Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kawaida wa Mwaka wa TOC unaofanyika Kituo cha Amani, Welezo Zanzibar

December 31, 2015
TOC
Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi akisoma taarifa yake ya mwaka katika Mkutano Mkuu wa TOC Kituo cha Amani Welezo, Zanzibar. Kulia ni Rais wa TOC Gulam Rashid na Mhazini msaidizi Juma Zaidi (kushoto).
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) wakati wa mkutano huo jana Zanzibar.
 







Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Gulam Rashid wakati wa ufunguzi  wa Mkutano Mkuu wa kawaida wa mwaka wa TOC unaofanyika leo Zanzibar. Kushoto ni Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi na Mhazini Mkuu Charles Nyange.




Mhazini Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Charles Nyange (kushoto) akipokea tuzo kwa niaba ya mmoja ya makampuni yaliyodhamini Siku ya Olimpiki.

Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TOC katika picha ya pamoja mjini Zanzibar.
 

RISALA YA KATIBU MKUU (TOC) KWENYE UFUNGUZI WA KAMISHENI YA WANAMICHEZO ZANZIBAR TAREHE 10/12/2015.

December 31, 2015
TOC




Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kamisheni ya Wachezaji ya Kamati ya Olimpiki Tanzania (Kawata) leo Zanzibar. Kushoto ni mwenyekiti wa Kawata, Ramadhan Zimbwe. Kushoto kwa Bayi ni Katibu Msaidizi wa TOC Jamal Adi na rais wa Toc Gulam Rashid.

 TANZANIA OLYMPIC COMMITTEE (TOC)
KAMATI YA OLIMPIKI TANZANIA

RISALA YA KATIBU MKUU (TOC), FILBERT BAYI KWENYE UFUNGUZI WA KAMISHENI YA WANAMICHEZO ZANZIBAR TAREHE 10/12/2015.

Ndugu Mgeni Rasmi Jamal Adi, Katibu Mkuu Msaidizi TOC

Ndugu Gulam Rashid, Rais wa TOC,

Ndugu Ramadhani Zimbwe, Mwenyekiti, KAWATA Taifa,

Ndugu Amina Ahmed, Katibu KAWATA Taifa

Viongozi Kamati yaUtendaji Waalikwa

Kamati ya Utendaji, KAWATA Taifa,

Wanamichezo Washiriki

Mabibi na Mabwana.

Kwa niaba ya Kamati ya Olimpiki Tanzania na kwa niaba yangu mwenyewe sina budi kumshukuru Katibu Mkuu Msaidizi wa TOC, pamoja na kuwa moja wa viongozi wa juu wa TOC kukubali mwaliko wa ofisi ya TOC kwa kuja hapa leo  kutufungulia Mkutano huu Mkuu wa Kamisheni ya Wanamichezo.

Ndugu Mgeni Rasmi, ofisi ya TOC imekuwa hapo awali ikialika wageni rasmi hasa katika shughuli hizi za ufunguzi wa mikutano yetu kutoka nje hasa taasisi na serikali, lakini kuanzia sasa itakapobidi shughuli hizi zitafanywa na viongozi wa TOC au Vyama/Mashirikisho ya Michezo.

Ndugu Mgeni Rasmi, tangu Kamisheni ya Taifa ilipoundwa hapo mwaka 2006, kazi kubwa ilikuwa kuhamasisha na kutoa wito kwa Vyama/Mashirikisho ya Michezo kuanzisha Kamisheni ya wachezaji katika Vyama/Mashirikisho yao ya Michezo. Ni Vyama/Mashirikisho chache ambayo yameitikia wito wetu kwa kufanya uchaguzi halali wa kidemokrasia.
Vyama vingi mpaka sasa vimekuwa vikiteua wajumbe wake kuhudhuria Mikutano Mikuu ya Kamisheni inayoandaliwa na TOC, lakini cha kushangaza kwa utafiti ulioofanywa na TOC/KAWATA Taifa, wachezaji hao siyo wajumbe katika Kamati za Utendaji na Mikutano Mikuu ya Vyama na Mashirikisho husika kama Muongozo wa Kamisheni unavyosema.

Sijui ni kwa nini Vyama/Mashirikisho ya Michezo yaogope kuwaingiza wachezaji kwenye chombo cha maamuzi (Kamati ya Utendaji/Mkutano Mkuu). Kuna siri gani kubwa katika vikao vya Kamati ya Utendaji na Mkutano Mkuu ambayo hayapaswi wachezaji kufahamu? 

Mimi nina imani kabisa wawakilishi wa wachezaji watakapokuwa kwenye vyombo hivyo vya maamuzi malalamiko na manung’uniko mengi ya wachezaji hayatakwepo, kwani watakuwa wameshiriki kikamilifu katika maamuzi.

Mahali ambako Mkutano Mkuu wa Kamisheni ya Wachezaji (Kawata) unapofanyikia leo Zanzibar.
Ndugu Mgeni rasmi, Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa (IOC), Vyama/Mashirikisho ya Kimataifa (IFs), ANOCA na NOCs kama TOC  zina Kamisheni zao ya Wanamichezo ambazo kazi zao kubwa ni kama:

1.     Kutoa ushauri, nasaha kwa wanamichezo waliostaafu na ambao bado wanaendelea na michezo.
2.     Kulinda maslahi ya wanamichezo ndani ya maadili ya Olimpiki.
3.     Kutoa mapendekezo kwa mambo yanayohusu maslahi ya wanamichezo ndani ya vikao ya Kamisheni husika.
4.     Kufanya lolote lile ambalo ni kwa faida ya wanamichezo kwa ujumla wake.

Kamisheni yetu ya Kitaifa tangu ianzishwe mwaka 2006 na wajumbe wake Kitaifa kuchaguliwa tena mwaka 2012 mjini Dodoma  imechelewa kwa kiasi fulani kutokana na sababu ambazo ni pamoja na kukwamishwa na viongozi wa Vyama/Mashirikisho yao Kitaifa (NFs).

Baadhi ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa Kawaita mjini Zanzibar leo Alhamisi.
Wanamichezo wana uwezo mkubwa wa kushauri viongozi wa vyama/mashirikisho yao katika masuala yanayohusu maendeleo ya michezo, pia kushauri mashirika mbalimbali kuhusu ajira za wanamichezo pamoja na hali ya baadaye mchezaji mhusika anapostaafu.

Mhe. Mgeni Rasmi, michezo kwa sasa ni ajira, ndiyo maana IOC imehamasisha NOCs kuunda Kamisheni za Wanamichezo ili watambuliwe kuwa sekta muhimu ya maendeleo ya michezo katika Taifa letu.

TOC  inaamini kwamba kukiwa na uwakilishi wa wanamichezo katika vyama/mashirikisho ya michezo na asasi za umma nchi yetu itakuwa imepiga hatua katika kupiga vita madawa ya kuongeza nguvu katika michezo ambayo kwa sasa yamepamba moto duniani.
Baadhi ya waalikwa katika mkutano Mkuu wa Kamisheni ya Wachezaji Tanzania (Kawata) Kutoka kushoto Irine Mwasanga, Peter Mwita na Mwinga Mwanjala wakati wa mkutano huo leo Zanzibar.
Mhe. Mgeni Rasmi, bado vyama/mashirikisho ya michezo ya kutothibitisho yanaendelea. Mwaka huu kutoka Bara ni Vyama/Mashirikisho ya Kuogelea, Mpira wa Magongo na kwa Zanzibar Mpira wa Meza na Kikapu havikuthibitisha, lakini wakatma washiriki. Riadha Tanzania kuwasilishwa na wajumbe 3 (wm 2, mk 1).

Kwa haya machache naomba nikukaribishe ili uzungumze na wanamichezo walio mbele yako kisha utufungulie Mkutano huu wa Kamisheni ya wanamichezo kwa mwaka 2015 kama tulivyokuomba.


Ahsanteni kwa kunisikiliza.




Katibu Mkuu wa TOC Filbert Bayi akifuatilia jambo na mjumbe wa Kamati ya TOC Irine Mashanga wakati wa Mkutani Mkuu wa Kawata Zanzibar .
 



Katibu msaidizi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Jamal Adi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kamishenu ya Wachezai (Kawata) Zanzibar. Kulia kwa Adi ni Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi.

HOTUBA YA MGENI RASMI WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO MKUU WA KAMISHENI YA WACHEZAJI TANZANIA (KAWATA) ULIOFANYIKA ,ZANZIBAR

December 31, 2015
TOC


 
Ndugu Gulam A. Rashid, Rais wa Kamati ya Olimpiki ya Tanzania,

Ndugu Filbert Bayi  Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania,

Ndugu Viongozi wa Kamisheni ya Wachezaji Tanzania,

Wageni Waalikwa,

Mabibina Mabwana.

Awali ya yote, napenda kutoa shukrani zangu kwa viongozi wenzangu wa TOC
kwa kunishirikisha na kunipa heshimahiiyakuwamgenirasmiwakuufunguaMkutanohuumuhimuwaKamisheniyaWachezaji Tanzania.

Kwanza naipongezaofisiyetuyaKamatiyaOlimpiki Tanzania kwakutekelezamaagizoyaKamatiyaOlimpikiyaKimataifayakuzitakaKamatizaOlimpikizaKitaifakujumuishawachezajikwenyeKamatizakezaUtendaji, naMikutanoMikuuyakehalikadhalikanaVyama/MashirikishoyaMichezowanachamawa TOC ambaomichezoyaoipokwenyeratibayaMichezoyaOlimpiki(Summer/Winter).

Ni matumainiyanguwengiwawawakilishiwaliohapaniwajumbehalaliwaliochaguliwanawachezajiwenzaondaniyaVyama/Mashirikishoyamchezohusikakwanjiayademokrasianasiyokuteuliwanaviongoziwavyama/mashirikishoyamichezoyenu, vile vilekutokaamadarakanizaidiyamudawauongoziambaoukokwenyemwongozowenukamamlivyoelekezwanaKamatiyaOlimpikiyaKimataifa (IOC) kupitiaKamatiyaOlimpikiyaTanznaia (TOC).

NatoawitokwaviongoziwaKamisheniyaWachezajiwanaowakilishavyama/mashirikishoyamichezokusaidiananaviongoziwaVyama/Mashirikishohusikailikamahavipohai, basiwajitahidikuvifufuakwamaanayakufanyauchaguzikwamudamuafakakufuatakatibazao. Kuna michezominginehufakutokananakutokuweponamsukumokutokawadauwavyama /mashirikishoyamichezoambaoniwachezaji. ViongoziwaKamishenikatikavyama/mashirikishovinawajibuwakusaidiamaendeleoyamichezokatikataifaletukupitiavyamanamashirikishoyao. Kamishenizilizochaguliwanazilizopoziwezekutoachangamotoyaushauriwanamnayakuendeshamichezonchini, kwanihadiduzarejeazakazizaonipamojanakuamshaariyawachezajiwenginewakitaifanakimataifakatikakufikiamahalipazuri pa kupatawachezajiwatakaowakilishavilabu, vyamanamashirikishoyetukatikangazimbalimbalizamashindano.KAWATA kuanziangaziyaVyama/MashrikishoyaMichezohadiTaifahaziwezikukwepalawamawakatitimuzetuzinapofanyavibayakatikaMashindanoyaKimataifa.

Nimefahamishwakuwawachezajiwengipamojanakwambammekamilikahapakuhudhuriamkutanohuu, lakinindaniyavyama/mashirikishoyenuhampewinafasiyakuwamojawawajumbewaKamatizaUtendajizaVyama, MashirikishonaVilabuvyamichezonakuwananafasiyauwakilishiwenyekurakatikaMikutanoMikuu.Ndaniyanafasihizokunamaamuzimengineyanawahusuwachezajiambaondiyowadauwakubwawavyombovyetuvyamichezohapanchini, lakinimaamuzihayoyamekuwayakiamuliwanaviongoziwavyama/mashirikishoyamichezo,ndiyomaanaTOC naIOC wakalionahilinakuamuawawepowawakilishiwaWachezaji. Ni matumainiyangukamamojawaviongoziwa TOC,VyamanaMashirikishoyaMichezo Tanzania Bara na Zanzibar wametekelezamaagizoya IOC kwafaidayaMichezokatikanchiyetu. .
  
Viongozi wa Kamisheni ya Wachezaji Tanzania Kawata), Katib u Mkuu Amina Ahmed (kushoto) na mwenyekiti wake, Ramadhabi Zimbwe pamoa na Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Filbert Bayi wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kawata leo Zanzibar.
Binafsi, ninaungakabisaumuhimuwaKamisheniyaWachezajikatika TOC, Vyama/MashirikishonaVilabuvyaMichezo, huuniuamuzimzuriwaKamatiyaOlimpiki Tanzania (TOC)naKamatiyaOlimpikiyaKimataifa (IOC), nanikatikakukamilishaazmayamaadiliyaOlimpikihasakuwapawachezajihakiyakutoamawazoyaokatikaKamatizaUtendajizaVyama/Mashirikishona TOC. 


PiaKamishenikupitiaVyama/MashirikishoyetuyaMichezoipingekwanguvuzoteutumiajiwamadawayakuongezanguvukatikamichezoambakokwasasaumeongezekakwakasi.Shirikisho la Riadha la Kimataifa (IAAF) imeshaanzakupambanananchiambazowanariadha wake wamekuwawakitumiamadawayakuongezanguvukatikariadha.

KamisheniivihamasisheVilabunaVyamavyaMichezokuwanaKamishenizaoilizisaidiemaendeleoyamichezohapanchini, msikubalidaimakutumwakatikamikutanokamahiikwakuteuliwabilakuchaguliwa.

KwahayamachachesasanikotayarikufunguarasmiMkutanowenunakuwatakiakila la kheri.


Ahsanteni kwa kunisikiliza.
 
Baadhi ya wajumbe wa Kamisheni ya Wachezaji Tanzania (Kawata) wakiwa katika mkutano mkuu wao leo Zanzibar.

Mkuu wa Wilaya ya Karatu ndiye mgeni rasmi tamasha la michezo la mwaka huu la Karatu

December 31, 2015
TOC

Baadhi ya wanariadha nyota wa kike wakichuana katika mbio za kilometa tano za Karatu mwaka jana

Na Mwandishi Wetu
MKUU wa wilaya ya Karatu, Omary Kwaanq anatarajia kuwa mgeni rasmi katika ufungaji wa tamasha la michezo la Karatu Jumamosi Desemba 19 kwenye Uwanja wa Mazingira Bora, imeelezwa.

Mratibu wa tamasha hilo, ambalo hufanyika kila mwaka mjini Karatu, Meta Petro alisema kuwa, mkuu huyo wa wilaya ndiye atakayetoa zawadi kwa washindi wa michezo mbalimbali katika tamasha hilo.

Baadhi ya waratibu wa mbio hizo wakijadili mambo wakati wa mbio za mwaka jana.
Alisema kuwa mbali na riadha, ambayo itashindaniwa katika mbio za kilometa 10, tano na 2.5, pia kutakuwa na michezo ya mpira wa wavu, soka, mbio za baiskeli na burudani za kwaya na ngoma.

Akizungumzia riadha, Petro ambaye aliwahi kuwa mwanariadha wa kimataifa wa Tanzania katika miaka ya nyuma alisema kuwa, wanariadha kibao nyota wamethibitisha kushiriki tamasha hilo katika mbio za kilometa 10 na tano, kwa wanaume na wanawake.
Wanariadha wa mbio za kilometa 10 za tamasha la Karatu wakijiandaa kuanza mbio za mwaka jana.
Aliwataja baadhi ya nyota waliothibitisha kushiriki mbio hizo kuwa ni pamoja na Fabian Nelson, bingwa wa mwaka huu wa Ngorongoro Marathoni Joseph Teophilo, bingwa wa Kilimanjaro Marathoni kwa wanawake, Abiola William na Bazil John.

Alisema kuwa mchezo wa soka ulianza leo Jumatano hatua ya wilaya, ambapo mshindi wa leo atacheza Ijumaa na mshindi wa kesho katika hatua ya fainali, ambapo mshindi ndiye atakuwa bingwa wa mwaka huu katika soka.
Mshindi wa mbio za kilometa tano kwa wanawake, Failuna Abdi akipewa zawadi na rais wazamani wa Riadha Tanzania, Francis John. anayeshuhudia ni mratibu wa mbio hizo, Meta Petro.
 Mbali na riadha na soka, mchezo wa mbio za baiskeli ambao huwa na msisimko wa aina yake,wenyewe utashindanisha washiriki katika umbali wa kilometa 60 kwa upande wa wanawake na wanaume.
Muandaaji wa tamasha la michezo la Karatu, Filbert Bayi (katikati), akiwa na washindi baada ya kukabidhiwa zawadi zao katika tamasha la mwaka jana mjini Karatu.

Tamasha la 14 la michezo na utamaduni la Karatu lilivyong'ara mwaka huu

December 31, 2015
TOC



Na Cosmas Mlekani, Karatu
TAMASHA la 14 la Michezo na Utamaduni la Karatu lilimaliziki mwishoni mwa wiki, huku likifungwa na Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Omary Kwaanq.
Mbali na riadha, tamasha hilo ambalo hufanyika Desemba kila mwaka, linashirikisha michezo ya soka, mpira wa wavu, mbio za baiskeli na ngoma za utamaduni pamoja na kwaya.
Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Omary Kwaanq (kulia), akienda kuanzisha mbio za kilomita 10 za Karatu. Kushoto ni mratibu wa tamasha hilo la michezo, Meta Petro na nyuma ni rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania Gulam Rashid.
Tamasha lengo kuu la tamasha hilo ni kuibua na kuendeleza vipaji kwa watoto na vijana wa Karatu na vitongoji vyake na Tanzania kwa ujumla ili kuwawezesha kutumia michezo hiyo kupata ajira.
Kwa hivi sasa michezo imekuwa ni ajira kubwa sana duniani, hivyo vijana wa Tanzania pia wanatakiwa kutumia fursa hizo kujipatia ajira kama wenzao wa nchi zingine kama Kenya, Ethiopia na hata nchi zilizoendelea kama Marekani, China na zingine.

 
Timu pia zilichuana katika mpira wa wavu katika tamasha hilo la Michezo la Karatu.
Tamasha hilo lilianzishwa miaka 14 iliyopita na bingwa wa dunia wazamani wa mbio za mita 1500 Filbert Bayi akiwa na lengo la kuibua vipaji katika mchezo wa riadha ili kupata nyota wengine wa mchezo huo hapa nchini, ambao watangara kimataifa kama alivyongara Bayi.
Kama inavyoeleweka kuwa maeneo hayo ya Karatu, Mbulu na kwingineko katika mikoa ya Arusha na Manyara kuna vipaji vingi vya wanariadha kama alivyo Bayi, lakini vinakosa watu wa kuviibua na kuviendeleza, hivyo Bayi kupitia Filbert Bayi Foundation (FBF), aliamua kuanzisha tamasha hilo.
Katibu wa Kamati ya Wanawake ya Kamati ya Olimpiki Tanzania, Nasra Juma akiigagua timu ya Karatu kabla ya kuanza kwa fainali dhidi ya Magereza.
Hatahivyo, miaka ilivyokwenda Bayi aliamua kuongeza baadhi ya michezo pamoja na vikundi vya utamaduni ili kuwaongezea vijana fursa ya kujiajiri.
Michezo iliyofuata baadae ni pamoja na soka, baiskeli, mpira wa wavu na mingine ambayo baadhi yao sasa haichezwi tena kama netiboli.
Nasra akikagua timu ya Magere, ambayo ilifungwa 3-0 katika fainali dhidi ya Karatu.
Kwa upande wa riadha mchezo huo umekuwa na msisimko wa aina yake, ambapo pia umeibua vipaji vya wanariadha wengi nyota ambao sasa wanatamba hata nje ya mipaka kama akina Fabian Joseph, Dickson Marwa, Alphonce Felix na wengineo.
Pia kwa upande wa utamaduni kumekuwa na vikundi kama vya Sangoma Mbulumbulu, ambavyo kwa njia moja au nyingine mbali na kueneza utamaduni pia hutoa ujumbe mahsusi kama ule wa gonjwa hatari la Ukimwi ili kutoa elimu kwa wananchi wa Karatu na vitongoji vyake.



 


Wachezaji wa timu ya Karatu wakishangilia kwa staili ya `Magufuli" (wakipiga pushapu baada ya kufunga bao la pili dhidi ya Magereza katika mchezo wa fainali.


Makamu mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Wavu Tanzania (TAVA), Muharami Mchume akikagua moja ya timu za wavu zilishiriki tamasha hilo la michezo la Karatu.







Sekretarieti ya tamasha la Karatu wakiwa kazini kwenye viwanja vya Mazingira Bora mjini Karatu.


Washindi wa kwanza wa baiskeli kwa upande wa wanawake ns wanaume wakiteta baada ya kumaliza mbio hizo za Karatu za kilomita 30 na 60 katika viwanja vya Mazingira Bora Karatu.
 




Usalama ulikuwa wa kutosha katika tamasha la Karatu, ambapo walikuwepo askari wa usalama barabarani, gari la wagonjwa na mgambo ili kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa kwa mujibu wa taratibu za mashindano ya kimataifa.
Pikipiki ikiendeshwa na John Mwingereza ikiongoza wanariadha wa mbio za kilomita 10.
Mwenyekiti wa Taasisi ya FBF, filbert Bayi (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Omary Kwaanq wa pili kutoka kushoto) na makamu mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Wavu Tanzania (Tava), Muharami Mchume kabla ya uzinduzi wa mbio za kilomita 10.

Mary Naali akimaliza wa tatu katika mbio za kilomita tano za wanawake za tamasha la Michezo la Karatu nyuma ya Angelina na Failuna Abdi waliomaliza wa kwanza na pili.
 

Copyright © 2015 - 2025 Athletics Tanzania All Right Reserved

Developed by Gadiola Emanuel
Theme By AP | Developed By Gadiola Emanuel