Matukio

< span data-type="recent" data-yes="5">

TIMU YA TAIFA YA RIADHA YAAGWA, KUSHIRIKI MASHINDANO YA “13TH ALL AFRICAN GAMES” ACCRA , GHANA.


 Timu ya Taifa ya Riadha Imeagwa na Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania Silas Isangi na Kaimu katibu mkuu Wakili Jackson Ndaweka katika uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro Leo tarehe 14/03/2024. 

Wanariadha 8 wakiwemo wa Mbio za Uwanjani, Mbio ndefu na Mrusha mkuki, wameondoka kwenda Accra , Ghana kushiriki mashindano ya Afrika “All African Games” ambayo yalianza toka tarehe 8 Machi hadi 23 Machi 2024.

Hapa Wakiwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid , na makocha na viongozi wao kufanya Majaribio "Trials" kabla ya kwenda Ghana.

hapa wanariadha na makocha wakiwa Kambini, Ngaramtoni, Arusha.

Post a Comment

0 Comments