ya iMBEJU.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mwansasu, aliongoza maelfu ya washiriki kwenye msimu huu wa sita wa CRDB Bank Marathon. 
Akitoa salamu zake, Dkt. Tulia alipongeza ubunifu wa CRDB Bank Foundation katika kuunganisha jamii kupitia michezo na kusaidia wenye uhitaji, akieleza kuwa mbio hizo ni mfano wa vitendo vya huruma vinavyogusa maisha ya wengi. 
 
“Ushiriki wetu katika CRDB Bank Marathon ni tendo la huruma linaloleta faraja kwa watoto na wakinamama na familia zao. Ni ushahidi kwamba tukishirikiana, tunaweza kubadilisha maisha,” alisema.
Akitoa salamu zake, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, aliipongeza Benki ya CRDB na CRDB Bank Foundation kuendelea kuandaa mbio hizo. 
 
Alisema, “CRDB Bank Marathon si tu imekuwa ikikuza afya na mshikamano wa kijamii, bali pia imekuwa ikifungua milango ya ajira na fursa za kiuchumi kwa vijana wetu. Michezo ni sekta inayoweza kubadili maisha, na ninapongeza sana kitendo cha kuweka zawadi nono kwa washindi. Hizi ni fursa ambazo zinaweza kuwa mtaji wa kuanzisha biashara na kuimarisha maisha ya vijana wetu. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau kama CRDB Bank Foundation kuhakikisha michezo inakuwa chachu ya maendeleo ya taifa.”
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alibainisha kuwa msimu wa sita wa CRDB Bank Marathon umefanyika sambamba na maadhimisho ya miaka 30 ya Benki ya CRDB, na kuendelea kupanua wigo wa matokeo yake ndani na nje ya Tanzania. Kwa mara ya pili, mbio hizi zimefanyika pia nchini Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), zikikusanya fedha kwa ajili ya miradi ya afya na ustawi wa jamii katika nchi hizo. 

Nsekela alisema kuwa mbio za mwaka huu zimeweza kuvutia zaidi ya washiriki 16,000, na kufanikisha lengo la kukusanya shilingi bilioni 2 ambapo pamoja na kusaidia maandalizi ya mbio hizo, shilingi milioni 450, zimeelekezwa kusaidia wenye uhitaji katika jamii. 
 
Kati ya hizo shilingi milioni 100 zimekwenda hospitali ya CCBRT kusaidia wakinama wenye ujauzito hatarishi kujifungua salama, shilingi milioni 100 zimekwenda Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kusaidia upasuaji wa Watoto wenye matatizo ya moyo, na shilingi 250 zitaelekezwa katika uwezeshaji wa vijana.
Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya mbio hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa, alieleza kuwa safari ya msimu wa sita imeanzia Lubumbashi, DRC, ambako zilikusanywa Dola za Marekani 70,000 kwa ajili ya kuboresha huduma za afya katika hospitali ya Jeshi la Ruashi, na kuendelea Bujumbura, Burundi, ambapo zilipatikana Faranga za Burundi milioni 175 kusaidia bima ya afya kwa zaidi ya watu 58,000 wasiojiweza. 
 
Mwambapa alisisitiza kuwa mafanikio haya ni matokeo ya mshikamano wa kipekee wa serikali za nchi shiriki, wadhamini na washiriki, akiwashukuru wadau wote waliotoa jitokeza kuchangia ikiwamo kampuni za bima za Sanlam Life na Alliance Life ambao wamekuwa sehemu ya mbio hizi tangu kuanzishwa kwake.
Washindi wa mbio za mwaka huu upande wa Tanzania kwa Kilometa 42 upande wa wanawake ni Joyloyce Kemuma kutoka Kenya, upande wa wanaume mshindi ni Abraham Kiptum kutoka Kenya. Kilometa 21 upande wa wanawake ni Catherine Syokau kutoka Kenya, na upande wa wanaume ni Joseph Panga kutoka Tanzania. Kilometa 10 upande wa wanawake ni Silia Ginoka kutoka Tanzania, na upande wa wanaume ni Boayi Maganga kutoka Tanzania.
 
Joseph Panga mshindi wa mbio za Kilometa 21 upande wa wanawake ameeleza furaha yake kushiriki katika mbio hizo na kusema kuwa ushindi wake ni sehemu ya kusaida matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo na matibabu ya wakinamama wenye ujauzito hatarishi hospitali ya CCBRT. 
 
“Mimi kama Mtanzania najisikia fahari kubwa kushiriki kusambaza tabasamu kwa watoto na wakinamama. Ni muhimu watu kufahamu kuwa afya bora ni haki ya kila mtoto, na hakuna mama anayestahili kupoteza maisha wakati wa kujifungua. Tunawashukuru CRDB Bank Foundation kwa kutuleta pamoja katika harakati hizi za kuokoa maisha,” amesema.
CRDB Bank Marathon imekuwa jukwaa muhimu la kuchochea ustawi wa kijamii katika ukanda huu wa Afrika ya Mashariki na kati hivi karibuni ikipata heshima ya kutambuliwa kimataifa kwa kushinda tuzo ya jukwaa bora la taasisi za fedha katika kusaidia kusaidia jamii.

Washindi NBC Dodoma Marathon Kuiwakilisha Tanzania Kimataifa, Dkt Ndumbaro Athibitisha Ushiriki Wake Mbio Za Km 42

July 23, 2024

Serikali imesisitiz dhamira yake ya kutumia mbio za NBC Dodoma Marathon kama chanzo cha kuwapata wanariadha sahihi watakaoliwakilisha taifa kwenye mashindano ya kimataifa yakiwemo mashindano ya Olympic na Mashindano ya Jumuiya ya Madola (Commonwealth).  Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro amebainisha dhamira hiyo ya serikali jijini Dar es Salaam leo huku akithibitisha nia yake ya kukimbia km 42 (full marathon) kwenye mbio hizo zinatotarajiwa kufanyika jijini Dodoma, Julai 28 mwaka huu. 

Lengo kuu la mbio hizo zinazotarajiwa kuongozwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ni kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na  kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga  ili kuboresha afya ya mama wa mtoto.

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya benki ya NBC  akiwa sambamba na mwenyeji wake Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw Theobald Sabi,  Dkt Ndumbaro pamoja na kusifia jitihada za benki hiyo katika kuinua sekta ya michezo nchini, alisema kwasasa taifa linakabiliwa na uhaba mkubwa wa wanariadha wenye sifa ya kushiriki mashindano ya kimataifa hivyo serikali imejipanga kutumia mbio hizo kutambua wanariadha wenye sifa sahihi kwa ajili ya maandalizi ya mashindano mbalimbali ya kimataifa.

“Kwasasa kwenye mashindano ya Olympic tunakwenda na wanariadha wachache sana kwasababu hatuna maandalizi ya kutosha. Hivyo NBC Dodoma Marathon ni moja ya chanzo cha kupata wanariadha wazuri ili baada ya mbio hizi tuweze kuwatamuba na kuwapa mafunzo zaidi ili mashindano ya ‘Commonwealth’ na Olympic na mengine mbalimbali ya kimataifa tuwe na wanariadha wengi zaidi.’’ Alibainisha Dkt. Ndumbaro huku akipongeza maandalizi ya mbio yenye kuzingatia viwango vya kimataifa.

Aidha Dkt. Ndumbaro aliipongeza benki hiyo kwa jitihada mbalimbali za kuendeleza sekta ya utamaduni, sana ana michezo kupitia mikakati mbalimbali ikiwemo udhamini wa michezo na huduma za kibenki zinazolenga kuwasaidia wadau mbalimbali wa sekta hizo.

Tofauti na mbio hizi, jitihada za benki ya NBC kwenye kuinua sekta ya michezo zinaonekana kupitia udhamini wake kwenye ligi za NBC Premier League, NBC Championship na NBC Youth league ambapo imewekeza kiasi cha Sh.32.6 Bilioni kwenye ligi hizo. Pia benki hii ina inashiriki katika uwezeshaji kiuchumi kwa wasanii kupitia mfuko wa maendeleo ya sanaa nchini sambamba na kusimamia kamati ya Hamasa ya Timu za Taifa ambapo mpaka sasa imeshakusanya kiasi cha Shilingi 2 bilioni kati kutokana na ahadi za awali za Sh.4 bilioni zilizopokelewa katika hafla ya uzinduzi wa kamati hiyo,’’ alisema.

Awali akizungumza kwenye mkutano huo, Sabi alisema jitihada za benki hiyo katika kuendeleza sekta ya michezo nchini kwa kiasi kikubwa inachagizwa na imani ya benki hiyo kuwa sanaa na michezo ni nguzo ya ajira na kuunganisha taifa.

“Kwa mfano kupitia udhamini wetu kwenye ligi tatu muhimu za mpira wa miguu hapa nchini, mbali na kuzalisha vipaji tumezalisha ajira za moja kwa moja zaidi ya 7,000 na mamilioni ya ajira zingine kwenye mnyororo wa uchumi. Zaidi pia kupitia mbio hizi za NBC Dodoma Marathon kwa kushirikiana na wadau wetu mbalimbali tunalenga kukusanya fedha kusaidia juhudi za Serikali katika kuboresha ya afya ya mama na mtoto kupitia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake na kutoa ufadhili kwa wakunga,’’ alisema.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro (kushoto) akipokea sweta maalum la mbio za NBC Dodoma Marathon kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi ikiwa ni ishara ya kumkaribisha rasmi Waziri huyo kwenye mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma zikiwa na lengo la  kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na  kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga  ili kuboresha afya ya mama wa mtoto Makabiziano hayo yamefanyika  makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam leo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kulia) akimpongeza Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro (kushoto) baada ya kuthibitisha dahamira yake ya kukimbia km 42 kwenye mbio za NBC Dodoma Marathon zinazoratibiwa na benki hiyo kwa lengo la  kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na  kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga  ili kuboresha afya ya mama wa mtoto. Dkt Ndumbaro  amethibitisha dhamira hiyo leo jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro (kushoto) akimpongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio za NBC Dodoma Marathon Bi Tatiana Masimba kwa maandalizi mazuri yam bio hizo zinazotarajiwa kufanyika Julai 28 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma zikiwa na lengo la  kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi na  kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga  ili kuboresha afya ya mama wa mtoto


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro (kushoto) akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mbio za NBC Dodoma Marathon pamoja mchango wa benki ya NBC katika kuendeleza sekta ya michezo nchini.   Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi



Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kulia) akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mbio za NBC Dodoma Marathon pamoja mchango wa benki ya NBC katika kuendeleza sekta ya michezo nchini. Kushoto ni Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Damas Ndumbaro.

JACKLINE SAKILU ASHINDA MBIO ZA CHONGQING INTERNATIONAL MARATHON, CHINA

March 24, 2024

 

Jackline Sakilu (TAN) competing in the women's marathon on day two of the Commonwealth Games at Cannon Hill Park, Edgbaston in Birmingham, England, on July 30, 2022. Credit : Gary Mitchell-GMP Media


Mwanariadha wa Kimataifa wa Mbio ndefu (Marathon) Jackline Juma Sakilu ashinda mbio za Chongqing International Marathon, China kwa kuwa wa kwanza kwa muda wa saa mbili na dakika ishirini na moja na sekunde ishirini na sita (02:21:26) leo tarehe 24/03/2024 na kuchukua medali ya Dahahabu.

Jackline Sakilu, amefuzu na wenzake 3 kushiriki mashindano makubwa ya olimpiki Jijini Paris, Ufaransa, wenzake waliofuzu kwa mashindano hayo ni Alphonce Felix Simbu, Gabriel Gerald Geay na Magdalena Crispine Shauri.

Tunampongeza Jackline Sakilu kwa Ushindi huo.

JK AKUTANA NA MWANARIADHA WA KIMATAIFA GABRIEL GERALD GEAY BOSTON, MAREKANI

April 19, 2023

 Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na wanariadha Gabriel Geay (kushoto kwake) na Wence Tarimo (kulia kwake) ambao walishiriki katika Mashindano ya Riadha yaliyofanyika Boston, Marekani tarehe 17 Aprili 2023, ambapo Geay aliibuka mshindi wa pili. Kulia ni Mhe. Saada Mkuya, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - Fedha na Uchumi - wa Zanzibar.
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea zawadi ya jezi toka kwa mhamasishaji mashuhuri Nick Reynolds maarufu kama Bongo Zozo wakati alipoonana na wanariadha Gabriel Geay (kushoto kwake) na Wence Tarimo (kulia kwake) ambao walishiriki katika Mashindano ya Riadha yaliyofanyika Boston, Marekani tarehe 17 Aprili 2023, ambapo Geay aliibuka mshindi wa pili. Kulia ni Mhe. Saada Mkuya, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - Fedha na Uchumi - wa Zanzibar.
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kwenye kitabu cha mwanariadha Gabriel Geay mjini Boston Marekani, siku moja baada ya shujaa huyo kushika nafasi ya pili kwenye mbio za Boston Marathon.
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na wanariadha Gabriel Geay (kushoto kwake) na Wence Tarimo (kulia kwake) ambao walishiriki katika Mashindano ya Riadha yaliyofanyika Boston, Marekani tarehe 17 Aprili 2023, ambapo Geay aliibuka mshindi wa pili. Kulia ni Mhe. Saada Mkuya, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - Fedha na Uchumi - wa Zanzibar na kushoto ni mhamasishaji mashuhuri Nick Reynolds maarufu kama Bongo Zozo.
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mhe. Saada Mkuya, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - Fedha na Uchumi - wa Zanzibar wakiwa na Watanzania waishio Marekani pamoja na wanariadha Gabriel Geay na Wence Tarimo ambao walishiriki katika Mashindano ya Riadha yaliyofanyika Boston, Marekani tarehe 17 Aprili 2023, ambapo Geay aliibuka mshindi wa pili. Kulia ni mhamasishaji mashuhuri Nick Reynolds maarufu kama Bongo Zozo na kushoto ni mtoto wa Bongo Zozo.
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi kitabu mwanariadha Gabriel Geay mjini Boston Marekani, siku moja baada ya shujaa huyo kushika nafasi ya pili kwenye mbio za Boston Marathon.

*******

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amekutana na Wanariadha Gabriel Geay na Wence Tarimo walioshiriki katika Mashindano ya Marathon yaliyofanyika Boston, Marekani tarehe 17 Aprili 2023.

Gabriel Geay aliibuka mshindi wa pili katika mashindano hayo. Mheshimiwa Rais Mstaafu amempongeza Gabriel Geay kwa ushindi mkubwa na kwa kupeperusha vyema bendera ya Tanzania.

Pamoja na wanariadha hao, walikuwepo pia wahamasishaji mbalimbali akiwemo “Bongo Zozo”. Amewapongeza pia kwa kuhamasisha ushindi huu na kufanikisha kuinua bendera ya Tanzania juu.

Mheshimiwa Rais Mstaafu yuko Boston, Marekani ambapo anashiriki katika kutoa mafunzo kwa Mawaziri wa Fedha kutoka nchi mbalimbali zinazoendelea kupitia Mpango wa Uongozi wa Harvard “Harvard Ministerial Leadership Program”.

Katika mafunzo hayo, Mhe. Saada Mkuya, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - Fedha na Uchumi - wa Zanzibar ameshiriki pia.

World Athletics makes commitment to a cleaner, greener, more equitable world

April 18, 2020
World Athletics President Sebastian Coe, Sustainable Development Advisory Group Chair Sylvia Barlag and HSH Prince Albert II are shown the air quality monitor by Kunak Technologies CEO Javier Fernandez Huerta (Philippe Fitte) © Copyright

World Athletics has today launched its Sustainability Strategy, which has a central goal of making the organisation carbon neutral by 2030. The strategy addresses global issues that pose a threat to the quality of our lives, using the power of sport and athletics to create a better world for communities.
The organisation will embrace sustainability principles and practices within its operations, its Member Federations and the organisation of future World Athletics Series events.
The ten-year strategy is designed to deliver tangible benefits across environmental, social and economic sustainability.
Among its commitments, World Athletics will reduce its carbon output by ten percent each year, switch to 100 percent renewable energy at its headquarters this year, introduce a sustainable procurement code and travel policy and develop best practice guides for its 214 Member Federations and its event organisers.
The strategy is divided into six pillars, each of which contain actions and targets for the organisation to pursue.
Some of the key components are:

Leadership in sustainability

  • Produce best practice guides for Member Federations and World Athletics Series event organisers
  • Embed sustainability principles in permit and licensing programmes
  • Align and embed sustainability goals into partnership agreements
  • Identify and engage our partners around the sustainability programme

Sustainable production and consumption

  • At headquarters, switch to 100 percent renewable energy
  • Implement comprehensive waste management system targeting reduction and reuse
  • Embed responsible procurement for all World Athletics activities and sanctioned events

Climate change and carbon

  • Reduce carbon footprint by ten percent each year to reach goal of carbon neutrality by 2030
  • Implement a sustainable travel policy reducing travel and building local capacity
  • All sanctioned events to commit to carbon neutrality targets

Local environment and air quality

  • Working with partners, establish low emission zones around athletics arenas
  • Maximise local economic impact around events by supporting local businesses
  • Develop a toolkit for improving air quality.
  • Air quality targets to be understood, set and monitored to protect runners and athletes
  • Air quality emissions to be included in equipment and venue standards.

Global equality

  • All geographic areas to have recognised opportunity pathways for both genders in all professions in athletics across athletes, coaches, technical officials, administrators
  • Build gender capacity with annual female leadership seminars conducted in all Areas

Diversity, accessibility and wellbeing

  • Protect athlete welfare with standardised basic health checks for all athletes before they compete in international events.
  • Ensure headquarters and other facilities are fully accessible
  • Ensure diverse workforce and fair treatment of staff and those working at and on our events, and for our suppliers and partners

World Athletics president Sebastian Coe said it was important for the organisation to make a commitment to a better future for coming generations.
“In the modern world, it has become apparent that our athletes and fans expect more from us than good governance of our sport. They also expect us to be a good global citizen, to take a leadership role in issues that affect the wider world and their communities. Sustainability is one of the great global challenges. We want to do our part to make this a better world and contribute to a cleaner, greener, more equitable future for everyone.
“We started on this path a couple of years ago when we made a commitment to assist the global campaign for improved air quality, and began installing air quality monitors in stadiums around the world, but it’s time for us to do more and I’m delighted to launch this roadmap for our organisation and our sport over the next decade. We have already ticked one item off the list, by switching to 100 percent renewable energy at our headquarters this year, and our ambition is to be a leader in organising sustainable events as we go forward.”
World Athletics

NGORONGORO NATIONAL OPEN ATHLETICS CHAMPIONSHIP 2019

May 01, 2019
 Katibu Mkuu Wilhelm Gidabuday , Mgeni rasmi na Viongozi wa RT
 High Jump
 Mgeni rasmi , Wanariadha na Viongozi wa RT

Serikali yakerwa na RT kutaka kuondoa jina la Alphonce Simbu katika Michezo ya Madola 2018

January 23, 2018


Mwanariadha nyota wa Tanzania, Alphonce Simbu.

Na Mwandishi Wetu
SUALA la Riadha Tanzania (RT) kutaka kuengua jina na mwanariadha nyota wa Tanzania, Alphonce Simbu limeingia sura mpya baada ya Serikali kuingilia kati.
Katika siku za hivi karibuni Katibu Mkuu wa RT, Wilhelm Gidabuday amekuwa akisisitiza kuwa mwanariadha huyo hatakwenda katika Michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Gold Coast, Australia Aprili.


Mkurugenzi wa Maendeleo nchini, Dk Yusuph Singo alisema jana kwa njia ya simu kutoka Dodoma kuwa, ameamua kuwaita Simbu, Gidabuday na Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi ili kupata ukweli wa jambo hilo.


Singo akizungumza na gazeti hili kutoka Dodoma alisema kuwa amekuwa akisikia uvumi wa taarifa hizo, lakini anapojaribu kuwaliza RT anaambiwa wamenukuliwa vibaya.


Mkurugenzi wa Michezo nchini, Dk Yusuph Singo.

Hatahivyo, mkurugenzi alisema kuwa anajua kuna kitu kinafichwa, hivyo ameamua kuitisha kikao mara moja kati ya watu hao ili kupata ukweli halisi.


Alisema kikao hicho kinaweza kufanyikia jijini Dar es Salaam au Dodoma kutegemea na nafasi yake (Dk Singo).


Alisema kuwa akimpigia simu Gidabuday anapata jibu tofauti kwani anasema waandishi wamemnukuu vibaya na akipiga kwa wengine anapata jibu tofauti, “hivyo nimeamua kuwaita kupata ukweli kamili.”


Juzi Gidabuday alisema kuwa Kamati ya Ufundi ya RT ilikutana kwadharura jijini Dar es Salaam na kuamu kutoa jina la Simbu katika orodha ya majina ya wanariadha watakaoshiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola.


Alisema wameamua hivyo ili kumuwezesha mchezaji huyo kupumzika na kujiandaa kwa ajili ya London Marathon zitakazofanyika London, Uingereza Aprili ili kujipatia fedha.

Katibu Mkuu TOC, Filbert Bayi.

Alisema mwanariadha huyo atawakilisha taifa katika mashindano ya dunia ya riadha yatakayofanyika Doha mwakani na yale ya Olimpiki Tokyo, Japan 2020, ili kulipatia taifa medali za dhahabu.


Gidabuday alisema Simbu amekimbia mashindano mengi ya kuliwakilisha taifa, ambayo yana presha kubwa, sasa anahitaji kupumzika na kukimbia mashindano ya mwaliko kama London Marathon.



Hivi karibuni Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi alisema kuwa wao kama waratibu wa michezo hiyo, hawana taarifa na kutolewa kwa jina la Simbu na kuitaka RT kupeleka barua TOC kama kweli wanataka kuliondoa jina hilo.

Katibu RT, Wilhelm Gidabuday.

Tigo yatangaza Zawadi Nono za Kili Marathon 2018

January 23, 2018


Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya simu za Mkononi ya Tigo Kanda ya Kaskazini, Henry Kinabo akizungumza wakati wa uzinduzi wa Msimu wa 16 wa Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro Marathon 2018,Uzinduzi uliofanyika katika Hoteli ya Kibo Palace Homes mjini Moshi juzi, Mashindano ambayo Kampuni ya Tigo inadhamini Mbio za Nusu Marathon,Km 21. Pichani (mwenye kofia) Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira na wadau mbalimbali. (Na Mpigapicha Wetu).

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Simu za mkononi ya Tigo imesema kuwa itadhamini tena mbio za nusu marathon za Kilimanjaro zitakazofanyika Machi 4 mjini Moshi.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mbio hizo juzi, Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya simu za Mkononi ya Tigo Kanda ya Kaskazini, Henry Kinabo alisema wanadhamini tena mbio hizo kwa mwaka wanne mfululizo.


Kinabo alisema wanaunga mkono mbio hizo, ambazo zinasaidia kuibua na kuviendeleza vipaji vya vijana na kuhakikisha Watanzania wanaishi katika maisha ya kiafya kwa kushiriki katika mchezo huo wa riadha.


Alitaja zawadi, ambazo zitatolewa kwa washindi wa kwanza kwa upande wa wanawake na wanaume, kila mmoja ataondoka na kitita cha sh milioni 2.


Huku washindi wa pili kila mmoja tazawadiwa sh milioni 1 huku mshindi watatu ataondoka n ash 650,000, wanne sh 500,000, mshindi wa sita sh 325,000 wakati wasabi atapewa sh 250,000.


Alisema kuwa mshindi wanane ataondoka na kiasi cha sh 150,000, huku mshindi wa tisa atapewa sh 125,000 na wa 10 atabeba sh 100,000.

Waziri Maghembe 'kuibeba' Rock City Marathon

August 22, 2017





Dar es Salaam;WAZIRI wa Maliasili na Utalii Prof Jumanne Maghembe mwishoni mwa wiki hii alizindua rasmi usajili wa msimu wa nane wa mbio za Rock City Marathon huku akiahidi kushirikiana na waandaaji wa mbio hizo katika kuhakikisha kuwa zinatumika vema kuutangaza utalii wa ndani.


Akizungumza kwenye hafla fupi ya uzinduzi huo iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa mchezo huo wakiwemo viongozi wa serikali pamoja na wadhamini mbalimbali wa mbio hizo, Waziri Maghembe alisema azma yake hiyo inasukumwa na malengo ya mbio hizo ambayo ni kutumia mchezo wa riadha katika kutangaza utalii hususani katika Ukanda wa Ziwa.


"Kwa kuzingatia uzito wa malengo ya mbio hizo nitamke bayana kuwa nipo tayari kushirikiana na waandaaji wa mbio hizi kuhakikisha kwamba kuanzia mwaka huu mbio hizi zinafana na zinavutia washiriki wengi zaidi hususani wa kimataifa,'' alisema Waziri Maghembe ambae pia alithibitisha ushiriki wake kwenye mbio hizo zinazoratarajiwa kufanyika Octoba 29, mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na kupita katika barabara mbalimbali za jiji hilo kabla hazijamalizikia katika uwanja huo.


Mbali na ushiriki wake,Waziri Maghembe alitoa wito kwa mashirika mbalimbali yaliyo chini ya wizara yake ikiwemo la Hifadhi za Taifa(Tanapa), Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori (TAWA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) na Makumbusho ya Taifa kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika kufanikisha mbio hizo.


"Ukanda wa Ziwa una vivutio vingi ambavyo pia kama Wizara yenye dhamana ya utalii lazima tuvigeukie na kuvitangaza kwa nguvu na kwa njia tofauti ikiwemo michezo,'' alisema Waziri Maghembe huku akivitaja baadhi ya vivutio hivyo kuwa ni pamoja na Kisiwa cha Saanane, Makumbusho ya kabila la Wasukuma pamoja na tamaduni za makabila ya wakazi wa Kanda ya Ziwa.


Mbio za Rock City Marathon zilizoanzishwa miaka minane iliyopita zinazozidi kujiongezea umaarufu kila mwaka na tayari zimefanikiwa kuwavutia baadhi ya wadhamini ikiwa ni pamoja na kampuni za TIPER, PUMA, Bodi ya Utalii Tanzania (TTB),Mwanza Hotel , Real PR Solutions Limited, Afrimax Strategic Partnerships Limited, EF Outdoor, CF Hospital na ATCL.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio hizo, Bw Zenno Ngowi alitoa wito kwa washiriki wa ndani hususani wa mikoa ya Kanda ya Ziwa pamoja na wadhamini kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mbio hizo ambazo kwa mwaka jana zilifanikiwa kuhusisha washiriki zaidi ya 2000 na watazamaji zaidi ya 30,000.


Naye Mratibu wa mbio hizo zinazoandaliwa na kampuni ya Capital Plus International, Bi Adeline Ndesanjo alisema mbio za mwaka huu zinatarajiwa kuhusisha washiriki wengi zaidi kutoka kila kona ya dunia ikiwemo Afrika, Ulaya,China,Mashariki ya Kati hususani Israel na Marekani huku akitoa wito kwa washiriki wa ndani kujisajili kwa wingi ili kuthibitisha ushiriki wao kwenye mbio hizo.


Akizungumza kwa niaba ya wadhamini wengine wa mbio hizo Meneja Masoko wa Kampuni ya mafuta ya Puma, Bw Machumani Shebe alisema ushiriki wao umechagizwa zaidi na azma ya kampuni hiyo kuisaidia serikali katika kuutangaza utalii wa ndani.


"Tukiwa kama wadau muhimu katika biashara ya mafuta hususani mafuta ya ndege tunategemea sana ustawi wa sekta ya utalii katika kuongeza soko la biashara yetu na kwa kuwa mchezo wa riadha umekuwa ukitumika zaidi katika kuwavutia watalii tukaona kuna haja ya kuunga mkono ufanikishaji wa mbio hizi,'' alisema.




WAZIRI wa Maliasili na Utalii Prof Jumanne Maghembe akizungumza na wadau mbalimbali wa mchezo wa riadha hapa nchini pamoja na waandaaji wa mbio za Rock City Marathon kwenye hafla maalumu ya uzinduzi rasmi usajili wa msimu msimu wa nane wa mbio hizo iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio hizo, Bw Zenno Ngowi akizungumza kwenye hafla hiyo. Alitoa wito kwa washiriki wa ndani hususani wa mikoa ya Kanda ya Ziwa pamoja na wadhamini kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mbio hizo ambazo kwa mwaka jana zilifanikiwa kuhusisha washiriki zaidi ya 2000 na watazamaji zaidi ya 30,000.

Mratibu wa mbio hizo zinazoandaliwa na kampuni ya Capital Plus International, Bi Adeline Ndesanjo akitoa maelezo kuhusu maandalizi ya mbio hizo kwenye hafla hiyo. Alisema mbio za mwaka huu zinatarajiwa kuhusisha washiriki wengi zaidi kutoka kila kona ya dunia ikiwemo Afrika, Ulaya,China,Mashariki ya Kati hususani Israel na Marekani .

Wadhamini nao hawakuwa nyuma!Meneja Masoko wa Kampuni ya mafuta ya Puma Energy, Bw Machumani Shebe alisema ushiriki wao kwenye mbio hizo umechagizwa zaidi na azma ya kampuni yake hiyo kuisaidia serikali katika kuutangaza utalii wa ndani.


Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.


WAZIRI wa Maliasili na Utalii Prof Jumanne Maghembe akiwa kwenye picha ya pamoja na waandaaji wa mbio hizo pamoja na wadau mbalimbali wa mchezo huo wakiwemo viongozi wa serikali pamoja na wadhamini wa mbio hizo.

WATANZANIA KUTIMUA VUMBI LONDON LEO! KUONEKANA MBASHARA DStv

August 05, 2017






Timu ya Taifa ya Riadha inayoshiriki mashindano ya Dunia ya riadha yanayoendelea jijini London inaanza kibarua cha kuipeperusha bendera yetu leo (Jumamosi 05/08/2017) ambapo mfukuza upepo Failuna Abdi Matanga atakimbia mbio za mita 10,000 leo .


Failuna atashuhudiwa na maelfu ya watanzania kupitia DStv Muda wa saa mbili usiku.

Akithibitisha kuonekana kwa matangazo hayo kupitia DStv, Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania Maharage Chande amesema DStv imefanya jitihada kubwa na kuhakikisha kuwa watanzania wanaishuhudia timu yetu ikituwakilisha katika mashindano hayo muhimu ulimwenguni.

“Tunawahakikishia watanzania burudani hii moja kwa moja kupitia DStv chaneli za Supersport. Tunaamini sote tutakuwa nyuma yao wachezaji wetu kuwashuhudia jinsi wanavyotuwakilisha” alisema Maharage

“Suala la watanzania kuwashuhudia vijana wetu wakishiriki katika mashindano makubwa kama haya lina maana kubwa sana. Vijana wadogo wakiwaona dada zao na kaka zao wakishiriki mashindano makubwa kama haya inawatia moyo na kuwapa ari na tamaa ya wao kujitahidi na kufika hatua kama hizo. Hili ni jambo la muhimu sana na sisi DStv tunalitilia mkazo sana. Ni njia moja wapo ya kuwashawishi na kuwatia moyo vijana wetu wanaochipukia na kuwajengea kujiamini”

Baada ya Failuna anayekimbia mita 10,000, watanzania watashuhudia tena shughuli pevu siku ya jumapili kupitia DStv kuanzia majira ya saa nne asubuhi ambapo vidume watatu - Alphonce Felix Simbu, Ezekiel Jafari Ng’imba na Stefano Huche Gwandu watakuwa wakikata upepo katika viunga vya jiji la Malkia London ikiwa ni mbio ndefu za kilomita 42.

Baada ya vidume hao kukamilisha kazi tuliyowatuma, wanawake wetu wa shoka nao wataingia barabarani ambapo Tanzania inawakilishwa na Sara Ramadhani Makera na Magdalena Crispin Shauri ambao nao watafukuza upepo umbali wa kilomita 42 majira ya saa nane mchana. Patashika yote hii itaonekana DStv.

Wanariadha wengine wawili wa mbio fupi za mita 5,000 ambao ni Emmanuel Giniki Gisamoda na Gabriel Gerald Geay watatimka siku ya Jumatano tarehe 9 Agosti majira ya mbili usiku hii ikiwa ni raundi ya mchujo na wakifuzu watashiriki fainali ya mita 5,000 siku ya Jumamosi Agost 12, majira ya mbili usiku. Nao pia watashuhudiwa mbashara kupitia DStv

Mashindano ya Dunia ya Riadha yalianza rasmi 1983 ambapo Tanzania imewahi kupata medali 1 tu ya Fedha kupitia mwanariadha Christopher Isegwe kwenye mbio za Marathon 2005 Helsinki Finland.

Ni mashindano ya pili kwa ukubwa baada ya Olimpiki ambapo nchi 204 zinashiriki mashindano hayo mwaka huu. Tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo mwaka huu ndiyo mwaka ambao Tanzania imeleta timu kubwa ya wanariadha 8, ambao ina mchanganyiko wa wanaume na wanawake na pia kuna wakimbiaji wa mbio za uwanjani.
Wanariadha wote wanaoshiriki wamefikia viwango vinavyotakiwa na Shirikisho la Riadha Duniani (IAAF)

Health Nusu Marathon Kufanyika Dar Aprili 26

April 21, 2017


Katibu Mkuu wa Taasisi ya Tanzania Health Summit Bi. Rebecca John (katikati) akisisitiza jambo kwa wandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akielezea maandalizi ya mbio za heart marathon na upimaji wa afya yenye lengo la kuisaidia serikali kupunguza magonjwa yasiyoambukizika mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Riadha Tanzania Bi. Ombeni Zavara na kulia ni Katibu Mkuu Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Lucas Nkungu.
Katibu Mkuu Msaidizi wa Chama cha Riadha Tanzania Bi. Ombeni Zavara akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya ya mbio za heart marathon na upimaji wa afya yenye lengo la kuisaidia serikali kupunguza magonjwa yasiyoambukizika mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Katibu Mkuu wa Taasisi ya Tanzania Health Summit Bi. Rebecca John.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Tanzania Health Summit Dkt. Omary Chillo (kulia) akifafanua jambo kwa wandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akielezea maandalizi ya mbio za heart marathon na upimaji wa afya yenye lengo la kuisaidia serikali kupunguza magonjwa yasiyoambukizika mapema hii leo jijini Dar es Salaam, katikati ni Katibu Mkuu Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Lucas Nkungu na kushoto ni Katibu Mkuu wa Taasisi ya Tanzania Health Summit Bi. Rebecca John.

……………..

Na Nuru Juma-Maelezo

Taasisi ya Tanzania Health Summit yaandaa mbio za nusu Marathon na Upimaji wa afya kwa lengo la kusaidia juhudi za serikali katika kupunguza magonjwa yasioambukiza, mbio hizo zinazotarajia kufanyika Aprili 26 katika barabara ya Kaole iliyopo Masaki jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Taasisi hiyo Rebecca John wakati alipokutana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuhamasisha jamii kushiriki.

“Kamati ya maandalizi ya ya mbio za Heart Marathon inapenda kuwa taarifu wadau wote wa sekta ya afya hapa nchini na jamii kwa ujumla juu ya mbio za Heart Marathon na upimaji wa afya ili kuungana na serikali katika juhudi za kupunguza magonjwa yasiyoambukiza” alisema Rebecca.

Aliongeza kuwa kwa mwaka huu mbio hizi zitashirikisha washiriki zaidi ya elfu mbili kutoka rika mbalimbali wakiwemo vijana, watoto, wazee, makundi ya watu wenye ulemavu na watu wenye magonjwa yasiyoambukiza.

Pia washiriki watapata nafasi ya kupima afya magonjwa mbalimbali kama vile shinikizo la damu ,wingi wa sukari katika damu, kiasi cha mafuta mwilini, uchunguzi wa uvimbe katika matiti na kupata ushauri wa wataalam kuhusiana na vyakula bora, magonjwa ya moyo na mishipa ya damu.

Aidha Bi. Rebecca aliongeza kuwa washiriki watakimbia umbali tofauti, kwani kuna mbio ndefu za kilometa 21.1 kwa ajili ya wakimbiaji wazoefu, kilometa 10 kwa wakimbiaji wa kati, kilometa 5 kwa wakimbiaji wa kawaida, kifamilia na kampuni na mbio za watoto chini ya miaka 12 ni meta 700 na zawadi itatolewa kwa mshindi wa kilometa 21.1 pekee kwa kiasi cha shilingi laki tano.

Kwa upande wake Rais wa Tanzania Health Summit Dr.Omary Chillo alisema kuwa washiriki watatakiwa kutoa kiasi kidogo cha fedha kwa ajili ya kununua flana pamoja na kifaaa maalum cha kuhesabia muda wakati wa kukimbia ila maji ya kutosha yatatolewa bure kwa ajili ya wakimbiaji.

Aliongeza kuwa wameimarisha ulinzi kwa kushirikiana na jeshi la polisi na ili kulinda usalama kwa washiriki na wananchi watakaokuwepo katika mashindano hayo.

“wananchi wasiwe na wasiwasi wa usalama kwani tutashirikiana na jeshi la polisi ili kuimarisha usalama na tumeweza kupata baraka nyingi kutoka kwao kwa kuweza kushirikiana nao” aliongeza Chillo.

Pia Katibu msaidizi wa Chama cha Riadha nchini Bi Ombeni Zavala alisema anashukuru wananchi wanavyoweza kujitokeza katika mashindano hayo na pia anawaomba wananchi hasa vijana waendelee kujitokeza kwa wingi kwani wanaweza kupata nafasi ya kuunda timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17.

Naye Sajenti Isaya Mlokozi kutoka kanda ya usalama barabarani alisema jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani litahusika vizuri katika sehem inayowahusu kuhakikisha watu wanafanya zoezi hilo kwa hali ya usalama na litajumuika na wananchi popote pale watakapokuwa wanakwenda.

Mashindano haya mwaka jana yalifanyika katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam lakini kutokana na kuongezeka kwa watu mwaka huu yatafanyikia barabara ya kaole yenye kauli mbiu ‘piga hatua moja mbele ya magonjwa sugu’

RT Yataja Majina 23 Waliochaguliwa kuunda timu ya Taifa ya Vijana

April 17, 2017
Na Mwandishi Wetu
RIADHA Tanzania (RT) imetangaza majina 23 kwa ajili ya kuunda timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 kwa ajili ya kushiriki katika mashindano ya Kanda ya Tano ya Afrika yatakayofanyika jijini Dar es Salaam mapema mwezi ujao.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa RT, Whilhem Gidabuday, timu hiyo itapiga kambi katika hosteli za Filbert Bayi zilizoko Mkuza Kibaha kuanzia Jumanne chini ya makocha Robert Kalyahe na Mwinga Mwanjala.
Timu hiyo inaundwa na wachezaji 12 wavulana wakatu wasichana katika timu hiyo wako 11 ma watashiriki katika michezo yam bio za meta 100, 200, 400, 800, 1500 na 3000 pamoja na miruko na mitupo.


Gidabuday alisema kuwa kambi hiyo itagharimu kiasi cha sh Milioni 20 kuanzia timu hiyo itakapokuwa kambini kwa karibu siku 20, wakati wa mashindano na huduma zingine.


Mbali na wenyeji Tanzania Bara, nchini zingine zitakazoshiriki ni pamoja na Zanzibar, Uganda, Kenya, Rwanda, Sudan, Sudan Kusini, Ethiopia, Eritrea na Djibout.


Timu hiyo ilichaguliwa jana mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya wazi ya taifa yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa na kuhudhuriwa na mikoa michache.
Baadhi ya wanariadha walioshiriki walitoka katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Arusha na Manyara, ambapo shule ya Filbert Bayi iliyopo mkoani Pwani, imeto wachezaji watano katika timu ya wasichana kutokana na umahiri wao.

Ukiondoa baadhi ya kasoro zilizokuwepo ikiwemo kutokuwa na huduma ya kwanza wala gari la wagonjwa, wachezaji wakishiriki bila ya kuwa na namba za kuwatambua na kuleta ugumu kwa waandishi wa habari kujua nani ni nani, mashindano yalienda vizuri.






















 

Copyright © 2015 - 2025 Athletics Tanzania All Right Reserved

Developed by Gadiola Emanuel
Theme By AP | Developed By Gadiola Emanuel