Kutoka Kulia: Ofisa wa BMT Charles Maguzu, Makamu wa Rais William Kallaghe na Mjumbe wa Kanda ya Kaskazini Alfredo Shahanga.
Kutoka Kulia: Ofisa wa BMT Charles Maguzu, Makamu wa Rais William Kallaghe na Mjumbe wa Kanda ya Kaskazini Alfredo Shahanga.
![]() |
Wanariadha wakichuana kwenye mashindano ya Majaribio Jijini Dar es Salaam. |
Kulia ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania RT , Ndugu William Kallaghe akikabidhi ripoti kwa Katibu Mkuu Mtendaji wa BMT, Bi. Neema Msitha Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu RT, Wakili Jackson Ndaweka.
SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT), limeitaka mikoa yote nchini kuhakikisha inaendesha mashindani ya Vijana chini miaka 20 na 18 'U-20 U-18' kuanzia ngazi ya Wilaya.
Maelekezo hayo yametolewa na Kaimu Katibu Mkuu RT, Wakili Msomi Jackson Ndaweka, katika barua yake ya Januari 25 kwenda kwa viongozi wa vyama vya mikoa Tanzania Bara.
Amewaelekeza viongozi hao, kukumbuka kwamba kuna jukumu kubwa mbele yao, kwani mwaka huu una mashindano mengi ya vijana wa umri huo.
Wakili Ndaweka, aliyataja mashindano hayo kuwa ni Afrika Mashariki U-18 na 20, Tanzania ikiwa mwenyeji, ambapo awali yalikuwa yamepangwa kufanyika Kigali, Rwanda.
Alisema, mashindano hayo yatafuatiwa na ya Afrika kwa umri huo Lusaka, Zambia Aprili 27 hadi Mei 3, 2023.
"Ili kuhakikisha nchi inashiriki kwa mafanikio mashindano hayo, lazima mashindano yaanzie ngazi ya Wilaya, kisha Mkoa na mwisho mashindano ya Taifa ya Wazi kwa vijana wa umri huo ambayo yanatarajiwa kufanyika Februari 25," alisema na kuongeza.
Mashindano ya Wilaya yafanyike kati ya Februari 9-11 na Mikoa Februari 13-19.
"Utaratibu huu, unakusudia kuhakikisha wanapatikana wachezaji wenye uwezo mkubwa, ili kuleta tija katika ushiriki wa nchi kwenye mashindano ya kimataifa," alisema Wakili Ndaweka.
Sambamba na hilo, RT inakusudia na imejipanga kuhakikisha kuwa kalenda yake inafuatwa na matukio yote yanafanyika kama yalivyopangwa.
Sudan Kusini yaipa shavu RT, Simbu Balozi mpya JICA
NA TULLO CHAMBO, RT
MASHINDANO Maalum ya Riadha ya Wanawake nchini Tanzania maarufu kama Ladies First, yamezidi kufungua ushirikiano wa mchezo huo kimataifa.
Ladies First ikiwa ni wazo la Nguli wa Riadha nchini Tanzania, Kanali mstaafu Juma Ikangaa, imefanyika mwaka huu ukiwa ni msimu wa nne na kushirikisha mikoa 30 Kati ya 31 Tanzania Bara na Visiwani.
Mwaka huu, mashindano hayo yalifanyika January 21 na 22 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam na kushirikisha zaidi ya wanariadha 186.
Kanali Mstaafu Ikangaa, ambaye enzi zake aliiwakilisha vema Tanzania kimataifa katika mbio za marathoni, ikiwemo nchini Japan, nchi hiyo imekuwa ikimuenzi na kumpa heshima kubwa ambapo hivi sasa ni Balozi wa Hiari wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA).
Katika kumuenzi Kanali Ikangaa, Japan ilimtaka kusema kitu ambacho nchi hiyo iifanyie Tanzania, ndipo kwa kushirikiana na wadau wake mbalimbali, akaja na wazo la kuwaenzi na kuhamasisha wanawake kushiriki katika mchezo wa Riadha, hasa ikizingatiwa medali ya kwanza ya kimataifa Tanzania ililetwa na Mwanamke Theresia Dismas mwaka 1964, katika michezo ya All Africa nchini Congo Brazzaville, kupitia mchezo wa Kurusha Mkuki 'Javelin'.
Wazo hilo lilianza kutekelezeka mwaka 2017 kwa mashindano yaliyofanyika Uwanja wa Taifa, sasa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, ambapo baadhi ya washindi wamekuwa wakipata nafasi ya kwenda kushiriki mbio za Nagai City nchini Japan.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa Tanzania (BMT), Bi. Neema Msitha, aliipongeza JICA na kampuni mbalimbali za Kijapan zinazofanya kazi nchini, Kanali Ikangaa,serikali ya Tanzania na Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), kwa kufanikisha mashindano hayo kwa msimu wa nne sasa.
Bi. Msitha, anasema mashindano hayo yalianza mwaka 2017 na kufanyika kwa mafanikio makubwa miaka mitatu mfululizo hadi 2019 kabla kusitishwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo janga la UVIKO 19 'Covid 19'.
"Lengo la mashindano haya ni kuhamasisha ushiriki wa watoto wa kike katika michezo hususan Riadha, kutoa fursa kwa wanariadha wa kike kuonyesha vipaji vyao na kuendeleza vipaji vya wanariadha ambao wataiwakilisha nchi katika mashindano ya kitaifa na kimataifa," anasema Bi. Msitha.
Tangu kuanza kwa mashindano hayo mwaka 2017, Wanariadha wa Tanzania na viongozi wao, wamekuwa wakipata nafasi ya kwenda kushiriki Nagai Marathon, ambapo wanariadha akiwemo Angel John Joseph Yumba, Fabian Nelson Sulle, Fabian Joseph, Alphonce Felix Simbu na wengineo wameweza kung'ara.
Mbali na hilo, Ladies First iliweza kuishirikisha nchi ya Sudan Kusini na kushiriki mashindano ya mwaka 2019 jijini Dar es Salaam.
Mwaka huu 2023, Ladies First imezidi kufungua milango katika mchezo wa Riadha Tanzania, ambapo Sudan Kusini iliwakilishwa na viongozi wake mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya Michezo nchini humo, Peter Baptist, Balozi wa nchi hiyo nchini Tanzania, Deng Abel na wengineo.
Baptist katika salamu zake, mbali na kushukuru na kupongeza Tanzania kwa mashindano hayo, anasema na kwao wana mashindano kama hayo yajulikanayo kama 'Umoja na Amani', yakilenga kutumia michezo kuhamasisha amani na umoja katika Taifa hilo ambalo liliandamwa na vita miongoni mwao kwa miaka kadhaa.
Mwakilishi huyo, anasema katika kuendeleza ushirikiano na Tanzania, wanatoa mwaliko kwa wanariadha wanne waliofanya vizuri katika Ladies First 2023 wa mbio tofauti ukiondoa mita 5000 kwenda Sudan Kusini kushiriki mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika miezi miwili ijayo.
Mbali na fursa hizo zilizojitokeza Ladies First 2023, nyingine ni kwa Mwanariadha anayefanya vema hivi sasa, Mshindi wa Medali ya Fedha Common Wealth Games 2022, Alphonce Simbu, naye kuteuliwa kuwa Balozi wa Hiari JICA, akiungana na Kanali mstaafu Ikangaa.
Haya ni kati ya mafanikio ya Ladies First 2023, na hakika uwajibikaji ukizidi kuongezeka, bila shaka milango zaidi itazidi kufunguka katika medani ya riadha Tanzania.
NA TULLO CHAMBO - AT
NA TULLO CHAMBO
WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dr. Dorothy Gwajima, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Mashindano Maalum ya Riadha ya Wanawake maarufu kama 'Ladies First' yanayotarajiwa kurindima kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa January 21 na 22 jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha, alisema mashindano hayo yamendaliwa na BMT, Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), na kuwezeshwa na Shirika la Maendeleo la Japan ( JICA), na huu ni msimu wake wa nne, yakiwa na lengo la kuwahamasisha wanawake kushiriki katika mchezo wa Riadha.
"Lengo la mashindano haya ni kuwahasisha watoto wa kike kushiriki katika michezo hususan Riadha, kutoa fursa ya wanariadha wa like kuonyesha vipaji vyao na kuendeleza vipaji vya wanariadha ambao watawakilisha nchi katika mashindano ya kitaifa na kimataifa siku zijazo," alisema Msitha.
Alisema mashindano ya mwaka huu, yatashirikisha wanariadha 186 kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani yakishirikisha mbio za Mira 100, 200, 400, 800, 1500, 5000, 10000, Kupokezana Vijiti 4x400 na Kurusha Mkuki na kushuhudiwa na watazamaji mbalimbali wakiwemo wanafunzi 1000 kutoka shule za Msingi na Sekondari za Manispaa ya Temeke.
"BMT inaishukuru Sana JICA na kampuni za Kijapan zinazofanya shughuli zake hapa nchini kwa kufadhili mashindano haya kwa mara ya nne, pia Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kutoa uwanja ambao utatumika kwa mshindano na ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke ambayo imetoa ruhusa kwa wanafunzi kushiriki na kujifunza katika mashindano haya," alisema Msitha na kuongeza.
Baraza linaendelea kusisitiza Kamati za Michezo za Mikoa, kuhakikisha zunawezesha ushiriki wa wanaridha wa mikoa yao katika mashindano haya na kuwaomba wananchi wote wa Jiji la Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi siku ya Jumamosi na Jumapili kushuhudia mashindano hayo ambapo hakuna kiingilio.
Kwa upande wake, Mwakilishi Mkuu wa JICA Tanzania, Naofumi Yamura, alisema wanajivunia kuanza kutoa ushirikiano kwa Tanzania toka mwaka 1962 na mashindano ya mwaka huu watayatumia kama maadhimisho ya miaka 60 ya ushirikiano wao na Tanzania.
Yamura, alisema mashindano ya mwaka huu yatahudhuriwa na watu mbalimbali maarufu akiwemo Balozi wa Japan Tanzania, viongozi kutoka Sudan ya Kusini, Mwanariadha nguli Kanali mstaafu Juma Ikangaa na mwanariadha anayewika hivi sasa Alphonce Simbu.
Naye Katibu wa Chama cha Riadha Zanzibar (ZAAA), Muhidin Masunzu akimwakilisha Kaimu Katibu Mkuu wa RT, Wakili Jackson Ndaweka, alisema wamejiandaa vema kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika kwa ufanisi.
Wazo la kuanzishwa mashindano hayo liliasisiwa na Kanali Ikangaa, ambaye pia no Balozi wa Hiari wa JICA, likitokana na kuenzi historia ambapo medali ya kwanza Tanzania kimataifa ililetwa na Mwanamama Thereza Dismas, aliyekuwa akirusha Mkuki.
Hurdling, sport in athletics (track and field) in which a runner races over a series of obstacles called hurdles, which are set a fixed distance apart.
Traditionally, there are two types of hurdle races—the 120-yard (110 meter) high hurdle and the 440-yard (403 meter) intermediate hurdle. The hurdles are 42 inches (1.06 meters) high in the 120-yard event and 36 inches (. 91 meters) high in the 440-yard event.
Athletics 400 metres | |
---|---|
The closing stages of a men's 400 m race | |
World records | |
Men | Wayde van Niekerk 43.03 (2016) |
Women | Marita Koch 47.60 (1985) |
The Local Organizing Committee (LOC) for the World Athletics Championships (WCH) Oregon22 has announced the global event’s marathons and race walks will be held in Eugene and Springfield, Oregon. These locations are within miles of the event’s main venue, Hayward Field at the University of Oregon.
The perimeter of Autzen Stadium, also located on the University of Oregon campus, will serve as a hub for the start and finish of all WCH Oregon22 Road Events, including the men’s and women’s marathon and men’s and women’s race walk events.
The LOC has been working with the Eugene Marathon team to develop courses for the road events that allow athletes, spectators, and digital fans to share in the glory of Oregon and the history of track & field in this community.
“We’re thrilled to have the chance to manage the WCH Oregon22 road events next summer,” Eugene Marathon Race Director and Oregon22 Road Events Course Manager Ian Dobson said. "We run on these roads every day and the thought of showing off our extraordinary community to the world, while also inspiring our own running community by bringing the world’s best athletes to them, is an opportunity unlike any other."
On the first day of competition, July 15, 2022, the women’s and men’s 20-kilometers race walk will take place. The only morning session of Day 8 is the women’s 35-kilometers race walk, the first of its kind in the World Championship series. Day 10, the final day of WCH Oregon22 is opened with the men’s 35-kilometers race walk. All race walk events will be conducted on a 1-kilometer looped course near Autzen Stadium.
The men’s marathon is set to open Day 3 of competition. The women’s marathon will be held the following morning on Day 4 of competition. Both the men’s and women’s marathon course will be a 14-kilometer looped course circling through Eugene and Springfield, Oregon. It will highlight the natural beauty and history of the heart and home of track and field in the U.S.
Copyright © 2015 - 2025 Athletics Tanzania All Right Reserved
Developed by Gadiola Emanuel