Showing posts with label Track and Fields. Show all posts
Showing posts with label Track and Fields. Show all posts

TIMU YA TAIFA YA RIADHA YAAGWA, KUSHIRIKI MASHINDANO YA “13TH ALL AFRICAN GAMES” ACCRA , GHANA.

March 17, 2024


 Timu ya Taifa ya Riadha Imeagwa na Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania Silas Isangi na Kaimu katibu mkuu Wakili Jackson Ndaweka katika uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro Leo tarehe 14/03/2024. 

Wanariadha 8 wakiwemo wa Mbio za Uwanjani, Mbio ndefu na Mrusha mkuki, wameondoka kwenda Accra , Ghana kushiriki mashindano ya Afrika “All African Games” ambayo yalianza toka tarehe 8 Machi hadi 23 Machi 2024.

Hapa Wakiwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid , na makocha na viongozi wao kufanya Majaribio "Trials" kabla ya kwenda Ghana.

hapa wanariadha na makocha wakiwa Kambini, Ngaramtoni, Arusha.

Mwanariadha Andrew Rhobi amepata muda wake Bora

March 10, 2024

 

Copyright @gettyimages

Hongera kwa Andrew Boniface Rhobi kutoka jeshi la polisi Tanzania kwa kupata muda wako bora wa dakika tatu na sekunde hamsini na moja ( 3:51.44) yaani ( Personal Best) mita 1500 (1500M) na kuwa nafasi ya Saba kwenye heat ya kwanza, kwenye Mashindano ya Dunia ya Ndani ( World Athletics indoors Championships Glasgow 2024) tarehe 1-3 Machi 2024, huko Glasgow, Scotland.

 

Copyright © 2015 - 2025 Athletics Tanzania All Right Reserved

Developed by Gadiola Emanuel
Theme By AP | Developed By Gadiola Emanuel