Matukio

< span data-type="recent" data-yes="5">

Hatimaye Shirikisho la Riadha Nchini (RT) Yajadili na Kupitia Katiba Mpya




Profesa Elisante Ole Gabriel

Chama Cha Riadha Tanzania (RT) kilifanikiwa kujadili na kupitisha katiba yake mjini Morogoro. 


Mkutano huo mkuu uliohudhuriwa na wajumbe wa mikoa 18 na kamati ya utendaji wa chama hicho ulifunguliwa na mgeni rasmi ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel.


Pamoja na vifungu vyote vilivyokuwa katika ‘Draft Proposal’ kupita lakini muhimu zaidi ni kipengele kilchoweka ushiriki maalum wa Zanzibar katika chama hicho.


Mkutano ulifanyika na kumalizika salama chini ya uenyekiti wa rais wa shirikisho hilo Anthon Mtaka (DC Hai) na Katibu wake Suleman Nyambui huku maelezo ya kisheria yakifafanuliwa na mwanasheria wa RT Thabit Bashir.

Post a Comment

0 Comments