Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kawaida wa Mwaka wa TOC unaofanyika Kituo cha Amani, Welezo Zanzibar

December 31, 2015
TOC
Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi akisoma taarifa yake ya mwaka katika Mkutano Mkuu wa TOC Kituo cha Amani Welezo, Zanzibar. Kulia ni Rais wa TOC Gulam Rashid na Mhazini msaidizi Juma Zaidi (kushoto).
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) wakati wa mkutano huo jana Zanzibar.
 







Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Gulam Rashid wakati wa ufunguzi  wa Mkutano Mkuu wa kawaida wa mwaka wa TOC unaofanyika leo Zanzibar. Kushoto ni Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi na Mhazini Mkuu Charles Nyange.




Mhazini Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Charles Nyange (kushoto) akipokea tuzo kwa niaba ya mmoja ya makampuni yaliyodhamini Siku ya Olimpiki.

Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TOC katika picha ya pamoja mjini Zanzibar.
 

RISALA YA KATIBU MKUU (TOC) KWENYE UFUNGUZI WA KAMISHENI YA WANAMICHEZO ZANZIBAR TAREHE 10/12/2015.

December 31, 2015
TOC




Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kamisheni ya Wachezaji ya Kamati ya Olimpiki Tanzania (Kawata) leo Zanzibar. Kushoto ni mwenyekiti wa Kawata, Ramadhan Zimbwe. Kushoto kwa Bayi ni Katibu Msaidizi wa TOC Jamal Adi na rais wa Toc Gulam Rashid.

 TANZANIA OLYMPIC COMMITTEE (TOC)
KAMATI YA OLIMPIKI TANZANIA

RISALA YA KATIBU MKUU (TOC), FILBERT BAYI KWENYE UFUNGUZI WA KAMISHENI YA WANAMICHEZO ZANZIBAR TAREHE 10/12/2015.

Ndugu Mgeni Rasmi Jamal Adi, Katibu Mkuu Msaidizi TOC

Ndugu Gulam Rashid, Rais wa TOC,

Ndugu Ramadhani Zimbwe, Mwenyekiti, KAWATA Taifa,

Ndugu Amina Ahmed, Katibu KAWATA Taifa

Viongozi Kamati yaUtendaji Waalikwa

Kamati ya Utendaji, KAWATA Taifa,

Wanamichezo Washiriki

Mabibi na Mabwana.

Kwa niaba ya Kamati ya Olimpiki Tanzania na kwa niaba yangu mwenyewe sina budi kumshukuru Katibu Mkuu Msaidizi wa TOC, pamoja na kuwa moja wa viongozi wa juu wa TOC kukubali mwaliko wa ofisi ya TOC kwa kuja hapa leo  kutufungulia Mkutano huu Mkuu wa Kamisheni ya Wanamichezo.

Ndugu Mgeni Rasmi, ofisi ya TOC imekuwa hapo awali ikialika wageni rasmi hasa katika shughuli hizi za ufunguzi wa mikutano yetu kutoka nje hasa taasisi na serikali, lakini kuanzia sasa itakapobidi shughuli hizi zitafanywa na viongozi wa TOC au Vyama/Mashirikisho ya Michezo.

Ndugu Mgeni Rasmi, tangu Kamisheni ya Taifa ilipoundwa hapo mwaka 2006, kazi kubwa ilikuwa kuhamasisha na kutoa wito kwa Vyama/Mashirikisho ya Michezo kuanzisha Kamisheni ya wachezaji katika Vyama/Mashirikisho yao ya Michezo. Ni Vyama/Mashirikisho chache ambayo yameitikia wito wetu kwa kufanya uchaguzi halali wa kidemokrasia.
Vyama vingi mpaka sasa vimekuwa vikiteua wajumbe wake kuhudhuria Mikutano Mikuu ya Kamisheni inayoandaliwa na TOC, lakini cha kushangaza kwa utafiti ulioofanywa na TOC/KAWATA Taifa, wachezaji hao siyo wajumbe katika Kamati za Utendaji na Mikutano Mikuu ya Vyama na Mashirikisho husika kama Muongozo wa Kamisheni unavyosema.

Sijui ni kwa nini Vyama/Mashirikisho ya Michezo yaogope kuwaingiza wachezaji kwenye chombo cha maamuzi (Kamati ya Utendaji/Mkutano Mkuu). Kuna siri gani kubwa katika vikao vya Kamati ya Utendaji na Mkutano Mkuu ambayo hayapaswi wachezaji kufahamu? 

Mimi nina imani kabisa wawakilishi wa wachezaji watakapokuwa kwenye vyombo hivyo vya maamuzi malalamiko na manung’uniko mengi ya wachezaji hayatakwepo, kwani watakuwa wameshiriki kikamilifu katika maamuzi.

Mahali ambako Mkutano Mkuu wa Kamisheni ya Wachezaji (Kawata) unapofanyikia leo Zanzibar.
Ndugu Mgeni rasmi, Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa (IOC), Vyama/Mashirikisho ya Kimataifa (IFs), ANOCA na NOCs kama TOC  zina Kamisheni zao ya Wanamichezo ambazo kazi zao kubwa ni kama:

1.     Kutoa ushauri, nasaha kwa wanamichezo waliostaafu na ambao bado wanaendelea na michezo.
2.     Kulinda maslahi ya wanamichezo ndani ya maadili ya Olimpiki.
3.     Kutoa mapendekezo kwa mambo yanayohusu maslahi ya wanamichezo ndani ya vikao ya Kamisheni husika.
4.     Kufanya lolote lile ambalo ni kwa faida ya wanamichezo kwa ujumla wake.

Kamisheni yetu ya Kitaifa tangu ianzishwe mwaka 2006 na wajumbe wake Kitaifa kuchaguliwa tena mwaka 2012 mjini Dodoma  imechelewa kwa kiasi fulani kutokana na sababu ambazo ni pamoja na kukwamishwa na viongozi wa Vyama/Mashirikisho yao Kitaifa (NFs).

Baadhi ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa Kawaita mjini Zanzibar leo Alhamisi.
Wanamichezo wana uwezo mkubwa wa kushauri viongozi wa vyama/mashirikisho yao katika masuala yanayohusu maendeleo ya michezo, pia kushauri mashirika mbalimbali kuhusu ajira za wanamichezo pamoja na hali ya baadaye mchezaji mhusika anapostaafu.

Mhe. Mgeni Rasmi, michezo kwa sasa ni ajira, ndiyo maana IOC imehamasisha NOCs kuunda Kamisheni za Wanamichezo ili watambuliwe kuwa sekta muhimu ya maendeleo ya michezo katika Taifa letu.

TOC  inaamini kwamba kukiwa na uwakilishi wa wanamichezo katika vyama/mashirikisho ya michezo na asasi za umma nchi yetu itakuwa imepiga hatua katika kupiga vita madawa ya kuongeza nguvu katika michezo ambayo kwa sasa yamepamba moto duniani.
Baadhi ya waalikwa katika mkutano Mkuu wa Kamisheni ya Wachezaji Tanzania (Kawata) Kutoka kushoto Irine Mwasanga, Peter Mwita na Mwinga Mwanjala wakati wa mkutano huo leo Zanzibar.
Mhe. Mgeni Rasmi, bado vyama/mashirikisho ya michezo ya kutothibitisho yanaendelea. Mwaka huu kutoka Bara ni Vyama/Mashirikisho ya Kuogelea, Mpira wa Magongo na kwa Zanzibar Mpira wa Meza na Kikapu havikuthibitisha, lakini wakatma washiriki. Riadha Tanzania kuwasilishwa na wajumbe 3 (wm 2, mk 1).

Kwa haya machache naomba nikukaribishe ili uzungumze na wanamichezo walio mbele yako kisha utufungulie Mkutano huu wa Kamisheni ya wanamichezo kwa mwaka 2015 kama tulivyokuomba.


Ahsanteni kwa kunisikiliza.




Katibu Mkuu wa TOC Filbert Bayi akifuatilia jambo na mjumbe wa Kamati ya TOC Irine Mashanga wakati wa Mkutani Mkuu wa Kawata Zanzibar .
 



Katibu msaidizi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Jamal Adi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kamishenu ya Wachezai (Kawata) Zanzibar. Kulia kwa Adi ni Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi.

HOTUBA YA MGENI RASMI WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO MKUU WA KAMISHENI YA WACHEZAJI TANZANIA (KAWATA) ULIOFANYIKA ,ZANZIBAR

December 31, 2015
TOC


 
Ndugu Gulam A. Rashid, Rais wa Kamati ya Olimpiki ya Tanzania,

Ndugu Filbert Bayi  Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania,

Ndugu Viongozi wa Kamisheni ya Wachezaji Tanzania,

Wageni Waalikwa,

Mabibina Mabwana.

Awali ya yote, napenda kutoa shukrani zangu kwa viongozi wenzangu wa TOC
kwa kunishirikisha na kunipa heshimahiiyakuwamgenirasmiwakuufunguaMkutanohuumuhimuwaKamisheniyaWachezaji Tanzania.

Kwanza naipongezaofisiyetuyaKamatiyaOlimpiki Tanzania kwakutekelezamaagizoyaKamatiyaOlimpikiyaKimataifayakuzitakaKamatizaOlimpikizaKitaifakujumuishawachezajikwenyeKamatizakezaUtendaji, naMikutanoMikuuyakehalikadhalikanaVyama/MashirikishoyaMichezowanachamawa TOC ambaomichezoyaoipokwenyeratibayaMichezoyaOlimpiki(Summer/Winter).

Ni matumainiyanguwengiwawawakilishiwaliohapaniwajumbehalaliwaliochaguliwanawachezajiwenzaondaniyaVyama/Mashirikishoyamchezohusikakwanjiayademokrasianasiyokuteuliwanaviongoziwavyama/mashirikishoyamichezoyenu, vile vilekutokaamadarakanizaidiyamudawauongoziambaoukokwenyemwongozowenukamamlivyoelekezwanaKamatiyaOlimpikiyaKimataifa (IOC) kupitiaKamatiyaOlimpikiyaTanznaia (TOC).

NatoawitokwaviongoziwaKamisheniyaWachezajiwanaowakilishavyama/mashirikishoyamichezokusaidiananaviongoziwaVyama/Mashirikishohusikailikamahavipohai, basiwajitahidikuvifufuakwamaanayakufanyauchaguzikwamudamuafakakufuatakatibazao. Kuna michezominginehufakutokananakutokuweponamsukumokutokawadauwavyama /mashirikishoyamichezoambaoniwachezaji. ViongoziwaKamishenikatikavyama/mashirikishovinawajibuwakusaidiamaendeleoyamichezokatikataifaletukupitiavyamanamashirikishoyao. Kamishenizilizochaguliwanazilizopoziwezekutoachangamotoyaushauriwanamnayakuendeshamichezonchini, kwanihadiduzarejeazakazizaonipamojanakuamshaariyawachezajiwenginewakitaifanakimataifakatikakufikiamahalipazuri pa kupatawachezajiwatakaowakilishavilabu, vyamanamashirikishoyetukatikangazimbalimbalizamashindano.KAWATA kuanziangaziyaVyama/MashrikishoyaMichezohadiTaifahaziwezikukwepalawamawakatitimuzetuzinapofanyavibayakatikaMashindanoyaKimataifa.

Nimefahamishwakuwawachezajiwengipamojanakwambammekamilikahapakuhudhuriamkutanohuu, lakinindaniyavyama/mashirikishoyenuhampewinafasiyakuwamojawawajumbewaKamatizaUtendajizaVyama, MashirikishonaVilabuvyamichezonakuwananafasiyauwakilishiwenyekurakatikaMikutanoMikuu.Ndaniyanafasihizokunamaamuzimengineyanawahusuwachezajiambaondiyowadauwakubwawavyombovyetuvyamichezohapanchini, lakinimaamuzihayoyamekuwayakiamuliwanaviongoziwavyama/mashirikishoyamichezo,ndiyomaanaTOC naIOC wakalionahilinakuamuawawepowawakilishiwaWachezaji. Ni matumainiyangukamamojawaviongoziwa TOC,VyamanaMashirikishoyaMichezo Tanzania Bara na Zanzibar wametekelezamaagizoya IOC kwafaidayaMichezokatikanchiyetu. .
  
Viongozi wa Kamisheni ya Wachezaji Tanzania Kawata), Katib u Mkuu Amina Ahmed (kushoto) na mwenyekiti wake, Ramadhabi Zimbwe pamoa na Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) Filbert Bayi wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kawata leo Zanzibar.
Binafsi, ninaungakabisaumuhimuwaKamisheniyaWachezajikatika TOC, Vyama/MashirikishonaVilabuvyaMichezo, huuniuamuzimzuriwaKamatiyaOlimpiki Tanzania (TOC)naKamatiyaOlimpikiyaKimataifa (IOC), nanikatikakukamilishaazmayamaadiliyaOlimpikihasakuwapawachezajihakiyakutoamawazoyaokatikaKamatizaUtendajizaVyama/Mashirikishona TOC. 


PiaKamishenikupitiaVyama/MashirikishoyetuyaMichezoipingekwanguvuzoteutumiajiwamadawayakuongezanguvukatikamichezoambakokwasasaumeongezekakwakasi.Shirikisho la Riadha la Kimataifa (IAAF) imeshaanzakupambanananchiambazowanariadha wake wamekuwawakitumiamadawayakuongezanguvukatikariadha.

KamisheniivihamasisheVilabunaVyamavyaMichezokuwanaKamishenizaoilizisaidiemaendeleoyamichezohapanchini, msikubalidaimakutumwakatikamikutanokamahiikwakuteuliwabilakuchaguliwa.

KwahayamachachesasanikotayarikufunguarasmiMkutanowenunakuwatakiakila la kheri.


Ahsanteni kwa kunisikiliza.
 
Baadhi ya wajumbe wa Kamisheni ya Wachezaji Tanzania (Kawata) wakiwa katika mkutano mkuu wao leo Zanzibar.

Mkuu wa Wilaya ya Karatu ndiye mgeni rasmi tamasha la michezo la mwaka huu la Karatu

December 31, 2015
TOC

Baadhi ya wanariadha nyota wa kike wakichuana katika mbio za kilometa tano za Karatu mwaka jana

Na Mwandishi Wetu
MKUU wa wilaya ya Karatu, Omary Kwaanq anatarajia kuwa mgeni rasmi katika ufungaji wa tamasha la michezo la Karatu Jumamosi Desemba 19 kwenye Uwanja wa Mazingira Bora, imeelezwa.

Mratibu wa tamasha hilo, ambalo hufanyika kila mwaka mjini Karatu, Meta Petro alisema kuwa, mkuu huyo wa wilaya ndiye atakayetoa zawadi kwa washindi wa michezo mbalimbali katika tamasha hilo.

Baadhi ya waratibu wa mbio hizo wakijadili mambo wakati wa mbio za mwaka jana.
Alisema kuwa mbali na riadha, ambayo itashindaniwa katika mbio za kilometa 10, tano na 2.5, pia kutakuwa na michezo ya mpira wa wavu, soka, mbio za baiskeli na burudani za kwaya na ngoma.

Akizungumzia riadha, Petro ambaye aliwahi kuwa mwanariadha wa kimataifa wa Tanzania katika miaka ya nyuma alisema kuwa, wanariadha kibao nyota wamethibitisha kushiriki tamasha hilo katika mbio za kilometa 10 na tano, kwa wanaume na wanawake.
Wanariadha wa mbio za kilometa 10 za tamasha la Karatu wakijiandaa kuanza mbio za mwaka jana.
Aliwataja baadhi ya nyota waliothibitisha kushiriki mbio hizo kuwa ni pamoja na Fabian Nelson, bingwa wa mwaka huu wa Ngorongoro Marathoni Joseph Teophilo, bingwa wa Kilimanjaro Marathoni kwa wanawake, Abiola William na Bazil John.

Alisema kuwa mchezo wa soka ulianza leo Jumatano hatua ya wilaya, ambapo mshindi wa leo atacheza Ijumaa na mshindi wa kesho katika hatua ya fainali, ambapo mshindi ndiye atakuwa bingwa wa mwaka huu katika soka.
Mshindi wa mbio za kilometa tano kwa wanawake, Failuna Abdi akipewa zawadi na rais wazamani wa Riadha Tanzania, Francis John. anayeshuhudia ni mratibu wa mbio hizo, Meta Petro.
 Mbali na riadha na soka, mchezo wa mbio za baiskeli ambao huwa na msisimko wa aina yake,wenyewe utashindanisha washiriki katika umbali wa kilometa 60 kwa upande wa wanawake na wanaume.
Muandaaji wa tamasha la michezo la Karatu, Filbert Bayi (katikati), akiwa na washindi baada ya kukabidhiwa zawadi zao katika tamasha la mwaka jana mjini Karatu.

Tamasha la 14 la michezo na utamaduni la Karatu lilivyong'ara mwaka huu

December 31, 2015
TOC



Na Cosmas Mlekani, Karatu
TAMASHA la 14 la Michezo na Utamaduni la Karatu lilimaliziki mwishoni mwa wiki, huku likifungwa na Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Omary Kwaanq.
Mbali na riadha, tamasha hilo ambalo hufanyika Desemba kila mwaka, linashirikisha michezo ya soka, mpira wa wavu, mbio za baiskeli na ngoma za utamaduni pamoja na kwaya.
Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Omary Kwaanq (kulia), akienda kuanzisha mbio za kilomita 10 za Karatu. Kushoto ni mratibu wa tamasha hilo la michezo, Meta Petro na nyuma ni rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania Gulam Rashid.
Tamasha lengo kuu la tamasha hilo ni kuibua na kuendeleza vipaji kwa watoto na vijana wa Karatu na vitongoji vyake na Tanzania kwa ujumla ili kuwawezesha kutumia michezo hiyo kupata ajira.
Kwa hivi sasa michezo imekuwa ni ajira kubwa sana duniani, hivyo vijana wa Tanzania pia wanatakiwa kutumia fursa hizo kujipatia ajira kama wenzao wa nchi zingine kama Kenya, Ethiopia na hata nchi zilizoendelea kama Marekani, China na zingine.

 
Timu pia zilichuana katika mpira wa wavu katika tamasha hilo la Michezo la Karatu.
Tamasha hilo lilianzishwa miaka 14 iliyopita na bingwa wa dunia wazamani wa mbio za mita 1500 Filbert Bayi akiwa na lengo la kuibua vipaji katika mchezo wa riadha ili kupata nyota wengine wa mchezo huo hapa nchini, ambao watangara kimataifa kama alivyongara Bayi.
Kama inavyoeleweka kuwa maeneo hayo ya Karatu, Mbulu na kwingineko katika mikoa ya Arusha na Manyara kuna vipaji vingi vya wanariadha kama alivyo Bayi, lakini vinakosa watu wa kuviibua na kuviendeleza, hivyo Bayi kupitia Filbert Bayi Foundation (FBF), aliamua kuanzisha tamasha hilo.
Katibu wa Kamati ya Wanawake ya Kamati ya Olimpiki Tanzania, Nasra Juma akiigagua timu ya Karatu kabla ya kuanza kwa fainali dhidi ya Magereza.
Hatahivyo, miaka ilivyokwenda Bayi aliamua kuongeza baadhi ya michezo pamoja na vikundi vya utamaduni ili kuwaongezea vijana fursa ya kujiajiri.
Michezo iliyofuata baadae ni pamoja na soka, baiskeli, mpira wa wavu na mingine ambayo baadhi yao sasa haichezwi tena kama netiboli.
Nasra akikagua timu ya Magere, ambayo ilifungwa 3-0 katika fainali dhidi ya Karatu.
Kwa upande wa riadha mchezo huo umekuwa na msisimko wa aina yake, ambapo pia umeibua vipaji vya wanariadha wengi nyota ambao sasa wanatamba hata nje ya mipaka kama akina Fabian Joseph, Dickson Marwa, Alphonce Felix na wengineo.
Pia kwa upande wa utamaduni kumekuwa na vikundi kama vya Sangoma Mbulumbulu, ambavyo kwa njia moja au nyingine mbali na kueneza utamaduni pia hutoa ujumbe mahsusi kama ule wa gonjwa hatari la Ukimwi ili kutoa elimu kwa wananchi wa Karatu na vitongoji vyake.



 


Wachezaji wa timu ya Karatu wakishangilia kwa staili ya `Magufuli" (wakipiga pushapu baada ya kufunga bao la pili dhidi ya Magereza katika mchezo wa fainali.


Makamu mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Wavu Tanzania (TAVA), Muharami Mchume akikagua moja ya timu za wavu zilishiriki tamasha hilo la michezo la Karatu.







Sekretarieti ya tamasha la Karatu wakiwa kazini kwenye viwanja vya Mazingira Bora mjini Karatu.


Washindi wa kwanza wa baiskeli kwa upande wa wanawake ns wanaume wakiteta baada ya kumaliza mbio hizo za Karatu za kilomita 30 na 60 katika viwanja vya Mazingira Bora Karatu.
 




Usalama ulikuwa wa kutosha katika tamasha la Karatu, ambapo walikuwepo askari wa usalama barabarani, gari la wagonjwa na mgambo ili kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa kwa mujibu wa taratibu za mashindano ya kimataifa.
Pikipiki ikiendeshwa na John Mwingereza ikiongoza wanariadha wa mbio za kilomita 10.
Mwenyekiti wa Taasisi ya FBF, filbert Bayi (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Omary Kwaanq wa pili kutoka kushoto) na makamu mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Wavu Tanzania (Tava), Muharami Mchume kabla ya uzinduzi wa mbio za kilomita 10.

Mary Naali akimaliza wa tatu katika mbio za kilomita tano za wanawake za tamasha la Michezo la Karatu nyuma ya Angelina na Failuna Abdi waliomaliza wa kwanza na pili.

Lucian na Fabian Joseph Watamba Arusha Tourism Mini - Marathon

December 29, 2015
TOC


  afisa utalii wa tanapa fredy shirima akiwa
anamkabidhi  zawadi  Mwanariadha Reginal Lucian baada  ya kushinda
kilometa 42,baada ya kukimbia kwa muda wa

1:00:05

baadhi ya wanariadha walifanikiwa kupata zawadi katika shindano Arusha tourism Marathon wakiwa katika picha ya pamoja
Na Woinde Shizza,Arusha
Mwanariadha Reginal Lucian  alifanikiwa kushinda kwa upande wa
wanaume,katika shindano la Arusha Tourism Marathon baada ya  kutumia
muda wa 1:00:05,akifuatiwa na mwanariadha wa kimataifa, Fabian Joseph
1:00:14, nafasi ya tatu,Gabriel Gerald muda wa 1.00.37.

katika mashindano hayo ya kilomita 42, yaliyoandaliwa na taasisi la
Alfredo Shahanga na  Mwanariadha kutoka Kenya, Evance Kiblanget
alishika nafasi ya nne baada ya kutumia muda wa 1:07 huku nafasi ya
tano ikishinda  Wilbart Peter na nafasi ya sita akishinda mwanariadha
wa kimataifa Dickson Marwa.

Kwa upande wa wasichana  Angelina Tsere alishinda kwa kutumia musa wa
1:11:17, akifuatiwa na mwanariadha wa kimataifa  Mary Naali muda wa
1:11:23, nafasi ya tatu ulikwenda kwa Mkenya  Ladis Shemayo aliyetumia
muda wa 1:11:37 .

Katika mashindano hayo, ambayo mgeni rasmi alikuwa ni ,Afisa Michezo
wa Mkoa wa Arusha,Mwamvita Okeng'o mshindi wa kwanza hadi wa 10
walipewa zawadi.

Viongozi wengine waliotoa zawadi ni pamoja na Katibu Mkuu wa kamati ya
Olimpic Tanzania(TOC), Filbert Bayi, Rais wa zamani wa chama cha
riadha nchini(TAAA)  Franis John na Afisa  Utalii wa TANAPA Fred
Shirima.

Katika mashindano hayo, washindi wa kwanza walipoewa zawadi ta
shilingi 500,000, washindi wa pili, 250,000,washindi wa tatu, 200,000,
wanne 150,000 na wa tano 100,000 ambapo wa 6 hadi 10 pia walipewa
zawadi.

Wakizungumza wakati wa kutoa zawadi, Bayi na Okeng'o walipongeza
wanariadha waliojitokeza kwa kuonesha upinzani mkubwa na kutoa wito
mashindano haya yafanyike kila mwaka ili kusaidia kukuza utalii wa
ndani.

Mkurugenzi wa Alfredo Shahanga kwa upande wake, alisema lengo la
mashindano hayo lilikuwa ni kuhamasisha utalii wa ndani, kuhamasisha
amani mkoa wa Arusha na kutaka sasa riadha itumike kutangaza utalii.

Mashindano hayo ambayo ni sehemu ya mashindano ya Arusha Tourism
Festival ni mara ya kwanza kufanyika nchini, yalidhamiwa na shirika la
hifadhi za Taifa(TANAPA), kampuni ya vinywaji ya SBC(T) Ltd, Radio
Sunrise,BiG Expedition,Mega Trade Investment,Tanzania Breweries na
Creative Solution.

IAAF's response to allegations of blood doping in athletics

December 04, 2015
The IAAF has sent a detailed response to the allegations that it has "idly sat by" and tolerated rampant blood doping in athletics, ahead of next week’s appearance by the IAAF before the UK Parliament’s Culture Media and Sport Select Committee’s inquiry into ‘Blood Doping in Athletics’.
The document, which is now published on the IAAF website here, demonstrates that:
- The IAAF has consistently been a pioneer in the war against blood doping in sport, using every tool available to it to catch blood dopers in athletics and with considerable success.
The Athlete Biological Passport (ABP) began in 2009. The IAAF in consultation with WADA was the first sports organisation to adopt the ABP across the whole sport.

- Prior to 2009, the IAAF screened nearly 8000 blood samples for potential markers of blood doping, and followed up with thousands of urine tests to detect the presence of rEPO.
That strategy, which continues to this day, has led to 145 athletes being caught with rEPO in their systems (including Rashid Ramzi, one of the athletes highlighted by The Sunday Times), and another eight athletes (including the four Russian athletes highlighted by The Sunday Times) being caught and banned for manipulating the tests in an attempt to evade detection.
The IAAF has created ABP profiles for more than 5500 athletes, based on more than 13,000 ABP samples collected from those athletes. As a result, 56 more athletes have been caught and sanctioned for blood doping with 13 further cases pending, and 12 more currently in the pipeline. This is significantly more ABP cases than every other anti-doping organisation in the world put together. 

- ARD/The Sunday Times and their consultants cannot deny any of this. Instead, they argue that the abnormal values found in the blood screening tests conducted by the IAAF from 2001-2009 (i.e., pre-ABP) were not just indicators of potential doping that could be used to target expensive urine tests for rEPO, but instead constituted "compelling evidence" of blood doping so stating the IAAF should have charged the athletes based on that evidence alone, without the need for any further testing. 

- The IAAF fundamentally disagrees with that assertion, and it is not alone. WADA and Dick Pound, the chair of its Independent Commission, have also stated clearly and unequivocally that "no test data derived from the IAAF database prior to the adoption of the ABP in 2009 can be considered to be proof of doping. It would be reckless, if not libellous, to make such an allegation. The reported values may be suspicious and lead to targeted testing of the athletes involved, but nothing more could be done with the information". 

- In the response published today, the IAAF sets out in detail why that is correct, and why the contrary stance of ARD/The Sunday Times and their retained consultants lacks any scientific or legal basis. 
The results of testing of an athlete's blood samples are only reliable, and may only be fairly compared with the results from other samples in that athlete's profile, if all of the samples are collected in strict compliance with stringent and standardised sample collection, transport and analysis procedures. 
If not, any apparent differences in results from one sample to the next have no scientific validity. Those standardised procedures were only introduced in 2009, with WADA's adoption of the ABP programme. 
The samples collected by the IAAF before that date were not collected pursuant to those procedures.  Therefore, while they could be used to help focus expensive urine testing for rEPO on potentially suspicious athletes, they certainly could not be used as evidence of doping in and of themselves.

- Furthermore, even if the pre-2009 values had been reliable and fairly comparable with each other, deviations in those values could be caused not by blood doping but rather by innocent factors (such as altitude, exercise, medical conditions, etc.). Therefore, an abnormal value is not evidence of doping, which is a classic 'prosecutor's fallacy. 
Instead, information has to be gathered so experts can assess and seek explanations for the abnormal readings an athlete's profile. Only if they conclude that the abnormal reading is highly likely to be due to blood doping, and that no other potential explanation is plausible, can blood doping charges be brought.
But these potentially confounding factors were only fully identified when the ABP programme was adopted by WADA in 2009. Prior to that time the necessary information was not collected by anyone to enable these other factors to be assessed. 
As a result, no charge could ever be brought based on the pre-2009 data, for fear of mistaking an abnormal reading for blood doping when it could have been entirely innocent.

- Paula Radcliffe's case illustrates the point perfectly. She has been publicly accused of blood doping based on the gross misinterpretation of raw and incomplete data. When all of the necessary information is considered, however (as the WADA ABP protocols require), there are clearly plausible explanations for the values in her profile that are entirely innocent.
For example, in two of the cases highlighted by The Sunday Times, the samples were collected immediately after competition (when dehydration causes a decrease in plasma concentration, and so an increase in reported haemoglobin concentration, even though there has been no increase in red blood cells).
Any competent scientist would therefore immediately conclude that they should be disregarded.  Furthermore, the IAAF followed up by testing Ms Radcliffe's urine samples for rEPO, and her blood samples for evidence of blood transfusions, and all of those tests came back negative. 
The IAAF is not complacent about doping in its sport. It will continue to use every tool at its disposal to fight doping and protect clean athletes, and hopes that investigative journalists will continue to assist it by unearthing evidence of cheating for it to follow up. 
The IAAF also acknowledges the important role of the media in holding it and other anti-doping organisations to account in their efforts to fight doping. 
The IAAF cannot sit idly by while public confidence in its willingness to protect the integrity of its sport is undermined by allegations of inaction/incompetence that are based on bad scientific and legal argument. Instead it has both a right and an obligation to set the record straight
---
The IAAF will respond separately to the allegations in the report issued by the Independent Commission on 9 November 2015, that high-ranking officials at or associated with the IAAF corruptly delayed the prosecution of up to eight ABP cases in 2012, thereby allowing certain athletes to compete at the London Olympics who should instead have been provisionally suspended from the sport. 

Bid process opened for reallocation of 2016 IAAF events

December 04, 2015
An accelerated bidding process has been opened today for the reallocation of two 2016 IAAF World Athletics Series competitions, with the decisions due on 7 January 2016.
Following confirmation last week of the full suspension of the Russian IAAF Member Federation ARAF, the process is now underway to reallocate the 2016 IAAF World Race Walking Team Championships (Cheboksary, RUS) and 2016 IAAF World U20 (Junior) Championships (Kazan, RUS) which were originally awarded to ARAF.
IAAF Member Federations have been formally invited to submit applications to host these two events, it being understood that this will be an accelerated process to ensure maximum time available for the successful hosts to organise these two championships.
TIMELINE (for both events)

7 December 2015: Member Federations interested in this opportunity are to submit a Letter of Interest signed by the Member Federation and the authorities of the proposed Host City.

7 December 2015: IAAF sends Application Form and additional documentation to Member Federations submitting a Letter of Interest.

10 December 2015: Conference Call for candidates (IAAF to provide supplementary information and to answer questions).

22 December 2015: Completed Bid Applications to be submitted to the IAAF.

23 December 2015 to 6 January 2016: Review of Applications by the IAAF.

7 January 2016: Electronic vote by the IAAF Council on Host Venue. Successful candidate city announced.
 

Copyright © 2015 - 2025 Athletics Tanzania All Right Reserved

Developed by Gadiola Emanuel
Theme By AP | Developed By Gadiola Emanuel