Matukio Mbalimbali katika mbio za DODOMA HAPA KAZI TU HALF MARATHON

February 05, 2016

 Picha Zote na Gadiola Emanuel, Dodoma. 0755 643 633
Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa akifika kwenye banda la kuandikishwa washindi wa mbio hizo za HAPA KAZI TU Dodoma Half Marathon iliyofanyika tarehe 30 Jan, 2016 Mjini Dodoma.
Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa akielekea jukwaa kuu baada ya kukimbia km 2 katika mbio za HAPA KAZI TU Dodoma Half Marathon iliyofanyika tarehe 30 Jan, 2016 Mjini Dodoma.

Mhe. Waziri mhe. Majaliwa (katikati), Naibu Spika (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Chiku Galawa (kulia)

Waziri Mavunde baada ya kushiriki mbio hizo
Mwanamuziki Stara Thomas nae alishiriki

Waziri Angellah Kairuki, Mama Samwel Sitta na Waheshimiwa wengine walishiriki
watoto hawa nao walishiriki mbo hizo
Officials wa chama cha riadha nchini, wakiongozwa na Filbert Bayi wakipanga mipango mbali mbali
washiriki wa mbio za km 21.1 wakijiandaa


Waziri Nape Nnauye




Waziri Mkuu akijiandaa kupuliza filimbi ya kuashiria kuanza kwa mashindano ya km 21.1 ya wanariadha wazoefu.

Filbert Bayi : Race that stopped a nation

February 03, 2016
TOC

Filbert Bayi to a risk in lead from the front at the start of the 1974 Commonwealth Games 1500m race. Photo / Herald archives

By Michael Brown
Forty years ago on Sunday at the 1974 Commonwealth Games in Christchurch

The world witnessed one of the greatest middle distance races of all time.


Some say it was the greatest-contested by one of the best fields for a major competition. This is their story.


The Buildup

The track and field meeting burst into life on the opening day when Dick Tayler won gold for New Zealand in the 10,000m and continued with a series of top performances in the 800m, 5000m, 3000m steeplechase and marathon.

But there was tremendous excitement as the field lined up for the 1500m, a field that included three medallists from the 1972 Olympic Games - Rod Dixon (bronze in 1500m), Ben Jipcho (silver in 3000m steeplechase), Mike Boit (bronze in 800m) - as well as England's Brendan Foster, who won bronze in the 1500m at the 1970 Commonwealth Games, top Australian Graham Crouch and 1980 Olympic 5000m silver medallist Suleiman Nyambui And John Walker and Filbert Bayi.

Keith Quinn (TVNZ commentator)

I wrote a preview for the Listener a couple of weeks out from the Commonwealth Games and said I thought one of the highlights might be the 1500m race between John Walker, Rod Dixon and Filbert Bayi. Some smart sub-editor at the Listener thought there was no way anyone would have a name like Filbert so changed it to Gilbert Bayi. I was furious. Of course, in those days, I knew everything.

Rod Dixon (New Zealand)

At a race in Wales in 1973, John came up alongside me and passed me. I knew then, as the bronze medallist from the last Olympics, I was in trouble. At the trials for the Commonwealth Games, John beat me well and truly. I went back into training but was having some trouble with back pain. I had pinched a nerve and couldn't shake it off, but I went to the Cooks Gardens Mile and beat him. That put me on an even footing with John but I was still very aware of his potential.

John Walker (New Zealand)

My coach said it would be fast. He said to me I would have to break a world record to beat Bayi. I said, 'no way. I can't run that fast'. I had run 3.38 and to improve another five seconds I couldn't comprehend that. Arch reassured me that I would do it and I would break the world record.

Brendan Foster (England)

I had already run the 5000m against Jipcho. We ran the second and third fastest 5000m in history and it was a really close finish - he just beat me on the line - so my preparation was all for that. Because it was the Commonwealth Games and I had run the 1500m in the past - I got a medal in the 1970 Games - it was just like an extra race for me. I was enjoying all the buildup. I already had my medal and had run a really good race.

Dixon

As the Commonwealth Games approached, I hurt my back again. I couldn't come to the opening ceremony and stayed in Nelson to get treatment. I remember John running in the 800m when he got third and I knew with Walker and Bayi we had a 1500 final that was going to be a hell of a race.

Graham Crouch (Australia)

In Stockholm in 1973, Jipcho beat Bayi in a mile race in 3.52. They would both be in Christchurch, so I knew from then on how the race would be run. With Dixon, Foster and Boit all in Munich in 1972, and having been in Canada in 1973 with the emerging Walker, I knew I was preparing for a "hot'' race. I left Europe knowing what I had to prepare for. My training from then on was based around the expectation of Bayi running through 800m in 1.52.

Filbert Bayi (Tanzania)

I preferred to run that way after what happened at the Munich Olympics in 1972 when there was a lot of jostling and pushing. I thought then, 'why not run in front by myself?'

Walker

I had never seen Bayi before. I had heard about him and knew the way he ran but I didn't think he would do that in the final.

Bayi

Going out fast was my style and a new revolution of middle distance running - catch me if you can. I planned for both the heats and finals of the 1500m one week earlier, just after I arrived and got used to the atmosphere of Christchurch. I knew my front running would work due to the training and time trials I did in competition before arriving in New Zealand. There was no doubt about my tactics due to the fact I knew all my opponents.

Ralph King (New Zealand Herald Jan 31)

The top-ranked 1500m runner in the Commonwealth, F Bayi of Tanzania, should also qualify [for the final] but as Walker came from considerably behind to sprint him out of the 800m bronze medal on Tuesday, neither Dixon nor Walker will hold any fears of him.

Quinn

It wasn't always clear Walker was going to be the better of the New Zealanders. After all, Dixon had won bronze at the Munich Olympics two years before in the same event so was highly rated. Walker was seen in 1972 as an 800m man. I think he and Bruce Hunter the All Black should have gone to Munich in the 800m. Both had qualified but the New Zealand Olympic Committee, in their wisdom, took neither.

Arch Jelley (Walker's coach)

I remember the week before [the Commonwealth Games] John had to run a 400m race in preparation for the 800. He ran 49.9, which was very slow for him but he had been lying in the sun all day and by the time he had got to his race he was a bit fatigued. The press wrote him off. I was in Auckland but I thought I should go down right away so I went down and put him over 600m and he did a personal best. I said to him, 'look, boy, you're in great shape, don't worry about your 400'.

Walker

I was in the best shape of my life, probably better shape than I was at the Olympics [in 1976]. But I couldn't see myself getting a medal. I was young and naive. I had only run three 1500s in my life. I classified myself as an 800m runner and I had already got a medal in that. Anything I did in the 1500 was a bonus because the calibre of the field was very strong.

Jelley

The day before [the 1500m final] he came out to my brother's place where we were staying and we had a game a cricket, not that John was a cricketer. The bat was only a foot long and we played for a few hours. John did a lot of bending down. When he work up the next morning he was a bit stiff with all his bending.

Walker

I woke up the next morning so stiff and sore I could hardly walk. I was using muscles I don't normally use. I had to do an extra 20 minutes warmup.

Jelley

He went for a bit of a run. I remember someone yelling out, 'who do you think you are? Are you training for the Olympics?' There was never a truer word.

The Start Line



By the time the competitors lined up for the 1500m final, the last race on the Commonwealth Games programme, there was intense interest in the contest.

Quinn

The event badly needed a race like Dick Tayler's to lift the crowd. We didn't really understand the Commonwealth Games and it took the excitement of Dick Tayler's race to lift interest in track and field. If you look at the back straight on the first day it's empty but after Tayler won - and it was a big colour TV event being the first time we had seen colour TV at a summer sports event in New Zealand - that sparked the interest. By the time the 1500m race came, you couldn't get a seat. It was fantastic.

Foster

Before the race, there was plenty of chatter. We all knew what the guy was going to do and, because it was a the Commonwealth Games, everyone could speak English. 'My god, he's going to go out and he's probably going to out earlier than we think'. My compatriot, John Kirkbride said, `are you going to go with him, it's a stupid way to run a 1500m race? I said, `John, we've got no choice'.

Dixon

Walker had the image of Bjorn Borg with the long hair. He knew this was his moment. He felt the crowd had come to see him. He was strutting his stuff but that was John. We never talked about running for New Zealand. John was running for himself and Rod was running for himself. Being a bit more of a romantic than John, I thought it would be cool to have a one-two for New Zealand like Snell and Davies in Tokyo in 1964 (ed - Davies was third in Tokyo). Obviously I wanted to be first and John second.

Jelley

At that time we didn't know John would even be placed in the race. He was a 3.38 runner and all these guys were 3.34, 3.35 so he was by no means the favourite.

Quinn

David Coleman of the BBC was right behind us. We were very envious because he had a young lad who just looked after him for the Games. We would often see this lad running milkshakes, Coca Cola or pies up the aisle to David Coleman. He was incredibly powerful and had the big reputation, too.

The Gun

Almost immediately, Bayi opened up a sizeable gap on the rest of the field.

Walker

I wasn't going to run with him. I didn't think I could run that fast. Here was me, five seconds slower. I had to sit back. I thought Dixon was the man to get me up there. He was the Olympic bronze medallist and was going to be my savour. I would follow him because I had beaten him a couple of times.

Crouch

My plan was to go with the group, knowing Bayi would be out front. I was comfortable with the pace because all my training for the previous six months had been preparing for it. Jipcho had caught Bayi in Stockholm, so my plan was to stay with the following group.

Dixon

Bayi sprang out and, although he didn't run away from us, he got this incredible gap. Traditionally in the 1500, everyone lazily takes off. If you want to put any distance on anyone, you have to do it in the first 150m. You can catch a lot of guys napping.

Foster

The 1500m up to that point had been steady for three laps and then a sprint. Filbert changed the rules.

Jelley

We thought Bayi would go out fast like he had done in Europe. In every other race he had gone out fast and folded so we thought we would let him go and fight it out with the rest.

Dixon

John and his coach had decided they were going to watch me and follow me. I sensed that.

The First Lap

 The First Lap

Bayi took just 40.6 seconds to reach the finish line for the first time, which was five seconds faster than Jim Ryun had done when setting the world record in 1967, and covered the first 400m in 54.4 seconds. He had a 10m-gap on the rest of the field.

Foster

Unfortunately his first lap was about 54 seconds and I thought there was no way you could run 54 seconds and keep going - certainly I couldn't. The race went on at a furious pace. It was like oxygen debt after 200m and it was a case of hanging on. It was a real test of strength. It was more like a distance race than a 1500m race. The guy was phenomenal.

Walker

I thought I was running pretty smart. He went through in 54 and I went through in 57. I felt good. I felt so good during that race.

Bayi

After the first lap, I knew something was going to happen - winning gold, improving my previous best time over 1500m or even breaking Jim Ryun's world record. It was going according to my plan, [and I] recalled my race with the great 1500m Kenyan athlete Kip Keino when I beat him in Lagos, Nigeria, at the All Africa Games and used the same tactics.

Dixon

I felt that, like the Olympics, if it was hard from the gun I had a better chance. I was a strength runner rather than a speed runner. When Bayi went out I thought, 'this is good'. Once he set his pace and wasn't running away I knew we had the potential to catch him with 600m to go. I felt we would catch him - strength in numbers. He was the hunted and knew it.
Continued below.

Related Content


New management structure for Jacko Gill


Quinn

Our commentary was good. At one stage (co-commentator) John Davies said as a little sidebar, 'there's Filbert Bayi. Back in Tanzania he trains by running through the jungle and sometimes when he runs home from school he gets chased by a tiger'. The TVNZ switchboard in Auckland lit up with people shouting down the phone, `tell that commentator there are no tigers in Africa'.

The Bell



Bayi's third lap of 59.5 seconds was the slowest but he still had a significant lead when the bell signalled the final 400m.

Bayi

At the bell I looked over my shoulder and saw the chasing group closing on me. I then accelerated and widened the gap again but at the same time saving my strength for the last 50 or 100m when Walker, Jipcho, Dixon and others were good.

Dixon

I knew something was going on. We didn't watch a video board like runners today. I could hear the times and I knew we were running fast, which suited me fine. I liked the pace. I thought the pace was great.

Crouch

I was concentrating on the group around me only, and thinking the move is being made to chase him down.

Foster

I thought Bayi was running too well. He was running brilliantly. He was the only one accustomed to going out like that because he had tried it a few times. It hadn't always come off but you knew he was getting stronger and better.

Jelley

I thought it would be difficult (to catch Bayi). It was quite a significant gap. But on every previous occasion Filbert Bayi had folded and everybody had caught him. This was the exception.

Dixon

There was nobody else prepared to go after him. We were coming up with a lap to go and I had to take over. I thought, 'I'm going to run this last 400 as hard as I can. I'm not going to sit around and wait for a sprint. I have to go out'.

Walker

Rod didn't go. That was the problem. I needed someone to go and I would go with them. That was my gameplan. I was a 21-year-old and didn't really know much better. When he didn't move I got frightened.

Bayi

With the training I did prior to the Games, I was confident anyone trying to close the gap over the last 100 or 200m had to be ready for the challenge.

Dixon

I led around the top bend and down the back straight and that was when Jipcho and Walker passed me. Going into the bottom turn I sensed Jipcho was starting to fade and I could see Walker closing on Bayi. I knew I had to keep my speed going.

Walker

I started moving with about 200m to go. I got on the outside of Rod. I was waiting for him to go but he never went. Then I realised [I had to go]. Bayi was still too far in front so I chased him and I ran hard around the bend. Really hard.

Bayi

I looked back several times to see how far the guys were behind. I saw Walker closing the gap. That made me relax and wait for the big sprint.

Dixon

Coming up the home straight, I was picking up a little bit but, as I was becoming a little more desperate because I wasn't catching him, I tried to run faster and as soon as you do that you go into oxygen debt. I was fading and Jipcho came back and claimed third. I was fourth.

Bayi

With 50m to to to the finish I sprinted. I am sure that sprint helped me to break the world record. Thanks to Walker who really pushed me to find last gear.

Walker

I wasted too much energy trying to catch him. By the time I got to the straight, it looked like I was catching him but I wasn't. He was still holding me the whole way. I was tying up at 90m. He never slowed down. He won that race. Not me. He didn't die. If I had got up to him, he might have faltered because there's a big difference when there's pressure on but he never died.

The Finish Line


Bayi crossed the tape in 3.32.2 to set a new world record. Walker was second in 3.32.5, which also broke Ryun's record of 3.33.1, with Jipcho third in 3.33.2. As well as a new world record, five new national records were set. Bayi and Walker immediately embraced, exhausted, but exhilarated.

Quinn

When Bayi crossed the line, we all jumped out of our seats and said, 'world record, 3.32.2'.

Walker

I was absolutely ecstatic, delighted. I said to Filbert, 'you've broken the world record' and he said, 'so have you'. He wanted me to do a victory lap with him and I said, 'no, it's your time, you have broken the world record'. He insisted and I felt a bit embarrassed.

Bayi (This is Your Life)

It really was a surprise [to see Walker second] because I had not heard of him before. I said, 'who is this guy who came behind me?'

Dixon

How is it I can run the fifth fastest time in history and finish fourth in a race?

Foster

When I crossed the time and saw the times I thought, 'wow, look at that'. I knew Filbert had won but I didn't know some of the other results. Nobody could live with Filbert. He was at the limit of human endeavour at that time. In those days we didn't have pacemakers. Filbert was a fantastic pacemaker but he just kept going. He was changing the rules. People only broke world records when they had pacemakers. The pacemaker broke the world record that day. It was a new era in distance running.

Bayi

I was so happy to win the gold, but when I looked at the screen and saw the screen flashing, 'world record' I was even happier. I jumped up and down while going for the victory lap.

Jelley

When John failed to catch Bayi I was a bit disappointed but then I looked at my watch. I'm usually fairly quiet and just concentrate on the race. Instead of being the usual quiet coach, I jumped onto my seat and started yelling out, 'it's a world record, it's a world record'.

King (NZ Herald, February 4)

It was the most glorious metric mile in history.

Crouch

Fellow Australian athlete Randall Markey kept saying, 'I wasn't even in the home straight'. His coach had believed he could win.

Dixon

I stood there in total amazement. I walked off the track and someone called to me, 'loser'. I thought, 'shit, come on, I ran the fifth fastest time in history. I know I finished fourth but was only three steps away from winning. How can I be a loser?' In fourth place you don't get any prizes. I experienced that again in '76. Fourth is not a good place.

The Aftermath


Walker

If I had the race again, I would have beaten him. I would have gone with him. It's pretty arrogant saying it now but it taught me a lot. I proved it by going with him at the Helsinki World Games which was only six months later and beat him by 35m. When he went out in front ... I couldn't do it and nor could anyone else. He dictated the race so he could go fast or slow. There was no pressure on him.

Foster

The great thing was that Jipcho, Walker and Dixon were even able to compete with him. The New Zealand crowd saw what I believe, apart from the first four-minute mile, the most significant mile/1500m race in history. When you look back on it, it is still a wonderful performance by Filbert Bayi. There wasn't a human being living who could have got anywhere near that. That was his moment. Sadly he didn't get a chance in '76 (because of the African boycott of the Olympics). When I see who was behind him - Mike Boit, Walker, Dixon, Jipcho, Graham Crouch - and I was in seventh setting a British record... it was an amazing bunch of athletes and it was the beginning of a new era. In those days athletes didn't come together every couple of weeks for Diamond League events. To be part of such an historic event was absolutely fantastic.

Bayi

I [felt like I changed middle distance running] but I'm not sure if world knows that. Nothing much has been talked about my front-running. Today, in any distance starting from the 800m, pace setters (rabbits) are there to help an individual break a world record and these are the people who are inducted into the Hall of Fame by the IAAF. I have been attending Commonwealth Games since Manchester in 2002. In all these Games, nothing has been mentioned about my unbeaten 1500m Commonwealth record which, for five years (1974-1979) was the world record.

Crouch

It was great to be part of a historic race, but I never wanted to finish fifth.

Bayi

In New Zealand, things were quiet but every citizen in Tanzania went crazy to celebrate my achievement.

Dixon

At the time we realised I needed to be looking at the 5000m because these young guys were showing much more ability over the 1500m than I had.

Walker

I didn't appreciate what we had done at time. It was only afterwards once I started reading the press. We had just run one of the greatest foot races in history at a Commonwealth Games in little, old New Zealand. It was pretty phenomenal. Those Commonwealth Games were special. We will never see another one like it. In those days they were one of the biggest events. We didn't have world champs, you weren't paid.

Dixon

The Commonwealths in those days were huge. It was a world attention grabber. The world stopped. When we went to Europe in '74, people were talking about it everywhere. John loved it and went on to do incredible things. I feel privileged to have been a part of that race.

Bayi

The 1500m race in Christchurch didn't change my life financially compared to these days when an athlete breaks the world record - they always make a fortune. In those days, athletics was fully amateur and receiving money as an award was illegal.

Walker

Before the race, no one knew who I was. After that, everyone knew. It took one race to get noticed. The invitations came from all over Europe. I didn't have to beg, borrow and steal and rely on other athletes to get me into races. I had to turn them down in the end.

Foster

I knew that day when I saw John he was going to be the greatest and he went on to become world record holder and Olympic champion.

  • Filbert Bayi (TAN) - 3:32.16 (WR)
  • John Walker (NZL) - 3.32.52 (NR)
  • Ben Jipcho (KEN) - 3.33.16 (NR)
  • Rod Dixon (NZL) - 3.33.89
  • Graham Crouch (AUS) - 3.34.42 (NR)
  • Mike Boit (KEN) - 3.36.84
  • Brendan Foster (ENG) - 3.37.64 (NR)
  • Suleiman Nyambui (TAN) - 3.39.62
  •  Source : The New Zealand Herald

WAZIRI MKUU MAJALIWA AONGOZA MBIO ZA HAPA KAZI TU DODOMA HALF MARATHON

February 01, 2016


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongoza mbio za Wabunge za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon zilizoanzia Bungeni hadi uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Januari 30, 2016, Kushoto ni Mhe. Nape Nnauye na kulia ni Naibu Spika Dk. Tulia na Dokii msanii wa Bongo Movie.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongoza mbio za Wabunge za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon zilizoanzia Bungeni hadi uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Januari 30, 2016. Kushoyo kwake ni Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye na kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Dkt Tulia Ackson. Mwansasu (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya Washiriki wa mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon wakishiriki mbio hizo mjini Dodoma Januari 30, 2016.
Mmoja wa wapigapicha walioshiriki mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon alilazimika kuomba msaada kwa askari wa usalama barabarani Mjini Dodoma Januari 30, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi ufunguo wa pikipiki mshindi wa kwanza wa mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon upande wa wanaume, Emmanuel Giniki kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Januari 30, 2016.
Mbunge wa Mbulu Vijijini akionyesha umahiri wake wa kuruka sarakasi , Mhe. Frate
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi zawadi ya Pikipiki mshindi wa kwanza upande wa wanawake wa Mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon, Angela Davile (kulia) kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Januari 30, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Dodoma ambao wamedhamini pambano la mpira wa miguu kati ya wabunge na benki hiyo kwenye uwanja wa Jamhuri Januari 30,2016. Benki hiyo pia ilitoa vifaa vya michezo kwa timu ya Bunge. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemtaka Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuandaa kikao cha haraka na viongozi wa vyama vya michezo nchini ili wamueleze kila mmoja amejipanga vipi kuinua viwango vya michezo katika chama chake.

Ametoa agizo hilo leo mchana (Jumamosi, Januari 30, 2016) wakati akizungumza na mamia ya viongozi na wakazi mbalimbali wa mkoa wa Dodoma ambao walishiriki mashindano ya mbio za nusu marathon (km. 21 na km. 5) zilizofanyika leo mjini Dodoma.

Mashindano hayo yalijulikana kama “HAPA KAZI TU HALF MARATHON” yamefanyika ikiwa ni sehemu ya kuhimiza uchapakazi miongoni mwa Watanzania lakini pia ni sehemu ya maandalizi ya kuelekea kuadhimisha siku 100 za utendaji kazi tangu Rais John Pombe Magufuli alipoapishwa na kuanza kazi.

“Kuna maboresho yanaendelea ndani ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo lakini haya yote hayawezi kufanikiwa kama viongozi wa michezo hawajajipanga vizuri. Ninatakata niandaliwe kikao cha siku moja na viongozi wa vyama vya michezo nchini ili waje wanieleze kila mmoja amejipanga vipi kuinua hali ya mchezo wake,” alisema huku akishangiliwa.

Alitumia fursa hiyo kuupongeza uongozi wa Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuandaa mbio hizo muhimu za kuhimiza Watanzania kuchapa kazi, lakini pia ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kushiriki katika mashindano ya Olimpiki yatakayofanyika baadaye mwaka huu huko Rio de Janeiro, Brazil.

“Tunataka tuondokane na kauli ya Tanzania kuwa ni kichwa cha mwendawazimu na nipende kusisitiza kuwa maandalizi haya yasiwe ya mwisho bali yawe ya muda mrefu kwa sababu tunaenda kushiriki mashindano ya dunia. Nasema tena, tuache utamaduni wa maandalizi ya kukurupuka,” alisisitiza.

Aliwataka wadau mbalimbali wajitokeze kusaidia taasisi za michezo.

Waziri Mkuu Majaliwa ambaye alishiriki mbio za km. 2.5 kuanzia saa 1 asubuhi, alikimbia kutoka eneo la Bunge hadi uwanja wa Jamhuri na kuzindua mashindano ya km. 21 saa 1:47 asubuhi na yale ya km. tano aliyazindua saa 1:51 asubuhi.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alikabidhi pikipiki aina ya GSM kwa washindi wa kwanza wa nusu marathon, mabati 100 kwa washindi wa pili na mabati 40 kwa washindi wa tatu. Mshindi wa tatu hadi wa 10 kwa wanawake na wanaume walikabidhiwa fedha taslimu.

Washindi wa kwanza hadi wa tatu waliokabidhiwa zawadi na Waziri Mkuu upande wa wanawake ni  Anjelina Daniel (Pikipiki); Fadhila Salum (mabati 100) na Catherine Lange (mabati 40). Wote wanatoka mkoa wa Arusha.

Kwa wanaume walioshinda nafasi kama hizo ni Emmanuel Giniki (Katesh, Babati) aliyeshinda pikipiki; Gabriel Gerald wa Arusha (mabati 100) na Fabian Joseph wa Arusha (mabati 40).

Wakati huo huo, Benki ya CRDB Dodoma ilitoa zawadi za sh. 250,000/- kila mmoja kwa washiriki watatu ambao ni walemavu walioamua kushiriki mbio hizo mwanzo hadi mwisho. Waliokabidhiwa zawadi hizo na Waziri Mkuu ni Bw. Hassan Hussein Sharif, Bw, Christian Ally Amour na Bw. Shukuru Khalfani.

Benki hiyo ilikabidhi pia vifaa vya michezo kwa ajili ya timu ya wabunge kwa ajili ya pambano la soka linalotarajiwa kufanyika leo saa 10 jioni kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma baina ya timu ya Bunge na timu ya CRDB. 

RT LAANDAA MBIO FUPI KWA AJILI YA KUHITIMISHA SIKU 1OO ZA RAIS DKT MAGUFULI KUWA IKULU

January 25, 2016
SHIRIKISHO la Riadha Tanzania(RT) limeandaa mbio fupi kwa ajili ya kuhitimisha siku 100 za rais Dk.John Pombe Magufuli kuwa Ikulu zitakazotimua vumbi jumamosi hii januari 30 mwaka huu mjini Dodoma.

Mbio hizo zimepewa jina maalumu la Dodoma ‘hapa kazi tu’ Half Marathon ambazo zitashirikisha washiriki mbali mbali wakiwamo waheshimiwa wabunge,mawaziri,wanafunzi,walemavu na wanariadha wakongwe nchini.Akizindua mbio hizo mjini Moshi mwishoni mwa wiki zinazodhaminiwa na Kampuni ya JSM,Rais wa shirikisho hilo,Anthony Mtaka alisema kuwa lengo la kuanzishwa kwa mbio hizo ambazo zimeandaliwa na kuendeshwa na shirikisho hilo ni kufufua michezo hapa nchini.

Pia alisema mbio hizo zitatumika kwa ajili ya kumpongeza Rais Dk.John Pombe Magufuli kutimiza siku 100 tangu aingie maradakani ambazo zitakuwa februari 14 mwaka huu.Kwa mujibu wa rais huyo wa RT,mbio hizo zimegawanywa katika makundi matatu ambako mbio za kwanza ni za kilomita 2.5 ambazo zitashirikisha wabunge,mawaziri,walemavu,wanafunzi ,wazee na watu mbalimbali.

Mbio za kilomita 5 ambazo ni za kujifurahisha zitashirikisha wakimbiaji wote na mbio za nusu marathon ambazo zitakuwa ni mbio za ushindani washindi watapata zawadi .Akitangaza zawadi kwa washindi,Mtaka alisema mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaumme na wanawake atapata zawadi ya piki piki yenye thamani ya sh,Milioni 2.8,mshindi wa pili akipata bati 100,wa tatu bati 40,mshindi wa nne akipata sh,200,000 huku mshindi wa tano akiondoka nash,100,000.

Mshindi wa sita hadi wa kumi watapata kifuta jasho cha sh,50,000 kila mmoja huku waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa ndiye atayakuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mbio hizo na atashiriki  mbio za kilomita 2.5.Wanafunzi waatakaopenda kushiriki mbio hizo watasajiliwa kwa sh,500,huku vwasio wanafunzi wakisajiliwa kwa sh,1,000 na wingine ambao hawakutajwa ni kundi gani wakisajiliwa kwa sh,5,000 na fedha hizo kwa mujibu wa Mtaka zitasaidia kambi ya wanariadha watakaoshiriki michuano ya Olimpiki.

Uzinduzi huo pia ulitumika kuwatambulisha wanariadha wawili ambao wamekidhi vigezo vya kushiriki michuano ya Olimpiki itakayofanyika nchini Brazil mapema mwezi Agosti mwaka huu ambako nchi zaidi ya 216 kutoka kila kona ya dunia zitashiriki

Wanariadha hao ni Alphonce Felix ambaye ana wastani wa muda wa kukimbia wa saa 2:12.01 na Said Makula ambaye muda wake wa kukimbia ni saa 2:13.27 na watatumia mbio hizo mjini Dodoma kama majaribio yao ya kitaifa kati ya majaribio sita ya kitaifa kabla ya kwenda Brazil.

Julai 6 mwaka jana,Felix alishiriki mbio za Gold Coast Marathon nchini Australia na kumaliza nafasi ya sita huku Makula akishiriki mbio za Casablanca Marathon oktoba 25 mwaka jana na kumaliza katika nafasi ya nne.
 
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania ,Anthony Mtaka akiwa na Mwe3nye3kiti wa Chama cha riadha mkoa wa Kilimanjaro,( KAA) Liston Methacha wakati wa uzinduzi rasmi wa mbio za Dodoma Hapa Kazi tu Half Marathoni 2016 zinzotarajia kufanyika January 30 mwaka huu mjini Dodoma.  
Baadhi ya wadau wa Riadha wakifuatiia mkutano wa uzinduzi wa Mbio za Dodoma Hapa kazi tu Half Marathon 2016 uliofanyika katika Hotel ya Nyumbani mjini Moshi.  
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka akizungumza na wanahabari (hawako pichani ) wakati wa uzinduzi rasmi wa Mbio hizo. 
 


Kocha wa timu ya taifa ya Riadha ,Francis John akiwa na wanariadha ,Alphonce Felix na Said Makula waliofuzu viwango vya kushiriki mashindano ya Olyipiki ,walipotamburishwa mbele ya wanahabari .  
Raisi wa RT ,Mtaka kifanya mahojiano na Mwandishi wa habari ,Enos Masanja wa Azam TV.Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

HAPA KAZI TU HALF MARATHON KUFANYIKA DODOMA, WAZIRI MKUU MHE. MAJALIWA KASSIM KUWA MGENI RASMI

January 16, 2016

 
KARIBUNI NYOTE 

PONGEZI/SHUKRANI ZA TOC KWA RAIS MSTAAFU MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE KWA KUENDELEZA MICHEZO KATIKA MIAKA 10 YA UONGOZI WAKE

December 31, 2015
TOC

Napenda kuchukua nafasi hii kuushukuru uongozi wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kwa kuandaa hafla ya kutoa tuzo kwa wanamichezo 10 bora waliofanya vizuri kwa kuiletea heshima  nchi yetu katika miaka 10 ya uongozi wa mwanamichezo mwenzetu Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pamoja na kutoa tuzo kwa Wanamichezo bora waliofanya vizuri miaka 10 iliyopita,  vile vile TASWA ilimtunuku tuzo Mhe Jakaya Mrisho Kikwete kwa mchango wako katika michezo.

Mhe. Rais, wakati anazungumza na wanamichezo waliokusanyika katika ukumbi wa Mlimani hapo tarehe 12/10/2015 alisononeka kwa wanamichezo wa Tanzania kutofanya vizuri wakati wa miaka 10 ya uongozi wake pamoja na kuleta walimu katika baadhi ya vyama vya michezo.

Mafanikio hata katika maisha ya kawaida ni mapambano hali kadhalika hata kupata mafanikio katika michezo ni mapambano. Katika miaka ya 70-80 michezo ilikuwa ridhaa, lakini kuanzia miaka ya 90 hadi sasa michezo imekuwa biashara na ajira kubwa kwa wanamichezo.
Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa akimpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kuendeleza michezo katika kipindi chake chote cha uongozi wake wa miaka 10.
Kwa mfumo huo wa michezo kuwa biashara na ajira kila moja angefikiria kwamba tungepaswa kuwa na wanamichezo wengi  kwa hiari yao kuchangamkia mazoezi ya hali ya juu ili nao waweze kuwa wawakilishi wazuri wa nchi yetu na kujipatia zawadi nono za fedha, lakini badala yake hali inazidi kuwa mbaya.

Hali hii inawezekana vile vile imesababishwa na hali ya ukata wa vyama vya michezo ambao hawana uwezo wa kutafuta vipaji huko walipo hasa Vijijini, Wilayani na Mikoani.

Katika miaka ya 70-80,  Vyama vyetu vilikuwa vinapata ruzuku kutoka Serikalini kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT), ruzuku ambayo ilikuwa inawasaidia kuendesha ofisi na kuandaa Mashindano  kama ya Taifa ambayo wanamichezo wengi wanakusanyika na vyama husika kufanya uteuzi wa wachezaji bora wenye vipaji ambao huwaendeleza.
Huo mfumo kwa sasa haupo kutokana na hali inayotamkwa na vyama vya michezo kama ukata na Serikali (BMT) kutokuwa na fedha.

Katika risala yake wakati wa tuzo kwa wanamichezo bora, Mhe. Rais alikiri bila kuwekeza tusitegemee kupata mafanikio, lakini nani awekeze, kwa haraka kwa tulio na uelewa mdogo ni Serikali ndiyo iwekeze kama nchi zingine duniani inavyofanya.

Mhe. Rais amefanya mengi kuinua michezo wakati wa uongozi wake. Naomba nitaje chache:
1.     WALIMU WA MICHEZO KUTOKA NJE.
Aliweza kuwalipa mishahara walimu wa michezo kama mpira wa miguu, netiboli, ngumi na riadha (pamoja na walimu wa riadha kutokuwa wa viwango) kupitia mpango wa ushirikiano kati ya Tanzania na Cuba. Kila mmoja wetu aliona jitihada zake,  na nakiri kwamba kwa namna moja au nyingine, vyama/mashirikisho ya michezo hawakutekeleza wajibu wao kutokana na hali ya ukata.

Hata wanamichezo wetu hawakutambua na kuona michezo kama ajira.
Mhe. Rais anakiri mafanikio yana gharama, bila nchi kuwekeza hafikirii kama tutakuwa na mwelekeo mwema hasa kwa vijana wetu kufanya vizuri katika medani ya Kimataifa. Nchi nyingi zinazofanya vizuri katika michezo ya kimataifa  kwa asilimia kubwa wamewekeza katika michezo. Pamoja na WHVUM kutengewa bajeti ndogo ya michezo, bado suala la kuwekeza haliwezi kukwepeka kwa hali ya sasa ya michezo duniani.

2.    MICHEZO YA UMITASHUMTA/UMISSETA.
Tutakukumbuka hasa pale Mhe Jakaya aliporejesha michezo ya Umitashumta na Umisseta  mwaka 2007 baada ya kusimama kwa zaidi ya miaka 9.
 
Binafsi naamini kilichotufikisha hapa tulipo leo ni pamoja na kutofundishwa kwa elimu ya viungo (PE) sambamba na kutokuwepo walimu wa masomo hayo kwenye shule zetu na kusimama kwa michezo hiyo  na  Michezo ya Majeshi (BAMATA).

Michezo ya Umitashumta/Umisseta ndiyo ilikuwa kiwanda cha kuandaa wachezaji ambapo wanapofanya vizuri hupata ajira katika taasisi za Serikali (JWTZ, Polisi, Magereza, Jeshi la Kujenga Taifa) lakini kwa sasa imekuwa tofauti kwani taasisi hizo haziajiri kama ilivyo huko nyuma kutokana na kutofanyika Michezo ya Majeshi (BAMATA) ambayo ilikuwa na ushindani mkubwa.

Ni zaidi ya miaka 8 tangu aliporejesha michezo ya Umitashumta/Umisseta kwa nia na madhumuni ya kupata vipaji vitakavyoendelezwa na kuwa na nafasi nzuri ya kutuwakilisha Kimataifa.

Imekuwa vigumu kuendeleza  vipaji vinavyoonekana katika michezo hiyo kwani hakuna maandalizi yaliyofanywa kuwaendeleza  baada ya michezo hiyo kumalizika. Hata wale wanaomaliza masomo yao katika ngazi husika hawapati ajira kutokana na taasisi za Serikali nilizotaja kutokuwa na ajira rasmi kama ilivyo zamani. Mpaka sasa ni shule chache za binafsi  na taasisi zimekuwa na  mpango wa kuwasajili katika shule zao wanafunzi wazuri wenye vipaji na baadhi yao kutoa elimu bure (Scholarships) na kuwaendeleza katika baadhi ya michezo:

a.Shule ya Sekondari ya Alliance, Mwanza (Mpira wa Miguu na Riadha).

b.Shule za Filbert Bayi, Mkuza, Kibaha Mkoa wa Pwani (Riadha na Netiboli)


c.Shule ya Sekondari ya Lord Baden Powel, Bagamoyo (Mpira wa Miguu kwa Wanaume na  Wanawake,  Mpira wa Kikapu, Mpira wa Wavu na Riadha).

d.Shule ya Sekondari ya Winning Spirit, Arusha (Riadha)

e.Shule ya Sekondari ya Makongo, Dar Es Salaam (Mpira wa Miguu, Netiboli Kikapu na Wavu).

Naomba niishauri Serikali (Wizara ya Elimu na Tamisemi) kuunda Kanda ili kila baada ya michezo ya Umitashumta na Umisseta wanamichezo wenye vipaji wawekwe katika shule zilizo katika Kanda zitakazoundwa wakiendelea na masomo hali kadhalika na kucheza kwa Wizara husika kupeleka wataalamu (coaches) katika Kanda husika. Kama hilo haliwezekani, basi shule binafsi na taasisi zisaidiwe ili ziweze kuimarisha zaidi mipango waliyonayo ya kuendeleza michezo

Bila kuwa na utaratibu na mipango mahsusi, michezo ya Umitashumta na Umisseta,  itakuwa kama tamasha tu.

3.     UWANJA WA TAIFA
Hakuna ubishi kwa ushiriki wake katika ujenzi wa uwanja wa Taifa wakati wa uongozi wa Rais wa awamu ya tatu Mhe. Benjamin William Mkapa akiwa kama Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mpaka alipochaguliwa kuwa Rais wa awamu ya nne na kumalizia kazi za ujenzi zilizobaki.

Uwanja wetu ni mzuri sana, lakini matumizi yake kwa mchezo wa riadha yamekuwa nadra sana kutokana na gharama kubwa ambayo wakati mwingine  Riadha Tanzania inashindwa kuchangia hasa inapotaka kufanya michezo ya Taifa ambayo hufanyika mara moja kwa mwaka.

4.     MAFANIKIO YA MICHEZO WAKATI WA UONGOZI WAKO.
Mhe. Jakaya wakati wa uongozi wake wa miaka 10 kulikuwa na mafanikio ambayo hayaridhishi kwa nchi kama Tanzania yenye watu zaidi ya Milion 45, lakini kutokana na hali halisi niliyotaja hapo juu naomba nitaje mafanikio hayo kama ifuatavyo:

Samson Ramadhani
1.Samson Ramadhani NYONYI, (Riadha):”Marathon”>Dhahabu: Michezo ya Jumuiya ya Madola, Melbourne, Australia 2006.

2.Fabian Joseph NAASI, (Riadha): Mita 10000>Shaba: Michezo ya Jumuiya ya Modola, Melbourne, Australia 2006.
Fabian Joseph.
3.Martin SULLE, (Riadha) Km 21.1>Medali ya Fedha>Michezo ya Afrika, Algiers, Algeria, 2007.

4.Timu ya Netiboli, (Netiboli)>Medali ya Fedha>Michezo ya Afrika, Maputo, Msumbiji, 2011.

5.Timu ya Netiboli (Netiboli)>Kushinda Kombe la Mataifa 6, Singapore, 2012.

6.Timu ya Netiboli (Netiboli>Nafasi ya Pili, Mashindano ya Africa, Dar Es Salaam, 2012.

7.Timu ya Mpira wa Miguu watoto wa Mitaani (Street Children World Cup)>Dhahabu, Mashindano Kombe la Dunia, Rio de Jeneiro, Brazil, 2014.

8.Timu ya Mpira wa Miguu-Vijana chini ya Miaka 15>Medali ya Fedha> Michezo ya Vijana Afrika, Gaborone, Botswana, 2014.

5.     SHUGHULI ZA TOC.
Wakati wa uongozi wake wa miaka 10 kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kamati ya Olimpiki Tanzania imeweza kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo kwa vyama vya michezo, baadhi ya hizo shughuli zilikuwa ni kuendesha mafunzo ya ufundi kwa walimu wa michezo kutoka Vyama/Mashirikisho ya michezo wanachama wa TOC kwa kuleta Wakufunzi kutoka nje ya nchi hali kadhalika na Mafunzo ya Utawala na Uongozi wa Michezo kwa viongozi wa Vyama/Mashirikisho ya Mikoa na Taifa kwa nyakati tofauti.
Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania, Filbert Bayi (kushoto) akizungumza kabla ya kuwakabidhi hati wachezaji watatu wa Tanzania waliodhaminiwa na Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki kupiga kambi Eldoret nchini Kenya. kutoka kulia ni Fabian Joseph, Fabian Nelson na Bazil John.
Kwa ujumla Walimu 523 (448/75) na viongozi 380 (304/76) waliweza kupata elimu ya kufundisha wachezaji kwa madaraja tofauti na uongozi na utawala bora.
(Orodha Nyongeza “A” na “B”imeambatanishwa).

HITIMISHO
Kwa niaba ya Kamati ya Olimpiki Tanzania na kwa niaba yangu napenda nichukue nafasi hii kumshukuru Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa kutoa posho za kujikimu, mavazi ya taifa, vifaa vya mazoezi na mashindano timu zetu za Taifa zilizowahi kushiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola (Melbourne, Australia 2006, New Delhi, India 2010 na Glasgow, Scotland 2014) na Olimpiki (Beijing, China 2008, London, Uingereza 2012).
Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi akisaini moja ya hati za kuwadhamini wanariadha watatu wa Tanzania kupiga kambi Eldoret, Kenya huku Katibu Mkuu wa Riadha Tanzania, Suleuman Nyambui akishuhudia. Kushoto ni Rais wa TOC, Gulam Rashid.
Nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sitamshukuru Mhe. Bernard Camillius Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa ushirikiano na WHVUM kuwatafutia mazoezi ya nje (China, Ethiopia, Uturuki na New Zealand) kwa kutumia mpango wa Diplomasia ya Michezo (Sports Diplomacy) wanamichezo wetu kabla ya Michezo ya Jumuiya ya Madola, yaliyofanyika Glasgow, Scotland mwaka jana (2014).

Akiwa kama mwanamichezo nambari moja hata baada ya kustaafu bado wanamichezo wenzako tutahitaji ushauri wake katika maendeleo ya michezo katika
nchi yetu.

Mwisho kabisa natoa wito kwa wanamichezo wote kujitokeza na kutumia haki yao ya Kikatiba hapo Jumapili tarehe 25/10/2015 kupiga kura kuchagua mafiga matatu (Diwani, Mbunge na Rais) kwa kipindi cha miaka 5 (2015-2020) ijayo.

Nawatakia Wanamichezo wote kila la kheri katika mchakato mzima na tulinde  amani tuliyonayo.

Filbert Bayi,


KATIBU MKUU.
 

Copyright © 2015 - 2025 Athletics Tanzania All Right Reserved

Developed by Gadiola Emanuel
Theme By AP | Developed By Gadiola Emanuel